Skip to main content

KUSINI WAONGOZA KWA UVAMIZI WA ARDHI- SMZ

 

 




 


                 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

  

Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar imesema kumekua na uvamizi pamoja na uuzaji holela wa maeneo ya ardhi ya akiba kitendo ambacho kinachangia ongezeko la migogoro ya ardhi Zanzibar.

Kauli hiyo imetolewa jana na waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali alipokutana na Masheha wa Wilaya ya Kusini Unguja, kikao maalum kilichofanyika ofisi za Mkuu wa Wilaya hiyo alisema   kumekua na uvamizi na uuzaji holela wa maeneo ya ardhi ya akiba yaliyotengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Waziri Rahma alisema Wizara yake itahakikisha inaweka mikakati imara ya udhibiti wa uuzaji ardhi kiholela hasa katika maeneo ya ardhi ya akiba yaliyotengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Aidha alieleza kwamba Wilaya ya Kusini Unguja inaongoza kwa uvamizi na uuzaji wa  ardhi kiholela hasa katika maeneo ya fukwe za bahari yiliyopo wazi  hivyo kutokana uwezo wa wizara yake kupewa dhamana ya usimamizi wa ardhi kwa mujibu wa tangazo la kisheria Nam 137 ya Mwaka 2020 itahakikisha inayadhibiti maeneo hayo.

“ Wilaya ya kusini Unguja  inaongoza kwa uvamizi na uuzaji wa maeneo kiholela hasa maeneo ya fukwe na yaliyo wazi  hivyo kwa vile Wizara yangu ndio iliyopewa dhamana ya usimamizi wa ardhi kwa mujibu wa sheria nitahakikisha ninayadhibiti maeneo hayo na atakaebainikia kwenda kinyume hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake” Alisema waziri huyo.

Hivyo  Waziri huyo amewataka masheha hao kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika usimamizi wa masuala ya ardhi pamoja na kufanya kazi zao ipasavyo kwa kutojihusiha na vitendo vya uuzaji wa ardhi bila kufuata sheria zilizowekwa.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mzee Ali Haji alitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya ardhi kwa wageni ambapo alisema kwa mujibu wa Sheria ya ardhi Nam.12 ya mwaka 1992 imekataza kuuziwa ardhi mgeni yeyote bali atatakiwa kukodishwa kwa ajili ya uwekezaji na sio vyenginevyo.

Kwa upande Mkurugenzi Mipango Miji na Vijiji Kutoka Kamisheni ya Ardhi Muchi Juma Ameir alisema tayari Kamisheni ya Ardhi  imeyaainisha  maeneo yote yenye ardhi ya akiba yaliyoko katika Mkoa wa Kusini Unguja yakiwemo Paje, Muungoni,na Muyuni kwa lengo la kuyapanga na kuyapima kwa kuyawekea alama na  kuyadhibiti ili yasiweze kuvamiwa kwa uuzaji wa viwanja kiholea .

Kwa upande wa mashe Shehia ya paje Mohammed Rajabu Makame alisema kuwa  kwa kiasi kikubwa wanasheria ndio wanaohusika na masuala ya ukiukwaji wa sheria kwa kufanya vitendo hivyo na hata wao kuwakosesha ufanisi mzuri wa kiutendaji hasa katika kazi zao za usheha.

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Kusini Rajab Mkasaba alimkaribisha waziri huyo na kuwataka masheha kuwa mabalozi wazuri katika kutoa elimu kwa jamii juu ya umiliki wa ardhi katika shehiya zao.

Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kujadili na kuweka mipango mikakati  ya usimamizi madhubutu ambao utasaidia kuondoa changamoto ya uuzaji wa ardhi kiholela  pamoja na kupunguza migogoro ya ardhi nchini.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch