Skip to main content

KATIBU MKUU WEMA ASISITIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

 

 


 

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, DAR-ES-SALAAM@@@@

 

KATIBU Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said amesema, ili kupata taifa lenye maendeleo na wataalamu wabobevu, kila mmoja anapaswa kuekeza mapema kwa watoto.

 

Akifunga mafunzo ya siku nne kwa waandishi wa habari wa Zanzibar, kuhusu makuzi, malezi na maendeleo ya awali ya mtoto, alisema kuwa waandishi wanapaswa kutumia kalamu zao vizuri kuibadlisha jamii na kuwa yenye kutekeleza malezi bora kwa watoto.

 

Alisema kuwa, kila mmoja anapaswa kuekeza mapema kwa mtoto, hivyo ni jukumu la wanahabari kuhakikisha wazazi wanafuata utaratibu mzima wa malezi na makuzi bora ya watoto kwa kuwapatia lishe bora, afya imara, kuwapa nafasi ya kujifunza mapema na kuwa nao karibu, hali ambayo itawajenga kuwa na kipaji kikubwa ambacho kitawaleta mabadiliko chanya.

 


"Tusipokuwa na wataalamu tutachelewa kupata maendeleo, hivyo tuanze kumkuza mtoto katika malezi bora kuanzia, kwa ajili ya kujenga taifa imara," alieleza Katibu huyo.

 

Aidha aliwataka waandishi wa habari watetee kwa sauti kubwa ili watoto wapate haki zao za msingi kwa mustakbali wa maisha bora ya baadae.

 

Kwa upande wake Mtaalamu wa Programu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kutoka UNICEF Alinune Nsemwa, alieleza kuwa ni muhimu kuiwezeha jamii kuhakikisha wanatoa huduma bora katika makuzi ya awali ili watoto wa Tanzania wafikie utimilifu wao.

 

"Asilimia 47 tu ya watoto Tanzania wamekuwa kwa utimilifu lakini asilimia 53 wanahitaji wakue na kufikia utimilifu, hivyo ni jukumu letu kuhakikisha tunatoa elimu ipasavyo ili tufukie malengo, " alieleza.

 


Nae Meneja wa Huduma za Jamii Zanzibar (ZPDB) Dk. Ibrahim Byatike Kabole alifafanua kuwa, mafunzo hayo yanasaidia sana katika ukuwaji wa watoto ikiwa waandishi wa habari watakiwa mstari wa mbele kutoa elimu kwenye vyombo vyao, kwani wao ni sauti ya wasio na sauti.

 

"Malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ni muhimu sana kwa ajili ya kujenga taifa bora, kwa hiyo waandishi tunawaomba mutumie kalamu zenu vizuri ili jamii iwelewe umuhimu wa kumlea mtoto katika malezi bora," alieleza.


 

Mkurugenzi Mtendaji wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Kenethic Simbaya alisema kuwa, kuwaelimisha waandishi wa habari ni kuweka msingi imara ambao utaleta mafanikio ya baadae, hivyo Umoja huo umeona ni muhimu kuungana na Serikali kuhakikisha suala la ECCD linapewa kipao mbele.

 




Meneja wa Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar Bakar Hamad Magarawa alisema, wataendelea kuwajengea uwezo wanajamii na kuonyesha changamoto zinazowakabili kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi, ili kusudi waboreshe malezi ya watoto wao.

 

Mafunzo hayo ya utangulizi kuhusu utelekezaji wa Programu Jumuishi ya Zanzibar ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto Zanzibar, yameandaliwa na UTPC kwa kushirikiana na Zanzibar Presidential Delivery Bureau pamoja na Zanzibar Mult-Sectoral (ECCD) kwa ufadhili wa Shirika la UNICEF Zanzibar pamoja na Big Win UK.

                              MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...