Skip to main content

TIGO-ZANTEL WAUMIMINIA MILION 350 MFUKO WA WANAOANGUKA MIKARAFUU

 


 HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MTANDAO wa simu za mkononi wa Tigo-Zantel, umechangia shilingia milion 350, kwenye mfuko wa fidia kwa ajili ya wananchi wanaopatwa na hasara ya kuanguka mkarafuu, wakati wanapoliokoa zao hilo.

Hafla ya kukabidhi fedha hizo, kupitia mfano wa hundi, lilifanyika leo Augost 27, 2024 ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake Pemba, kwenye hafla pia ya kuwakabidhi zawadi wakulima bora wa karafuu, waliokubali fedha zao za malipo kupitia Tigo pesa.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mfano huo wa hundi, Mkurugenzi wa mtandao wa simu wa Tigo- Zantel Aziz Said Ali, alisema huo ni mwanzo kwa Tigo-Zantel, kuwachangia wanoanguka mikarafuu.



Alieleza kuwa, mtandao wa simu, kila siku umekuwa ukijali mno ubinaadamu na maendeleo yao, na ndio maana, wamevutika mno kutoa shilingi milioni 350, kwa ajili ya kuutunisha mfuko huo.

Aidha, mtandao huo wa simu katika hafla hiyo, iliwakabidhi wakulima 25 zawadi za simu, baiskeli na piki piki, kwa baadhi yao waliopokelea fedha za mauzo ya karafuu kwa njia ya Tigo pesa.

‘’Hawa wakulima 25, kati yao watatu wamekabidhiwa baiskeli mpya na wawili ambao ni washindi wamekabidhiwa piki piki na wengine wamekabidhi simu janja,’’alifafanua.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo wa Tigo-Zantel, alisema watalifanyia kazi ombi la Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Omar Said Shaaban, wa kuweka zawadi ya gari kwa washindi, kwa msimu ujao.

Mapema Waziri huyo, alipongeza hatua ya Tigo-Zantel, moja kuwatunuku zawadi wakulima hao 25, na kisha kukabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 350, kwa ajili ya mfuko wa fidia kwa wanaoanguka mikarafuu.



''Niwaagize wenzetu wa ‘ZSTC’ kufanya mazungumzo na Benki ya watu wa Zanzibar ‘PBZ’, nao kuiga mfano wa Tigo-Zantel kwa kuuchangia mfuko huu,’’alieleza.

Eneo jingine, Waziri huyo alitumia nafasi hiyo kuwashawishi wakulima, kuacha kiliasfirisha nje ya nchi, kwa njia ya magendo zao la karafuu, na badala yake wakimbilie ‘ZSTC’ kwa kuliuza.

‘’Kwa wananchi wanaotaka kulisafirisha zao la karafuu, waje ZSTC kununua, na watapewa vibali maalum, ambavyo kisha watakuwa huru kulisafirisha watakapo,’’alifafanua.

Hata hivyo Waziri huyo, aliwataka wakulima hao, kuendelea kupokelea fedha zao za malipo ya karafuu, kwa mtandao wa tigo pesa, kwani salama zaidi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Taifa la Biashara Zanzibar ‘ZSTC’ Soud Said Ali, alisema wameshajipanga kwa msimu huu wa mwaka 2024/2025 kuzinunua karafuu kwa mfumo wa kisasa.



‘’Mkulima sasa atakuwa anaona karafuu zake zinavyopimwa, atapokea idadi ya kilo, daraja na fedha zake za kuuzia hata kabla hajatoka ndani ya kituo cha mauzo,’’alieleza.

Akiwasilisha mfumo huo, Mkuu wa ‘TEHAMA’ kutoka ‘ZSTC’ Najma Nuhu, alisema hatua ambazo mkulima atazipitia kabla ya kupokea malipo yake ni tano, katika mfumo huo wa kisasa.

‘’Kwanza ni usajili, ambao utathibitishwa na cheti, kupewa daraja la karafuu zake, hatua ya tatu ni kuchungwa, upimaji na hatua ya tano ni kupokea malipo kupitia ujumbe mfupi wa simu yake,’’alifafanua.



Hata hivyo, alisema mchakato huo wote, kwa muuzaji mmoja wa karafuu, hautarajiwi kumaliza dakika moja, kuanzia usajili hadi kupokea ujumbe wa malipo yake.

Badhi ya wanufaika wa zawadi hizo, akiwemo Hamad Khalid Hamad, aliyeshinda piki piki, alisema amefurahishwa na mpango huo wa Tigo-Zanztel, kwani sasa ana uhakika wa safari.







Nae Kombo Ali Mussa, aliyepata zawadi ya baiskeli, alisema hakuamini kuwa, engewa miongoni mwa washindi, kwani alikuwa anapokelea malipo yake kupitia tigop pesa, bila ya kushindana na mtu.

                                       Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan