Skip to main content

MAKAMU WA PILI AIPA KAZI WIZARA, KUENDELEZA, KUKUZA, KULINDA UTAMADUNI


 NA KHAULAT SULEIMAN, SUZA@@@@

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, amesema kua Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, inajukumu la kuhakikisha wanalinda mila, silka na asili ya Zanzibar, kwa kuona kua ni fursa kwa wananchi na serikali kwa ujumla. 

Ameeleza hayo kwenye Tamasha la Utamaduni wa mswahili wa kipemba, jana August 25, 2024 lililofanyika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema wakati umefika sasa kwa Wizara hiyo, kwa kuweka taratibu mbali mbali ambazo zitaihamasisha jamii, kuendeleza kulinda na kuuenzi utamaduni wa Zanzibar. 




"Wizara  mnatakiwa kua wabunifu, ili kuendelea kuongeza watalii na pato katika nchi, mnatakiwa kutoa elimu katika jamii, kwamba utalii sio wa kutembea uchi, kwani ni fursa ambayo inasaidia kuleta maendeleo yenye kulinda heshima na utamaduni,''alisema.

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mudrik Ramadhani Soraga, amempongeza Afisa Mdhamin Zuhura Mgeni Othman kwa kuona ipo haja ya kuandaa matamasha ambayo yatasaidia kuikumbusha jamiii kuendeleza mila na tamaduni zao. 

"Dhamira ya matamasha haya, ni kufungua fursa za uwekezaji na utalii, ambazo zitapatikana kisiwani Pemba, tumejionea jinsi utajiri uliopo hapa, katika kuenzi utamaduni, kisiwa cha Kojani wamejitahidi sana bado ule msukumo namna gani, utakua wa kivutio na kua fursa katika jamiii,''alieleza. 

"Ni tamasha la kwanza hili, lakini limeakisi yale kuliyoyatarajiwa kuyafikisha katika jamiii, kua ipo haja ya kuenzi utamaduni wetu, kwani ni wa kipekee ambao tunao na kuendelea kuwa nao. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib amesema jamii, ipo haja ya kuunga mkono juhudi za serikali, katika kuikumbusha jamiii juu ya kuenzi mila, silka, asili ya watu wa Pemba, kwa kuandaa matamasha mbali mbali. 

"Tumeona kwa sasa, jamii ilivyo na mporomoko wa madili, hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu anathamini utamaduni wake, ili kuwa wa upekee, kujivunia juuu ya utamaduni huo. 

Mapema Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Rahimu Mohamed Bhaloo, alieleza kua serrkali kwa sasa imekua kwa kasi kikubwa, katika sekta ya utalii, kwa kuona zaidi ya wageni 600,000 wanaitembelea Zanzibar. 


"Tunaona jitihada mbali mbali katika sekta ya utalii, zinachukuliwa ili kuhamasisha wageni na wenyeji kujionea utalii wetu wa Zanzibar, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuunga mkono, jitihada hizo ili tuweze kupata maendeleo katika nchi yetu. 

Afisa Mdhamin Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Pemba, Zuhura Mgeni Othaman, amewashukuru viongozi mbali mbali na wananchi, katika kumuunga mkono kwa kuandaa matamasha, ambayo yataikumbusha jamiii, pamoja na kuwavutia wageni kufika katika kisiwa cha Pemba.




Aidha ameyahidi kuyafanyia kazi yote ambayo wameagizwa na serikali, ili kuhakikisha sekta ya utalii, inazidi kuleta maendeleo na mchango mkubwa, katika kuingiza na kukuza pato la nchi. 

Tamasha hilo la mswahili wa kipemba, lilianza kwa matembezi yake kwa shughuli kadhaa, ikiwemo gari za ng'ombe na mitindo mbali mbali ambayo yanalengo la kuenzi utamaduni wa kipemba.
                                          mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan