Skip to main content

HAKI HAISUBIRIWI, INATAFUTWA: LAZIMA WANANCHI WAWE NA UWELEWA WA HAKI ZAO - WADAU

 






ZANZIBAR:::


KATIKA kuhakikisha jamii inakuwa na uwezo wa kutambua umuhimu  wa kudai upatikanaji wa haki zao za msingi, kamati za wananchi kutoka shehia za Wilaya za Micheweni, Wete, Mkoani na Chake Chake Pemba zimeshauriwa kuendelea kuwashirikisha wananchi kujadili changamoto zinazowakabili ili kuzipatia ufumbuzi kwa njia na wakati sahihi bila kusababisha madhara.


Ushauri huo umetolewa wakati wa mkutano na kamati za wananchi kutoka shehia za wilaya hizo kisiwani Pemba ulioandaliwa na Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba (PEGAO) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa lengo la kuzijengea uwezo kamati hizo kufuatilia kero zinazokwaza haki za wanawake ambazo ziliibuliwa na wahamasishaji jamii kwenye maeneo yao.


Akizungumza katika mkutano huo ambao ni utekelezaji mradi wa kuwawezesha wanawake kwenye uongozi unaofadhiliwa na Ubalozi wa Norway Tanzania, afisa tathimini na ufuatiliaji wa TAMWA ZNZ, Moh’d Khatib, alihimiza jamii kuwa na utamaduni wa kukutana kujadili kero zinazowakabili na kukwaza haki za wanawake ili kuzitaftia suluhu kwa pamoja.


Alisema, “lazima kamati hizi zikutane na wananchi ili wao wenyewe waseme wana changamoto gani kuliko kuwasemea, hii itasaidia kuwa na uthibitisho na ushahidi wa kutosha juu ya changamoto yoyote inayotafutiwa ufumbuzi.”

Alibainisha kupitia ushirikishwaji wa wananchi kujadili changamoto na kero zinazowakabili wanawake kupata haki zao itasaidia kukuza uelewa wa jamii kushiriki moja kwa moja kudai haki zao.


“Kupitia kamati za shehia, wananchi wote wanatakiwa wawe na uwezo wa kutambua changamoto zao na wajue kuwa ni wajibu wao kuzitaftia ufumbuzi na kudai haki zao kwa kujua nani anapaswa kuzitatua ili wachukue hatua wenyewe katika kuhakikisha wanapata haki muhimu hasa wanawake,” alifahamisha.


Aidha aliongeza kuwa Ubalozi wa Norway kwa kushirikiana na TAMWA, ZAFELA na PEGAO kupitia mradi huo unalenga kujenga jamii imara yenye uwezo wa kupaza sauti kwenye kero zinazopelekea kuwakosesha wanawake haki za msingi katika jamii.


 “Lengo kubwa la mradi huu tunataka kujenga jamii ya wananchi wenye uthubutu wa kupaza sauti juu ya changamoto zinazowakabili kwenye maeneo yao hasa wanawake ili kusaidia utatuzi wa kero hizo kwa wakati,” alisema afisa huyo.


Mapemba mkurugenzi  wa mradi huo kwa upande wa PEGAO, Hafid Abdi, alifahamisha  jamii inapaswa kutambua kwamba inao wajibu wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili ili kujenga jamii yenye kufuata misingi ya usawa wa kijinsia kwa wote katika kila eneo.


Alieleza, “wananchi wanatakiwa wajue kwamba kero zilizopo katika jamii ni zao na wanao wajibu wa kuzitaftia ufumbuzi kwa njia sahihi ili kuwepo na misingi ya upatikanaji wa haki za msingi kwa kila mmoja hasa wanawake katika nyanja zote ikiwemo kiuongozi.”


Nae Mratibu TAMWA ZNZ ofisi ya Pemba, Fat-hiya Mussa, alisema “haki haisubiriwi, haki inatafutwa, hivyo ni lazima wananchi wawe na uelewa wa kutosha juu ya zipi ni haki zao na namna gani wanapaswa kudai haki zao kwa njia iliyo sahihi.”


Mapema Mohamed Abdalla mjumbe wa kamati hizo alihimiza jamii kutumia vyombo vya habari kupaza sauti zao ili changamoto zinazowakabili ziweze kuwafikia walengwa kwa wakati.


Alibainisha, “ili changamoto hizi ziweze kutatuliwa, ni lazima sisi wananchi katika kila maeneo ambayo tunaona ni kikwazo kwetu tupate wandishi wa habari ambao watatusaidia kupasa sauti zetu.”


Kamati za wananchi katika shehia zilizoundwa kupitia mradi huo kupitia Ubalozi wa Norway zinafanya kazi kwa kuwashirikisha wananchi kujadili changamoto na vikwazo vinavyowakabili hasa wanawake na kupelekea kushindwa kupata haki zao za msingi ikiwemo ushiriki wao katika uongozi.

mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch