Skip to main content

HAROUN: 'KITUO CHA UTATUZI MIGOGORO ZANZIBAR KIVUTIZI KWA WAWEKEZAJI'



 

NA FAKI MJAKA, AMM -ZANZIBAR@@@@

 

Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Mh. Haroun Ali Suleiman amesema kuanzishwa kwa Sheria ya Usuluhishi na Kituo cha Utatuzi wa Migogoro Zanzibar kutaongeza imani ya wawekezaji kuja nchini kuwekeza miradi yao ya kimaendeleo.

 

Amesema kituo hicho kitakapoanzishwa kitawahudumia wenyeji na wageni na hivyo kupunguza kasi ya watu kuepelekana mahkamani hasa pale migogoro ya kibiashara na uwekezaji inapotokea.

 

Waziri Haroun aliyasema hayo huko katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege alipofungua Mkutano wa Wadau uliojadili Rasimu za Miswada ya Sheria ya Usuluhishi na Sheria ya kuanzisha Kituo cha Usuluhishi wa Migogoro Zanzibar uliohudhuriwa na wadau kutoka sekta mbali mbali nchini.

 

Alisema hali ya Zanzibar kiuchumi inaimarika sana kutokana na juhudi zinazochukuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi za kuwavutia Wawekezaji kuwekeza miradi yao ya kiuchumi Zanzibar.

 

Alisema suala la uwekezaji linahitaji pia kuwa na sheria nzuri ili kuwavutia wengi zaidi kuja kuwekeza nchini na kuleta tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

 

Alifahamisha kuwa, waligundua kwama, Sheria iliyopo kwa sasa ya utatuzi wa migogoro imepitwa na wakati na hupelekea migogoro mingi ambayo huchukua muda mrefu na gharama kubwa mahkamani.

 

Alisema Serikali kwa makusudi imeamua kuanzisha Kituo maalum cha usuluhishi wa migogoro ambacho kitakuwa na jukumu la kuipatia ufumbuzi migogoro itakayojitokeza.

 

“Badala watu kupelekana Mahkamani panapotokea mgogoro sasa watu watakuwa wanaenda katika kituo hicho kwa ajili ya kutafuta suluhu, na imani yetu watakaokwenda kituoni watatoka hapo kila upande ukiwa umeridhika” Alifafanua Waziri Haroun.

 

Aliongeza kuwa, Kituo hicho kitakuwa chini ya Mwenyekiti wake (atakayeteuliwa na Rais), ambaye pia atakuwa na jukumu la kutumia busara kwa kushirikiana na Wajumbe wake kuitatua migogoro itakayofikishwa katika kituo hicho.

 

“Ukweli ni kwamba Wawekezaji hupenda mazingira salama ya uwekejazi wao. Wanapopelekwa mahkamani, huvunjika moyo na kutafuta nchi nyingine zenye mazingira rafiki ya uwekezaji wao, ili yasifikie hayo Kituo hiki kitakuwa kichocheo cha kuwaongezea Imani na usalama wao” Aliongeza Waziri Haroun.

 

Akitoa historia ya chimbuko la uwamuzi huo, Waziri Haroun alisema, Rais Dkt. Mwinyi baada ya kuingia madarakani aliagiza sheria zote zilizopitwa na wakati zifanyiwe marekisho au kufutwa na kutungwa upya. Miongoni mwa Sheria hizo ni sheria ya usuluhishi ambayo ilitungwa toka zama za wakoloni mwaka 1926 hivyo ni wajibu kufutwa ili kuendana na hali halisi ya sasa.

 

Akizungumza katika Mkutano huo, Mwanasheria Mkuu Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji alisema ni muda muafaka wa Zanzibar kuwa na kituo chake cha usuluhishi wa migogoro hasa kutokana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Nane ya kushajihisha Uchumi wa Buluu na uwekezaji wake.

 

Alisema Rasimu mbili zilizokuwa zinajadiliwa zitatoa Dira muhimu na mustakabi mwema wa Zanzibar ambapo shughuli za uwekezaji zitakapoongezeka, zitawanufaisha wananchi kwa ujumla wake.

 

Alifahamisha kuwa, kiutaratibu Rasimu hiyo itapelekwa katika kamati ya uongozi ya Wizara na baadaye kikao cha Makatibu wakuu kabla ya kupelekwa Baraza la Wawakilishi kwa hatua za kujadiliwa zaidi.

 

Amesema kukamilika kwa Sheria na Kituo hicho cha usuluhishi kutachochea imani zaidi kwa wawekezaji kwamba Zanzibar ni sehemu nzuri ya uwekezaji na hivyo kupelekea kutekeleza dhamira ya Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kuifungua Zanzibar kiuwekezaji hasa katika uchumi wa Buluu.

 

Akichangia katika mkutano huo, Mwenyekiti mstaafu wa tume ya kurekebisha sheria Zanzibar ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Jaji Mshibe Ali Bakari amesema moja ya faida ya Kituo hicho ni kuipunguzia mzigo mkubwa Mahkama kwani migogoro mingi itapatiwa ufumbuzi katika kituo hicho badala ya mahkamani.

 

Kwa upande wake Rais mtaafu wa Jumuiya ya Mawakili Zanzibar na Wakili wa kujitegemea Slim said Abdala amesema uzoefu unaoenesha kuwa migogoro ya kibiashara na uwekezaji haitakiwi kwenda katika Mahkama za kawaida, bali hupelekwa katika Vituo vya usuluhishi.

 

Amesema Kituo cha usuluhishi ni sehemu muafaka zaidi kwa vile ni maamuzi hutolewa kwa haraka zaidi na kwa ufanisi bila kuvutana katika mahkama kunakochukua muda mrefu na gharama kubwa.

 

Wakili Slim aliahidi kuwa wapo tayari kuunga mkono kituo hicho ambacho ana Imani kitazidi kuchochea kasi ya uwekezaji na maendeleo nchi.

 

 

mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch