Skip to main content

JAMII YAKUMBUSHWA KUILINDA HAKI KUU YA BINAADAMU


 


NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@

JAMII imekumbushwa kuwa, moja ya haki kuu ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni kosa kwa mtu mwengine yeyote kumuondolea mwenzake.

Hayo yalielezwa na mtoa mada mwanasheria kutoka Shirika la Msaada na Haki za Binaadamu Siti Habib Mohamed, wakati akiendesha mafunzo ya siku nne kwa waandishi wa habari, wadau wa habari na wasaidizi wa sheria, yanayofanyika Chuo cha Amali Vitongoji Chake chake na kuandaliwa na Mwemvuli wa asasi za Kirai Pemba PACSO kwa ufadhili wa UNDP.

Alisema kua zana ya haki za binadamu ilianzishwa mnamo  mwaka 1948 baada ya vita vya kwanza vya dunia, hivyo ni wajibu wa kila mmoja hadi leo hii, kuhakikisha anailinda na kuitetea haki ya kuishi ya mwanzake.

Alieleza kuwa, haki za binadamu kimsingi ni yale madai au haki zote ambazo anadai binamu mara baada ya kuzaliwa, na kwa kawida hakuna taasisi yoyote ambayo inaweza kuzuia.



‘’Ni kweli haki ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha anailinda yake mwenyewe na mwenzake,’’anaelkeza.

 Hata hivyo alieleza kua kupitia Mkataba wahaki za  binadamu ambao uliasisiwa mwaka 1966 na kuanza kufanyaka kazi mwaka 1976, umeanisha haki nyingine kadhaa za binadamu kama vile kutoa maoni.

Katika hatua nyingine mtoa mada huyo alieleza kua zipo hatua mbali mbali, ambazo zimekuja kwa ajili ya kuzilinda haki hizo ikiwa ni pamoja na kuanzishwa wizara maalum, kuanzishwa kwa tume ya Haki za binadamu na utawala bora.

‘’Lakini hata kuingizwa kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na ile ya Zanzibar ya mwaka 1894 na uwepo wa wizara husika na asasi ni sehemu ya kuzilinda,’’alifafanua.

Mapema Mkurugenzi wa PACSO Mohamed Najim Omar, alisema waliona wakutane na waandishi wa habari, wanaharakati wa haki za binadamu na wasaidizi wa sheria, ili kuwajengea uwezo.

‘’Waandishi wananafasi kubwa ya kuhakikisha wanakemea matendo ya uvunjifu wa haki za binadamu kupitia kazi zao,’’alieleza.



Washiriki wa mafunzo hayo walisema bado elimu inahitajika kwa jamii, ili wafahamu athari za uvunjifu wa haki za binadamu.

Mshiriki kutoka chama cha ACT Wazalendo Saleh Nassor Juma, waliishukuru taasisi hii ya PACSO kwa kuwapa mafunzo hayo, ambayo yamewapa uwelewa zaidi.

Nae mtaangazaji wa Redio Istiqama Pemba Bakar Khamis Juma, alisema kama mataifa makubwa, yatajenga utamaduni wa kuziheshimu haki za binadamu dunia itakuwa salama.

Nao washiriki Abubakar Mohamed Ali ,Mwache Juma Abdalla walisema, kama vyombo vya habari vitakuwa huru kufanya kazi, wanaweza kukemea matendo ya uvunjifu wa haki za binadamu yanayojitokeza.

Mratibu wa miradi kutoka Shirika la Maendeleo Ulimwenguni la UNDP Gamalick Sun  alisema wataendelea kuiunga mkono PACSO katika shughuli zao mbali mbali.



Alieleza kuwa, anaamini PACSO ni sehemu ya uwakilishi wa wananchi, na ndio maana hata mafunzo hayo yamewashirikisha watu wa kada mbali mbali.

Mafunzo hayo ya siku nne mada kadhaa zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na uhuru wa kujieleza, haki za binaadamu, majukumu ya waandishi wa habari na jukumu la jamii katika kulinda haki za binaadamu,.

                   Mwisho  


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch