Skip to main content

UKUZAJI VIPAJI VYA WANAFUNZI WA KIKE SKULI YA UWELEWENI, WAELEWA NA CHUNGU YA CHANGAMOTO

 

NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

MPIRA wa kikapu ‘basketball’ ni aina ya mchezo unaochezwa sehemu nyingi  duniani.

Kwani kama ilivyo michezo mingine, nao huimarisha afya, huleta ajira, huondosha ubaguzi, na kuunganisha watu wa aina mbalimbali.

Mchezo huu ni wa pili kwa umaarufu, baada ya mpira wa miguu kwa kupendwa na mashabiki wa michezo nchini, ambao wengi walicheza skulini na kupata wafuasi wengi.

Kwa mujibu wa umoja wa Mataifa, mchezo huu ulianzishwa na Mwalimu James Naismith, kwenye chuo cha Springfield College huko, Massachusetts mwaka 1891.

Alibuni mchezo huu kwa ajili ya wanafunzi wake, ili wapate mazoezi wakati wa kipupwe waliposhindwa kucheza nje, ambapo kwa mara ya kwanza, ulichezwa Disemba 21 mwaka huo huo 1891 nchini Berlin.

Mpira wa kikapu, ulienea haraka ndani na nje ya vyuo vya Marekani, katika karne ya 20, ambapo mwaka 1936 mchezo huu ulikubaliwa kwenye michezo ya Olimpiki.

Shirikisho la mpira wa kikapu duniani ‘FIBA’ na chombo cha usimamizi wa mpira huo duniani, linakadiria kuwa takriban watu milioni 450 duniani, wanacheza mchezo huo.

Kwa vile mchezo huu uliibuliwa kwa ajili ya wanafunzi, skuli ya Sekondari ya Uweleni Mkoani Pemba, nayo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha lengo linatimia.

Skuli hiyo yenye timu mbili ya wanawake na wanaume, imekuwa ikifanya vizuri na imeshachukuwa ushindi mara nne mfululizo, katika sherehe za elimu bila malipo Zanzibar, kwa wanaume.

Ingawa wanawake wanashikilia ushindi kwa Pemba, na kwenye fainali huishia ushindi wa pili, ingawa kwa hali zao si haba.

Licha ya timu ya wanawake ya ‘basketball’ skuli ya Uweleni kufanya vyema, bado inakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa uwanja.

Akizungumza na makala haya, kocha wa basketball wa timu ya wanawake wa skuli ya sekondari ya Uweleni, Mohamed Salim Khamis (Gabs) anasema, kutokuwa na uwanja maalum kwa wanafunzi wa kike, hasa katika hatuwa za awali.

Uwanja mmoja ambao wanacheza wanaume, ndio huo huo wanaochezewa na wanawake, huku ukiwa sehemu ya uwazi ni jambo linalowapelekea watoto wa kike kujiskia aibu.

 

“Nna uhakika kama tutapata uwanja wa kufanyia mazoezi uliostara kwa watoto wa kike, tutachukuwa nafasi ya kwanza kwenye fainali, bila wasiwasi kama tunavyochukuwa kwa wanaume,”anasema kocha.

Akizungumzia vipaji vya michezo kwa watoto wa kike skulini hapo vipo hasa katika mchezo huo wa basketball ila linalowarejesha nyuma ni uwanja pekee.

Anaelezea kutokuwa na uwanja maalum wa watoto wakike ndio kunakowatia hofu jamii na wazazi kushiriki watoto wao katika michezo na kusema ni uhuni.

Mwalimu anaeshughulikia michezo Skuli ya sekondari Uweleni Abdulla Ali Abdalla anasema asilimia kubwa ya watoto wa kike skulini hapo wanapenda michezo hasa wa basketball, ila wazazi hawaridhii kutokana na mchanganyiko wakati wa ufanyaji wa mazoezi.

JUHUDI ZA SKULI KUENDELEZA BASKETBALL KWA WANAWAKE

Mwalim Abdul anasema ni pamoja na kuwashajihisha wanafunzi wa kike kushiriki katika michezo, hatimae kuwa na utayari wa wanafunzi wenyewe kutokana na mapenzi ya mchezo huo.

Nyingine ni kuwapongeza wanafunzi wa michezo kila mwaka na kuwapa zawadi waliofanya vizuri zaidi, pamoja na kuzungumza na wazazi kuhusiana na umuhimu wa michezo kwa watoto wa kike na jinsi unavyowadhibiti na vishawishi vibaya.

WANAFUNZI WA KIKE

Maimuna Fatawi Khamis anasema kushiriki kwake katika mchezo huo kumemletea faida ikiwemo ya kuimarisha afya, kutembea sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi pamoja na kupata zawadi.

“Mimi nishakwenda baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, hadi nimefika nchi ya Uganda, kupitia michezo  hujiuliza kwa hali ya kawaida ningefikaje,”anasema kwa bashasha.

Fatma Masoud Kombo, anasema kwa vile michezo ni ajira baada ya kumaliza skuli, ataweza kujiajiri kupitia michezo bila ya kusubiria serikalini.



“Pamoja na maneno mengi nnayoambiwa kama michezo kwa wanawake haina tija, haisaidii lakini sikubali kwani wapo wanawake wengi ‘wamewini’ kupitia michezo,”anasema.

Nasra Ali Sheha anasema, licha ya kutokuwa na uwanja wa kufanyia mazoezi ya mchezo basketball, lakini anaendelea na ataendelea kufanya vizuri.

“Wapo wanafunzi wenzetu wanatuonea choyo na wanataka kuingia katika michezo, ingawa wanakatazwa kwao wanaambiwa michezo ni uhuni,”anasema bila hofu.

 

 

MIKAKATI YA SKULI

Msaidizi Mwalimu mkuu skuli ya sekondari Uweleni Khamis Mohamed Ussi, anasema baada ya kukaa pamoja na uongozi wa walimu wa michezo, wameamuwa kutengeneza goli moja nyuma ya skuli yao, ili wanafunzi wa kike wafanye mazoezi.

Anasema, ijapokuwa goli hilo ni la kienyeje ‘local post’  lakini linawasaidia, kiunyonge hasa ukianagalia mchezo huo unahitajika kuchezwa kwenye sakafu, ila wao wanacheza kwenye vumbi.

‘’Ilitubidi tuunde, tuwaze maarifa hayo, kwani bila ya hivyo ni shida kwa watoto wa kike kufanya mazoezi pamoja na wanaume,”alisema.

 WAZAZI

Subira Mohamed, anasema mwanzo hakuwa tayari mtoto wake wa kike kuingia katika michezo, ingawa baada ya kuelimishwa na walimu kuhusu faida yake, alikubali.

“Kilichonifanya nikatae mwanangu kuingia michezoni ni uchezaji wa pamoja, kati yao na wale wa kiume, jambo hilo si zuri kiutamaduni,”anasema.

 


Hashim Abdalla Ali, lazima tukatae wazazi maana kama wameamuwa kuchezesha mpira huo kwa watoto wa kike, wangewaekewa uwanja wao mbali, usiotumiwa na wanaume.

Said Omar Ali, anasema ni jukumula serikali kupitia wizara husika, ni kujenga viwanja vya michezo kwa watoto wa kike ili kufanyia mazoezi katika skuli ya Uweleni, linazingatiwa.


“Tulikuwa tushakataa watoto wa kike wasiingie katika michezo, lakini baada ya kuitwa na waalimu na wakatupa faida ya michezo kwa vijana wetu wakike, nikakubali,”anasema.

TAMWA ZANZIBAR                                                                                      

Afisa mradi wa kukuza usawa wa kijinsia na ujumuishi kwenye michezo Khairat Haji, anasema baada ya kuona watoto wa kike wako nyuma katika sula la michezo.

Ndipo chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar kupitia mradi wa michezo kwa maendeleo, imeona ipo haja ya kushirikiana na vyombo vya habari kuibuwa changamoto za aina hiyo.



Anasema, ni kweli watoto wa kike wako nyuma katika ushiriki wa michezo, na kuwataka waandishi wa habari kuhakikisha, wanatumia kalamu zao kulisemea jambo hilo, ili kuondokana na mawazo finyu.

Anasema lengo la mradi wa michezo kwa maendeleo unaodhaminiwa na shirika la maendeleo la kimataifa la Ujerumani, ambao unatekelezwa na jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’, kituo cha majadiliano kwa vijana ‘CYD’ ni kuhakikisha wanawake wanashiriki katika michezo, kwa hali ya kuridhisha.



‘Kwa vile kila mtu anayo haki ya kushiriki michezo, kwa nini wanawake wabakie nyuma na tutahakikisha usawa wa kijinsia unapatikana katika michezo,’’alisema.

 

WIZARA HUSIKA

Mkuu wa divisheni na utamaduni kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mzee Ali Abdalla, anasema ni vyema  walimu wakuu wachukuwe nafasi zao, kuweza kujenga viwanja vidogo vidogo, ili watoto wa kike wasikatishe michezo yao.

Anasema watoto wakipata uwanja wa karibu, wataweza kuvutiwa zaidi, kwani akili ya mtoto bora ni ile inayojengwa na kiwiliwili bora, ambapo ni kupitia michezo ni sehemu moja wapo.

KANUNI ZA MCHEZO HUO

Shabaha ya mchezo ni kushinda vikapu vingi kuliko timu nyingine, na mpira unaotumiwa kimataifa ni mpira wa ngozi au ‘mata sintetiki’, wenye kipenyo cha milimita 749 hadi 780 na uzito wa gramu 567 hadi 650.

Uwanja huwa na vipimo vya mita 28 kwa 15 ambapo wakati wa mchezo huwa kuna marefa 2-3 uwanjani wakati kando ya uwanja hukaa waamuzi wengine wanaoshika wakati na miniti za magoli na makosa.

                                        MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan