Skip to main content

USHIRIKIANO WIZARA ZA ARDHI SMZ, SMT KUIBUA KASI UJENZI NYUMBA NAFUU




Mashirikiano ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya  Makaazi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) yanatarajiwa kuibua kasi ya kiutendaji  katika sekta ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu ili wananchi waweze kuzimudu.

Akizungumza Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (SMZ) Dkt. Mngereza Mzee Miraji katika kikao cha mashirikiano ya kiutendaji kilichofanyika mwisho wa wiki iliyopita  katika ukumbi wa Wizara hiyo  Maisara Unguja, alisema kupitia vikao  vya mashirikiano baina sekta mbili hizo vitasaidia katika kuibua kasi ya utendaji hasa katika sekta ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu zenye kukidhi mahitaji ya wananchi wenye kipato tofauti.

Alisema kwamba kunamafanikio yameanza kuonekana kupitia vikao hivyo ikwemo kukamilika rasimu mbili ya makubaliano (MOU) zimekamilika kiutendaji ambapo zitarajiwa kusainiwa katika kikao kijao cha ngazi ya mawaziri wa pande zote mbili wa wizara ya Ardhi ya SMZ na SMT.

Dkt Mngereza alifafanua kwamba ‘MOU’ zilizokamilika ikiwemo ya Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC) na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na ‘MOU’ inahusu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi (SMT) ambapo kuna mambo mengi ya ushirikiano wamekubaliana ikiwemo ngazi ya kitalaamu, kubadilishana uzoefu pamoja na mafunzo kwa watendaji wa taasisi mbili hizo.

Pia alisema wizara ya Ardhi ya SMT imepiga hatua zaidi kiutendaji ambapo wanamfumo unayojulikana kwa jina la Intergreted Land Information System unasaidia kutatua changamoto ya urasimu pamoja na kuboresha huduma hivyo wizara yake kupitia Idara ya Kamisheni ya ardhi  imeanza maandalizi ya kuwa na mfumo huyo na wamefika katika hatua nzuri.



Sambamba na hayo Dkt Mngereza alisema wamekubaliana wawe na mashirikiano ya tafiti katika sekta ya ardhi na makaazi ya bei nafuu lakini katika kuanzia hilo watakuwa na kamati ya pamoja (Joint committee) ambayo imeshaingizwa katika mazungumzo ya yanayoendelea baina ya  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na taasisi ya Shelterafrique.

Alifahamisha kwamba taasisi ya Shelterafrique   inautaratibu wa kutoa mikopo ya bei nafuu kwa nchi wanachama zaidi ya nchi 30 na mwaka huu wanatarajia kutakua na mkutano  pamoja na maonesho ya teknolojia ya ujenzi wa maakazi ya bei nafuu.

Aidha Dkt Mngereza alisema wizara yake inakabiliwa na changamoto ya wataalamu wa upimaji ardhi ndani ya maji (Hydrographic Survey) hivyo wamekubaliana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi SMZ watakuwa na mpango mkakati wa kuwajengea uwezo  watendaji wao ambapo kila wizara italazimika kuingiza katika bajeti yake.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi (SMT) Dkt. Allan H. Kijazi alisema watahakikisha wanaweka misingi imara kwa watanzania wote kumiliki nyumba za bei nafuu na kuendeleza matumizi ya ardhi bila ya kuangalia tofauti yoyote.

Alieleza kwamba matarajio ya kikao hicho ni kuwa na mifumo ya pamoja ya uboreshwaji wa utoaji huduma kwa viwango vinavyofanana baina ya Taasisi mbili hizo kwa lengo la kukidhi mahitaji ya Taifa.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu Shirika la Nyumba Zanzibar(ZHC)Mwanaisha Ali Saidi  kupitia kikao hicho aliwaahidi wananchi wategemee mabadiliko katika sekta ya maakaazi nakusemba kwamba  Shirika lake limejipanga kimkakati katika kuhakikisha linatoa huduma ya nyumba bora na salama kwa bei nafuu.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemiah Kyando Mchechu alisema Shirika hilo kwa sasa limejikita zaidi kwenye miradi  ya ujenzi ambapo ndio kipamumbele chake kujenga nyumba katika jiji la Dar es salaam, Dodoma na maeneo ya miji na nyumba hizo ni za ghoroma na   bei nafuu.



Kwa upande wa watendaji waliyoshiriki kikao hicho wamezipongeza Serikali zote mbili(SMZ na SMT)  kwa kuagiza kuweko na mashirikiano ya kiutendaji katika Taasisi ambazo zinalingana kimajukumu na hazimo katika orodha ya sekta ziliyomo katika Muungano.

Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch