Skip to main content

MADEREVA PEMBA WAKERWA NA WANAFUNZI WANAOPUUZA HONI

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA::

MADEREVA wa vyombo vya moto kisiwani Pemba, wamewataka wanafunzi wa skuli, kutodharau honi wanazowapigia au mingurumo maalum ya mshine, ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika.

Walisema, wanafunzi waliowengi wamekuwa na tabia ya kudharau honi au mivumo isiyokuwa na kawaida, wanayoifanya ili wakae pembeni, jambo ambalo linaweza kuleta madhara.

Wakizungumza na mwandishi wa habari eneo la Ngwachani, ambapo dereva mmoja aliyekataa kutaja jina lake, alipoteremka kwenye gari, kuwaeilimisha wanafunzi waliodharau honi aliyowapigia mara tatu.

Alisema, alilazimika kuweka gari pembeni, na kuwapa maneno makali kundi la wanafunzi, baada ya kuwapigia honi na mivumo mikali ya mashine, bila ya kujali.

Dereva huyo alieleza kuwa, alikuwa amebeba mzingo akitokea bandarini Mkoani, na alipofika karibu na njia ya Tangaani, aliwapigia honi wanafunzi, ili wakae pembeni, ingawa hawakutii.

‘’Mbele yangu kuna gari mbili za abiria zinafukuzana zikitokezea mjini Chake chake, na upande wangu kuna kundi la wanafunzi kama 15, niliwapigia honi chaajabu, hakuna hata mmoja aliyegeuka nyuma,’’alisema.

Kwa upande wake dereva Ali Omar Ali wa gari ya Chake chake-Mkoani, alisema wanafunzi wenye tabia hiyo, hasa ni wa skuli zenye sekondari na zaidi wale wa kike, ndio ambao wameuwa wakidharau honi.

‘’Wale skuli za msingi ukiwapigia honi au gari ukiibadilisha mvumo wanakaa pembeni haraka, lakini hawa wakubwa ni wajeuri na wakati mwengine, inatubidi sisi tuwakwepe wao,’’alieleza.



Kwa upande wake dereva wa gari ya abiria, Hussein Kassim Omar alisema, kisheria wanafunzi wanapotembea iwe kwenda ama kurudi skuli, wavielekee vyombo vya moto na siku kuvipa mgongo.

Mwanafunzi mmoja Nassor Haji Ali, alisema kinachojitokeza ni kutokana na kukosekana kwa miundumbinu rafiki, ya watembea kwa miguu kwenye barabara Chake chake- Mkoani.

Nae mwanafunzi Aisha Khamis Adam, alisema sio kweli kuwa wao wamekuwa wakidharau honi, bali wakati mwengine madereva, wanakuwa wanawapigia karibu yao, pasi na dharura.

‘’Lakini madereva wengine hutupigia honi sisi wanafunzi wa kike, kama ishara ya kuanza kwa mahusiano ya kimapenzi na mmoja kati yetu, na hasa wanaemjua,’’alieleza.

Hata mwanafunzi Mwajuma Daudi Mohamed, alisema wamekuwa wakiziheshimu mno honi na mivumo ya gari, isiyo ya kawaida, ingawa shida ni madereva kutopunguza mwendo wanapowaona wanafunzi.

‘’Kama madereva wanafukuzana huko wanakotokea, hata wakikuta kundi la wanafunzi, hawapunguzi mwendo, sasa hili ni tatizo kwao na sio sisi,’’alieleza.

Hivi karibuni Mkuu wa usalama barabarani mkoa wa kusini Pemba kutoka Jeshi la Polisi, Shawali Abdallah, alisema wameshazimaliza skuli zote za msingi na sekondari, kuwaelimisha wanafunzi, matumizi sahihi ya barabara.

‘’Tumeshapita skuli zote za mjini na vijijini, kwa zile ambazo wanafunzi wanapita kwenye barabara kuu, kuwa wanapokwenda ama kurudi gari, wawe wamezipa uso gari, hii inaweza kuwa rahisi chombo kikipata hitilafu, kukimbia,’’alieleza.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amewakumbusha madereva, kuendelea kuheshimu sheria za usalama barabarani.

 Katika kipindi cha Januari hadi Disemba mwaka 2020 kikosi cha Usalama barabarani, kilifanikiwa kukamata makosa madogo ya Usalama barabarani 2,152,533 ikilinganishwa na makosa 2,311,538 yaliyokamatwa kwa mwaka 2019.



Kwa upande wa Tanzania Zanzibar, mkoa wa Mjini Magharibi uliongoza kwa matukio ya aina hiyo 7,031 na Mikoa iliyokuwa na idadi ndogo ya matukio ilikuwa ni Kaskazini Pemba 1,512 na Kusini Unguja 2,154.

Matukio ya usalama barabara kwa 2019, yaliripotiwa 104, yakisababisha majeruhi 290 na mwaka 2020, kulikuwa na watu 124 waliofariki, na majerehi 2092.

Ingawa pia ripoti hiyo ya Jeshi la Polisi Tanzania, ya mwaka 202o, iliripoti ajali 1,133 za piki piki, zilizosababisha vifo 744, sawa na majeruhi 948 kwa Tanzania yote.

                                        mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch