Skip to main content

UZINDUZI WA PROGRAMU YA ECD ZANZIBAR: UTPC yawanoa waandishi wa habari visiwani, 'Jamii yatakiwa kuzingatia malezi na makuzi bora kwa watoto wao'

 

            

 




IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ 

 

KILA tuamkapo asubuhi, wazazi wengi wana tabia ya kukimbilia sehemu zao za kazi kuliko kumkimbilia mtoto wake aliepo nyumbani.

 

Lakini hii ni kwa sababu watoto huchelewa kuamka ndipo mama huona ni bora kumuacha amalize usingizi wake, huku akijua hatoonana nae kwa masaa tisa baadae.

 

Inasikitisha sana kuona kwamba wazazi wa zama hizi hawana muda wa kuwashughulikia watoto, hawachezi nao na wala hawawajengei mazingira bora ya kumfanya achangamke kiakili na kukua vizuri.

 

Ingawa hili linaenda kupatiwa muarubaini baada ya UTPC kwa kushirikiana na Zanzibar Presidential Delivery Bureau pamoja na Zanzibar Mult-Sectoral (ECCD) kuwapa mafunzo wanahabari kwa ufadhili wa Shirika la UNICEF Zanzibar pamoja na Big Win UK.

 

Ni mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuelimisha jamii na kuripoti habari mbali mbali zinazohusiana na malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto Zanzibar.

 


David Gisuka ambae ni Mtaalamu wa Sayansi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Tanzania hakuwa nyuma kuwanowa wanahabari ili kusudi jamii ipate uelewa wa kumlea mtoto katika amazingira bora.

 

Anasema, wazazi wanasahau majukumu yao ya kumlea mtoto na kuona kwamba, jukumu lao ni kumpa chakula tu huku wakisahau majukumu mwengine muhimu kwa watoto wao.

 

Anachambua kuwa, watoto wanaanza kujifunza tangu pale mimba inapotungwa, hivyo ni wajibu wa kila mzazi kuwatunza watoto, kuwapatia lishe bora, kuhakikisha wanakuwa na afya njema, kumpa fursa ya kujifunza mapema na kumshirikisha katika mambo mbali mbali, ambayo yatamsaidia kukua vizuri na kuimarika kiafya.

 

"Elimu ya malezi na makuzi bora ya watoto inahitajika katika jamii yetu, ili kuhakikisha wazazi wanalea watoto wao katika malezi yaliyobora, kwa sababu wengine hawaelewi umuhimu wa malezi bora kwa watoto na wanaoelewa basi wanapuuza", anaeleza.

 


Madhara ya kumlea mtoto katika malezi yasiokubalika ni makubwa sana kwani humuathiri katika maisha yake yote na hatimae jamii husema... mtoto huyo amepotea, kumbe alikosewa katika malezi ya awali.

 

Anasema, kuna baadhi ya wazazi wana tabia ya kushughulikia zaidi kazi zao na kuwaacha watoto wao wakiwa wapweke, hali ambayo inawasababishia udumavu wa akili na kimwili.

 

"Watoto wanahitaji ukaribu wa wazazi wao ili kujifunza mambo mbali mbali ambayo yatawajenga kiakili, kwa sababu akili ya mtoto tangu akiwa tumboni mpakani siku 2000 baadae ni kama sponji, unapoliweka litafyonza, hiyo anachokiona ama kukisikia ni lazima atajifunza,"

 

Hivyo ni vyema wakawatengeneza kujifunza mambo yaliyobora ambayo yatawajenga kiakili kwa manufaa bora ya maisha yao ya baadae.

 

Wazazi wanatakiwa kuekeza mapema kwani siku 2000 kwa mtoto hujifunza kwa asilimia 90 huku asilimia zilizobaki hujifunza akiwa mkubwa, hivyo unapomkosea mtoto katika malezi ya awali, basi unakosea kumjengea maisha mazuri ya baadae.

 


"Mtoto anapozaliwa anakuwa na asilimia 25, anapotimiza miaka mitatu anakuwa na asilimia 80 na anapofikia miaka mitano huwa ana asilimia 90 ambazo ni sawa na siku 2000, hivyo ni muhimu kwa wazazi kujitahidi kwenye malezi kwa siku hizo, kwa sababu asilimia chache iliyobaki ndio anayotumia akiwa mkubwa," anaeleza 

 

Mkurugenzi wa taasisi ya Makuzi na Malezi Bora ya watoto Zanzibar (MECP-Z) Sharifa Suleiman Majid anasema, watoto wanahitaji kutunzwa, kupatiwa lishe bora, kuwa na afya njema, kucheza pamoja na kutengenezewa mazingira mazuri ya kuishi.

 

"Kuna baadhi ya wazazi hujitia pirika nyingi mpaka wakakosa muda wa kuwashughulikia watoto wao, jambo hili ni hatari katika maisha yao ya baadae kwa sababu mtoto anajifunza zaidi kuanzia pale mimba inapotungwa hadi miaka mitano kwa asilimia 90, hivyo iwapo atakosa malezi bora hatokuwa vizuri," anafafanua.

 

Mkurugenzi Sharifa anawasisitiza wazazi kuwapa watoto wao fursa ya kuzungumza na kuwasikiliza, ili wawe huru kusema chochote kinachowakabili katika maisha yao.

 

Anasema, namna unavyomlea mtoto wako siku 1000 (asilimia 80) ama siku 2000 (asilimia 90) baada ya kuzaliwa ndipo anapoweza kukua vizuri kimwili na kiakili huku akirithi tabia za wazazi kwa asilimia 50 na asilimia 50 zilizobaki hujifunza kwenye mazingira yaliyomzunguka.

 


"Ujifunzaji wa mtoto huanza kabla ya kuzaliwa, hivyo anahitaji lishe bora, kujifunza mapema, kumjengea mahusiano mazuri kati yake, wazazi na jamii iliyomzunguka," anafafanua.

 

Dk. Ibrahim Byatike Kabole ambae ni Meneja Huduma za Jamii (ZPDB), anawaambia waandishi wa habari kutumia kalamu zao vizuri kwa ajili ya kuwaelimisha wanajamii juu ya umuhimu wa malezi na makuzi bora ya watoto.

 

"Tushirikiane kuhakikisha kila mzazi anapata uelewa wa kutosha kuhusu malezi bora ya watoto, hili litasaidia watoto kukua vizuri na kuwa na ufahamu wa hali ya juu," anasema.

 

Anaeleza, mafunzo hayo yatasaidia sana katika ukuwaji wa watoto ikiwa waandishi wa habari watakuwa mstari wa mbele kutoa elimu kwenye vyombo vyao, kwani wao ni sauti ya wasio na sauti.

 


Dk. Kabole anaeleza kwamba malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ni muhimu sana kwa ajili ya kujenga taifa bora, hivyo waandishi wachukue jitihada za makusudi kuhakikisha kila mwanajamii anapata uelewa.

 

Kennethic Simbaya yeye ni Mkurugenzi wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) anasema, wanahabari wana jukumu la kuielimisha jamii juu ya malezi na matunzo ya watoto, kufanya hivyo kutalisaidia taifa kupata wataalamu wabobevu hapo baadae.

 

Anasema, kuwaelimisha waandishi wa habari ni kuweka msingi imara ambao utaleta mafanikio ya baadae, hivyo UTPC umeona ni muhimu kuungana na Serikali kuhakikisha suala la ECD linapewa kipao mbele.

 


Mtaalamu wa Programu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kutoka UNICEF Alinune Nsemwa anasema, ni muhimu kuiwezeha jamii kuhakikisha wanatoa huduma bora katika makuzi ya awali ya mtoto wa Tanzania ili wafikie utimilifu.

 

Anafafanua, asilimia 47 tu ya watoto wa Tanzania ndio ambao wamekuwa kwa utimilifu na asilimia 53 wanahitaji wakuwe na kufikia utimilifu, hivyo ni jukumu la kila mmoja kwa nafasi yake kutoa elimu kwa jamii ili lengo walilolikusudia lifikiwe.

 


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdulla Said anasema, ili kupata taifa lenye maendeleo na wataalamu wabobevu, kila mmoja anapaswa kuekeza mapema kwa watoto.

 

"Kuekeza mapema ni kupi? Ni kuhakikisha tunampatia malezi bora mtoto wetu tangu siku ya kutunga mimba kwa kumpatia lishe bora, awe na afya njema, tuhakikishe tunampa fursa ya kujifunza mapema na mazuri kutoka kwetu na mazingira yaliyomzunguka, tumpe fursa ya kucheza na tuwe nao karibu," anafahamisha Katibu huyo.

 

Anasema, nchi isipokuwa na wataalamu itachelewa kupata maendeleo, hivyo ni muhimu kumkuza mtoto katika malezi bora kuanzia akiwa tumboni, jambo ambalo litawajenga kuwa na kipaji kikubwa ambacho kitawaleta mabadiliko chanya katika maisha yao.

 


Bakar Hamad Magarawa ambae ni Meneja wa Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar anasema, wataendelea kuwajengea uwezo wanajamii na kuonyesha changamoto zinazowakabili kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi, ili kusudi waboreshe malezi ya watoto wao.

 

"Akinababa pia wawe makini wakati wa ujauzito wa wake zao kwa sababu mtoto anasikia kila kitu na anaanza kujifunza pale, hivyo ikiwa atakosa lishe bora au atakosa furaka pamoja na kuwa na msongo wa mawazo kuna hatari ya kuzaa mtoto ambae atakuwa na changamoto ya udumavu," anafahamisha.

 

Meneja Mradi wa Programu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Zanzibar Maryam Issa anasema, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Afya imeamua kuongeza nguvu katika malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto.

 

"Licha ya Serikali kuboresha huduma za afya imeona kuna haja kubwa ya kuongeza nguvu katika makuzi z malezi na maendeleo ya awali ya mtoto kuanzia umri wa zero (0) hadi miaka nane (8) ili kuwa na watoto wenye afya bora ya kimwili na kiakili," anafafanua Meneja huyo.

 

Mafunzo hayo ya utangulizi kuhusu utelekezaji wa Programu Jumuishi ya Zanzibar ya Malezi, Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Zanzibar, yaliyowashirikisha waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya Zanzibar ambayo yamefanyika katika Ukumbi wa hoteli ya Jamirex jijini Dar-Es-Salaam.

 

                                      MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...