Skip to main content

WAANDISHI WA HABARI, WASAIDIZI WA SHERIA, WATETEZI HAKI ZA BINAADAMU WAAHIDI KUIFIKIA JAMII PEMBA

 



ASHA ABDALLA NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@


WAANDISHI wa habari, wasaidizi wa sheria na watetezi wingine wa haki za binadamu kisiwani Pemba, wamesema baada ya kumalizika kwa mafunzo ya siku nne, sasa wako tayari kuisaidia jamii, namna bora ya kuzilinda haki za binaadamu.

Walisema kazi iliyofanywa na Mwemvuli wa asasi za kirais Pemba ‘PACSO’ kwa kushirikiana kwa na Shirika la kimaendeleo ulimwengini ‘UNDP’ ni jambo jema na lililobakia ni wao kuwafikia wananachi.

Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo, yaliyofanyika ukumbi wa Chuo cha Amali Vitongoji Chake chake, walisema wamepata elimu ya kutosha kwa ajili ya kuifikisha kwa jamii.

Watetezi hao wa haki za binaadamu walisema, PACSO na UNDP wameshatimiza wajibu wao kwa kuwapa mafunzo hayo, sasa kilichobakia kwao wao, ni kuhakikisha wanakutana na makundi kadhaa ndani ya vijiji mbali mbali.

Mmoja kati ya washiriki hao Mwalimu Mwache Juma Abdalla, alisema kazi iliyoko mbele yao ni kukutana na makundi kama vile wanafunzi, watu wenye ulemavu, wanasiasa na vijana kuwapa elimu hiyo.

Nae mtetezi wa haki za binaadamu Saleh Nassor Juma, alisema mafunzo hayo yamewafikia wakati mwafaka, kwani kwa sasa kunamatendo kadhaa ya uvujifu wa haki za binaadamu.

‘’Kwa mfano watoto na wanawake wamekuwa wakidhalilishwa kingono, kiuchumi, kisiasa, kielimu na hata kijamii, sasa ni wajibu wetu sisi baada ya mafunzo haya kuwafikia,’’alieleza.



Nae msaidizizi wa sheria kutoka wilaya y Micheweni Said Salum alisema watayatumia majukwaa ya wasaidizi wa sheria wenzao, kuhakikisha elimu hiyo inasambaa wilaya nzima.

‘’Ni kweli haki za binaadamu zinavunjwa wakati mwingine na vyombo vya serikali na kwa kiasi kikubwa jamii yenywe, sasa tutahakikisha elimu tuliyoipata hapa inaenea,’’alifafanua.

Mwandishi wa kituo cha redio cha ZENJ Fm Radhia Abdallah na mwenzake wa Muyaba Kombo wa Redio jamii Micheweni walisema, wataandaa vipindi, makala fupi fupi ili kuielimisha jamii madhara ya uvunjifu wa haki za binaadamu.

Hata hivyo mwandishi wa ITV na redio One Pemba Suleiman Rashid amewataka waandishi wa habari wenzake, kufanya utafiti wa kina wa habari zao za haki binaadamu, ili siwaachie wengine maumivu.

Mtaalamu wa mawasiliano ya umma kutoka Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Gaspary Charles, alisema mwandishi wa habari bora ni yule anayesikiliza kero za wananchi na kuziripoti, na sio kujiandikia habari mwenyewe.

Katika hatua nyingine mtoa mada huyo, alisema haki za binaadamu zinauwanja mpana, hivyo waandishi wanajukumu la kuhakikisha wanawaelimisha wananachi.   



Akifunga mafunzo hayo Mwenyekiti wa Mwenvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamd Ali Khamis, aliwataka washiriki hao, kuyafanyia kazi mafunzo hayo, ili lengo la kuomba mradi huo lifikiwe.

Alieleza kuwa, ilikuwa vigumu kwa PACSO kuwakusanya wananchi na watetezi wote wa haki za binaadamu kisiwani Pemba, hivyo waliopata nafasi hiyo wawe na hamu ya kuwapa elimu hiyo wenzao.



Mafunzo hayo ya siku nne mada kadhaa zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na uhuru wa kujieleza, haki za binaadamu, majukumu ya waandishi wa habari na jukumu la jamii katika kulinda haki za binaadamu,.

                                           Mwisho                                                                       

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...