Skip to main content

EU YAJA NA MRADI WA KIJANI PEMBA KUIMARISHA HUDUMA KWA WANANCHI

 




IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis amesema, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itahakikisha inasimamia vyema utekelezaji wa mradi wa Kijani (SASA) Pemba utakaoimarisha ustahamilivu wa mazingira, ambao unalenga kuleta mageuzi ya upatikanaji wa huduma bora nchini.

Alisema kuwa, mradi huo utasaidia upatikanaji wa maji safi na salama, kufanya ukarabati wa maskuli 19 na ukarabati wa vituo vya afya kumi (10), kuwawezesha wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuwapatia mafunzo na mikopo nafuu, kuwasaidia akinamama wanaolima mwani pamoja na usimamizi wa usafi wa mazingira katika miji.

Akizindua mradi huo katika Uwanja wa michezo Madungu Chake Chake Waziri huyo alisema kuwa, ni vyema mradi wa Kijani (Green and Smart Cities Programe) utekelezwe kwa haraka, ili wananchi wanufaike kwani ni muhimu sana kwao.

‘’Tuhakikishe mradi huu tunautekeleza kwa malengo tuliyoyakusudia na Serikali inaendelea kuthamini michango ya washirika wa maendeleo wa ndani na wa nje wakiwemo Umoja wa Ulaya (EU) na kuahidi kushirikiana ili kufanikiwa zaidi,’’ alisema Waziri.



Alisema kuwa, EU umeshatoa misaada mbali mbali ya utaalamu, kifedha na nyenzo tofauti katika nchi, ambapo tangu mwaka 1975 wameshashachangia zaidi ya Euro bilioni mbili kwa maendeleo ya nchi ya Tanzania kupitia miradi mbali mbali.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za SMZ Mikidad Mbarouk Mzee alisema, mikataba miwili ya ruzuku kwa ajili ya mabadiliko ya mradi wa Kijani (SASA) katika vitongoji vya miji ya Pemba vyenye jumla ya misaada ya Euro milioni 75 ambazo zitatumika katika mradi huo unaolenga kuimarisha ustahamilivu wa miji.

‘’Tunaishukuru EU kwa msaada wa fedha mbali mbali za uchumi wetu ikiwemo katika maeneo ya uchumi wa buluu na mabadiliko ya hali ya hewa, udhibiti na mageuzi ya taasisi, mpango wa ukuaji wa mitaji kwa wajasiriamali kwenye masuala ya kilimo na utawala, ukusanyaji wa takwimu za jinsia na udhibiti wa kazi za nishati,’’ alisema Naibu huyo.



Nae Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib alisema kuwa, wamaefarajika sana kupata mradi huo na kueleza kuwa watashirikiana na kuunga mkono jitihada hizo kwa kufanya usimamizi na ufuatiliaji.

Mapema Mkurugenzi wa Mradi huo Martino Vinci alisema, mradi huo unalenga kuboresha miundombinu ya mijini, kuimarisha huduma za msingi kama vile usimamizi wa maji safi na taka na kuibua fursa za kiuchumi kwa vijana, wanawake pamoja na biashara ndogo ndogo katika sekta ndogo za kilimo cha mwani na kuchakata taka.

‘’Nina furaha sana ya kusherehekea pamoja nanyi katika uzinduzi wa miradi hii na ninasisitiza kuwa dhamira yetu ya kufikia matokeo chanya yataonekana hivi karibuni,’’ alieleza.

Mtekelezaji wa mradi huo kutoka shirika la misaada la Ubelgiji (Enabel) Koenraad Goekint alifahamisha kuwa, mradi huo utaboresha ufanisi wa kazi katika taasisi zenu, mazingira mnayoishi na maisha ya familia zenu, watoto, vijana na wanawake.

‘’Katika mwaka mmoja au miwili ijayo tunatarajia kuona skuli zikiwa na hali bora kwa watoto, jamii zikiwa na maeneo ya umma yaliyoboreshwa, upungufu wa taka, usambazaji bora wa maji na usafi wa mazingira,’’ alifahamisha.



Mkurugenzi wa shirika la OIKOS Mary Birdi alifafanua ushirikiano unahitajika katika miradi inayotekelezwa, kwani itawasaidia wananchi mbali mbali na kuboresha miundombinu.

Balozi wa EU nchini Tanzania Christine Grau alisema kuwa, hiyo ni fursa muhimu kwa wananchi wa Pemba itakayowasaidia kuwa na mazingira bora na hewa ya kuvutia.

Mradi huo unaoendeshwa na Wizara ya Nchi Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za SMZ chini ya Ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU), unatekelezwa katika mikoa ya Tanga Mjini, Mwanza na kisiwani Pemba.

                                               MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan