Skip to main content

TAMWA -ZNZ: 'SHERIA MPYA YA HABARI, MWANGA WA KUWATOA WOGA WAANDISHI WA HABARI'



NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanzibar Dk Mzuri Issa amesema kuwepo kwa Sheria mpya ya habari inayokwenda sambamba na maendeleo ya Sayansi na teknolojia itatowa fursa kwa waandishi wahabari kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Akitowa taarifa kwa vyombo vya habari amesema pamoja na kuwepo maoni mengi yaliyotolewa na waandishi wahabari pamoja na wadau na watetezi wa haki za binadamu kuhusu mabadiliko ya sheria ya zamani iliodumu kwa takribani muongo mmoja bado kunahitajika kuwepo kwa sheria rafiki inayokwenda na wakati wa sasa.

Dk Mzuri amewapongeza wadau mbali mbali walioshirikiana na vyombo vya habari ikiwemo Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata haki yao ya msingi ya kupata habari kama inavyosema Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 18, pamoja na Mikataba ya Kikanda inayosimamia uhuru wa vyombo vya habari nchini.

“Wakati tunaingia mwaka mpya 2024 waandishi na vyombo vya habari wana matumaini makubwa ya kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili katika utendaji wao wa kazi,” Dk Mzuri.

Akizitaja sheria zinazohitaji kufanyiwa marekebisho amesema ni pamoja na Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu no 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria no 8 ya mwaka 1997 pamoja na sheria ya Utangazaji no 7 ya mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho na sheria no 1 ya mwaka 2010.

“Tuna hamu ya kupata Sheria mpya kwa kupitia kauli na matamshi ya Viongozi wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiongozwa na Rais na Waziri mwenye dhamana ya habari ambae alieleza wakati wa kutimiza siku mia moja lakini kwa bahati mbaya hadi leo Sheria hizo hazijarekebishwa,” Dk Mzuri.

Mapema Afisa Mradi wa Uhuru wa habari kutoka TAMWA,Zanzibar Zaina Mzee amesema kwa miaka mingi Sheria hii ya habari imekuwa kikwazo kwa waandishi wahabari na vyombo vya habari kwa ujumla kufanya kazi kwa ufanisi.

Akiwasilisha mada Mshauri Elekezi kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU) Said  Suleiman Ali katika mkutano uliwashirikisha wadau wa habari amesema Sheria ya Habari ina mapungufu mengi amabayo yanahitaji kufanyiwa marekebisho ya haraka kwa lengo la kuisaidia jamii.

“Uhuru wa habari si wa waandishi pekee, ni wa jamii nzima, kwani ukimnjima uhuru mwandishi kutekeleza majukumu yake ipasavyo na utainyima jamii fursa ya kupata habari,” Said Suleiman Ali ((Z).

Akiwasilisha Ripoti ya Uchambuzi wa Sheria ya Habari Zanzibar Juma Abdalla amesema Sheria ya habari inahitaji maboresho makubwa kwa sababu inaonekana kuwa na vikwazo kadhaa vinavyorejesha nyuma maendeleo na ufanisi kwa waandishi wa habari.

“Sheria ina mapungufu mengi na waandishi wanailalamikia kwa muda mrefu hivyo tunaomba irekebishwe kwa faida ya waandishi na kwa jamii,”

Nao wadau wa habari walikutana kujadili masuala ya Sheria hizo wametowa maoni yao kwa kusema Sheria hiyo imelalamikiwa kwa takribani miaka kumi na mitano tokea 2010 hadi leo haijafanyiwa marekebisho.

Salim Said Salim  Mwandishi Mwandamizi amesema kwa ulimwengu wa sasa wa Sayansi na Teknologia ipo haja ya kuwa na Sheria zinazomlinda mwandishi wahabari na kuleta tija kwa jamii

“Kwa sababu kuna sheria zimeeleza adhabu kubwa kwa mwandhishi wahabari endapo atafanya kosa, sheria kama hizo zinakwamisha waandishi na kupelekea kufanya kazi zao kwa woga,” Salim Said.

Shifaa Said kutoka Baraza la Habari Tanzania Zanzibar amesema waandishi wahabari kushirikiana kwa pamoja kujadili changamoto zinazojitokeza katika sheria hizo na kuendelea kuzifanyia uchambuzi na kuishauri Serikali kuzitafutia ufumbuzi  kwa sababu ni za mda mrefu.

Mradi wa kuimarisha masuala ya uhuru wa habari wa miaka miwili wenye lengo la kuendeleza mapitio ya uhuru wa Sheria za habari (ARFEL), Unaofadhiliwa na Common Wealth Foundation.

  

 

 

 

   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch