Skip to main content

KESI TUHMA YA KUUA KWA MAKSUDI PEMBA: 'PP HATUJAMALIZA MAELEZO YA MASHIDI KWANZA'

 


NA MARYAM NASSOR, PEMBA @@@@

 WATUHUMIWA wa kesi ya kuua kwa  makusudi, inayowakabili vijana wanne akiwemo Yassir  Mussa Omar ‘Makababu’ na wenzake , wote wakazi wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake,  wameendelea kusota rumande, baada ya upande wa mashtaka, kushindwa kukamilisha maelezo ya kesi na mashahidi kwa wakati.

Mara baada ya watuhumiwa hao kuwasili mahakamani hapo wakitokea rumande, Mwendesha Mashtaka kutoka  Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Pemba, Mohamed Abdallah Juma, alidai kutokamilisha kwa baadhi ya mambo muhimu.

 Alimueleza, Jaji wa Mahakama kuu Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa, kesi hiyo ipo mahkamani hapo kwa ajili ya kutajwa, ingawa bado maelezo ya shauri hilo hayajakamilika.

“Mheshimiwa Jaji leo (jana), kesi hii ipo kwa ajili ya kutajwa,  lakini bado hatujakamilisha maelezo ya  kesi na mashahidi , hivyo tunaomba utupangie tarehe nyengine kwa ajili ya kutajwa tena,”alidai.

Baada ya maelezo hayo, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar kanda ya Pemba, Ibrahim Mzee Ibrahim, alimuuliza wakili wa upande wa utetezi, Saleh Said Mohamed kuwa ana pingamizi yoyote, juu ya ombi hilo.

 Wakili huyo alidai kuwa, hana pingamizi yoyote juu ya ombi hilo, ila aliuomba upande wa mashtaka kujihimu  kukamilisha maelezo ya mashahidi, ili watuhumiwa hao wajuwe hatma yao.

“Mimi sina pingamizi na ombi la upande wa mashtaka, ila nawaomba wajihimu kukamilisha maelezo hayo, ili watuhumiwa hawa wajuwe hatma ya kesi inayowakabili,’’alidai.

Jaji wa mahakama hiyo, aliwauliza upande wa mashtaka kuwa, lini watakuwa wameshakamilisha maelezo ya kesi na mashahidi na kujibu kuwa wanahitaji wiki mbili.

Jaji huyo alisema kuwa, upande wa mashtaka wanatakiwa kukamilisha hayo yote ifikapo Febuari 5, mwaka huu na mahakama iwaite jopo la wazee wa mahakama, ili kushirikiana nao kwa  kesi hiyo.

Kwa mara ya kwanza shauri hilo, lilisomwa mahakamani hapo Novemba 14 mwaka 2023, na kughairishwa kwa kutokana na kutokuwepo kwa Jaji wa mahakama kuu.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo, na Mwendesha Mashtaka kutoka O fisi ya Mkurugenzi wa mashtaka kuwa, watuhumiwa hao Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwar Mussa Omar miaka 30, na Ali Mussa Omar ‘Mkapa’ miaka 29, kwa pamoja wanadaiwa kumuua kwa makusudi, kijana Said Seif Kombo.

Ilidaiwa kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16 mwaka 2023, baina ya majira ya saa 7:00 mchana na saa 11:00 jioni, katiak eneo la Machomanne wilaya ya Chake chake, mkoa wa kusini Pemba.

Kufanya hivyo ni kosa, kinyume na vifungu vya 179 na 180 vya sheria namba 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar, iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

Kesi hiyo rasmi, imeghairishwa Febuari, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa tena mahakamani hapo na watuhumiwa wamerejeshwa rumande.

                                      MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...