Skip to main content

TAMWA-ZANZIBAR YATOA RAI WAKATI WA UANDAAJI SERA, SHERIA

 


NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar Dk. Mzuri Issa  Ali ameishauri Serikali pamoja na Taasisi binafsi kuandaa Sera na Sheria za nchi kwa kuzingatia usawa na jinsia zote ili kuwepo usawa wakati wa teuzi mbali mbali zinazofanywa.

Akizinduwa waraka maalumu naoainisha changamoto zinazowakumba wanawake na watu wenye ulemavu katika kugombea nafasi za Uongozi hafla iliyofanyika Ofisi za ukumbi wa bima Mperani mjini Unguja.

Dk.Mzuri amesema kwa miaka mingi wanawake na watu wenye ulemavu wamekosa nafasi muhimu katika ngazi za maamuzi jambo ambalo linawanyima haki yao ya msingi ya kidemokrasia ya kutoa mawazo yao na uhuru wa kujieleza.

“Elimu ndio ngazi kubwa ya kuwapeleka wanawake katika Uongozi kwa miaka mingi iliyopita walinyimwa fursa ya elimu na baadhi ya wazee ama walezi kutishwa na kuwa na dhana potofu ya kuharibiwa watoto wao katika masuala ya udhalilishaji na kwa bahati mbaya fursa hizo kupata wanaume pekee,”  alisemai.

Aidha Dk. Mzuri ameiomba Serikali pamoja na Mrajisi wa vyama vya siasa kutoa ufafanuzi wa kina kuhusiana na vitimaalum licha ya kwamba nafasi hizo zimesaidia wanawake kujifunza masuala ya siasa kivitendo na kujenga weledi katika Uongozi.

“Viti maalum vimesaidia kuwainuwa wanawake wengi kujiamini na kujifunza katika Bunge na Baraza la Wawakilishi ila muda mwengine vinafaidisha wachache mpaka wengine wanaitwa malkia wa viti maalum (Qeens of special Seat), hivyo miaka mitano inatosha kujifunza,” alieleza DkMzuri.

Mapema akiwasilisha waraka huo maalum Mkurugenzi kutoka Jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar (ZAFELA)  Jamila Mahmoud amesema katika warakahuo wamewasilisha baadhi ya Sheria zinazowakwaza wanawake na watu wenye ulemavu zinazoonekana kupitwa na wakati kwa mazingira ya sasa.

“Tunatakauwepo sheria zinazozungumza wazi na kumlazimisha mtu yeyote kuhakikisha katika kila nafasi ya Uongozi, mwanamke anapewa nafasi sawa na mwanamme,” alifafanua Mkurugenzi huyo wa  ZAFELA.



Amesema baadhi ya Sera na Sheria zilizopo kwa sasa zinamapungufu hivyo endapo zitafanyiwa marekebisho zitaleta mabadiliko katika makundi maalum pamoja na wanawake katika kufikia usawa wa hamsini kwa hamsini katika ngazi za maamuzi.

Nae Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake wenye Ulemavu  Zanzibar (JUWAUZA) Salma Saadat amesema ipo haja ya kufanya utetezi wa pamoja ili kutoa nafasi ya ujumuishaji wa watu wa makundi maalum kushiriki katika nafasi za Uongozi.

“Mpaka sasa kwenye Baraza la Wawakilishi tuna wajumbe watatu tuwe wenye ulemavu jambo ambalo linaonesha kuwa bado ushiriki wao ni mdogo hivyo kukosa ujumuishi na ushiriki wao kikamilifu katika upatikanaji wa haki zao,”alisema Salma Saadat Haji.

Aidha Mkurugezi wa Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira Pemba (PEGAO) Hafidh Abdi Said amesema jamii inahitaji Amani na Utulivu pamoja na mshikamano kwa watu wote hivyo muda umefika kwa wanawake kupewa nafasi za Uongozi kwa sababu historia inaonyesha wanawake hufanya vizuri katika eneo hilo.

Nao wanawake wenye nia ya kugombea nafasi za Uongozi wamesema wamefarajika kupewa mafunzo yanayohusu Uongozi na Kuiomba Serikali kuzichukuwa changamoto zilizowasilishwa katika waraka huo na kuzifanyia kazi kwa vitendo ili kuleta mabadiliko nchini.


Baadhi ya Sheria zilizotajwa zinazoweka vikwazo ni pamoja na Sheria ya Ushirikishwaji katika Siasa (Perticipation of Political Party), Sheria ya Uchaguzi (Election Act)  No 4,2018, Sheria ya Utumishi wa Umma ( Public Service),No 2,2011, Zanzibar Civil Status Regulation Agency Act No 3,2018.

Waraka huo maalum umetayarishwa kwa pamoja na  Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA,ZNZ), JumuiyayaWanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya utetezi wa Mazingira Pemba (PEGAO) na Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA) wanaotekeleza kwa pamoja mradi wa kuwajengea uwezo wanawake kugombea nafasi za Uongozi (SWIL) unaofadhiliwa na Ubaloziwa NORWAY.

 

mwisho 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch