Skip to main content

‘CHAPO’ YAPATA MKURUGENZI MPYA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

ALIYEKUWA Mratibu wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, amechaguliwa kwa kura za ndio, kushika nafasi ya Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo, iliyokuwa wazi.

Mahamed Hassan, ambae hakuwa na mpinzani katika uchaguzi huo mdogo na wa dharura, alijizolea kura 15 kati ya kura zote 17 zizopigwa na wanachama wa CHAPO.

Akitoa matokeo hayo leo Augost 31, 2024, Makamu Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya 'CHAPO' Hafidh Abdi Said, alisema wapiga kura wote, walitarajiwa wewe 23, ingawa hadi muda wa kupiga kura unafika kulikuwa na wajumbe 17 pekee.



Alieleza kuwa, kwa mujibu wa katiba ya CHAPO, imeanisha idadi ya wajumbe wote, ni kufikia nusu, ili kufanya uamuzi iwe wa uchaguzi ama kupitisha ajenda.

‘’Idadi ya wanachama hai 17, kati ya 23 haijakikua katiba ya 'CHAPO' na ndio maana, tumefanya zoezi la uchaguzi na mshindi ambae ni Mohamed Hassan Aballa, kwa nafasi ya Mkurugenzi ameshinda,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Makamu huyo Mwenyemiti wa kamati ya uchaguzi, alisema kati ya wapiga kura wote 17, kwa bahati nzuri hakuna hata kura moja, iliyoharibika.

‘’Kabla ya kumtangaaza mshindi wetu, niwapongeze wanaCHAPO kwa kuendesha zoezi la upigaji kura, bila ya kuwepo hata kura moja iliyoharibiki,’’alieleza.

Mapema kabla ya kuanza kwa uchaguzi huo, Makamu huyo Mwenyekiti, aliwataka wapiga kura na utulivu wa hali ya juu, ili kulikamilisha zoezi hilo, kwa amani.


Akizungumza mara baada ya kupatikana kwa Mkurugenzi huyo mpya, Mjumbe wa bodi ya wadhamini ya ‘CHAPO’ Zuwena Hamad Ali, alimtaka Mkurugenzi huyo, kuondoa mipasuko ndani ya Jumuiya.

‘’Sasa uchaguzi umekwisha, hakuna haja tena ya mipasuko, makundi na kilichombele yako, ni kuwaunganisha wanajumuiya, ili kazi iendelee,’’alieleza.


Aidha Mjumbe huyo wa bodi, alisema hawatofurahishwa kusikia wapo wasaidizi wa sheria ni wa wavivu, hawapendi ushirikiano kwani, mwisho wake ni kuidhoofisha CHAPO.

‘’Tujitahidi sana, kwani malalamiko sio silaha ya kufikia mwafaka, bali watu wafanye kazi, kisha changamoto ndio njia ya kuelekea mafanikio,’’alieleza.

Kwa upande wake Mkurugenzi fedha wa ‘CHAPO’ Riziki Hamad Ali, alisisitiza haja kwa wanachama hao, kupita kila wakati ofisini hapo, na sio kwa ajili ya mikutano pekee.


Mwanachama wa ‘CHAPO’ Mashavu Juma Mabrouk, alisema njia ya kufikia malengo yao, ni kushrikiana na uongozi mzima wa CHAPO, kwa kila hatua.

Nae Ali Salim, alisema kilichopo mbele ya wanachama wa CHAPO kwa sasa, ni kuongeza juhudi za kazi, ili wananchi wasione tofauti, kati ya alipokuwepo Mkurugenzi aliyepita na sasa.


Msaidizi wa sheria Khadija Said Khalfan, alimtaka Mkurugenzi huyo mpya, kuwaunganisha watu wote, ili iwe rahisi kufanikisha mipango na mikakati yao.



Marehumu Nassor Bilali Ali, ambae alifariki August 7,2024 alikuwa uwanja wa ndege wa Pemba, kwa safari ya matibabuni kisiwani Unguja, ambapo alifariki papo hapo na kuzikwa kijijini kwao Vinguni wilaya ya Chake chake Pemba siku hiyo hiyo.

                     

             mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan