Skip to main content

WATUMISHI WA UMMA: 'MUSIANZISHE MIJDALA YA KUKEBEHI, KUDHARAU MWELEKEO WA SERIKALI' : MDHAMINI THABITI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:

OFISA Mdhamini Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Thabit Othman Abdalla, amewataka watumishi wa umma kisiwani Pemba, kutoungana na watu wengine, katika kukebehi na kudharau mipangano, sera na mikakati ya serikali, kwani kufanya hivyo ni ukiukwaji wa maadili ya kazi.

Alisema, kila mtumishi wa umma anapofanyakazi katika kitengo na idara yoyote ile, ajue kuwa anamwakilishi kiongozi wa nchi, hivyo lazima asikubali kuwa sehemu ya kuongoza mijadala ya kukibehi mwelekeo wa serikali.

Ofisa Mdhamini huyo aliyasema hayo Januari 15, 2023, ukumbi wa mikutano Baraza la mji wa Chake chake, wakati akiyafunga mafunzo ya siku tatu, kama sehemu ya uthibitishwaji wa kazi, kwa watumishi wapya wa umma, yalioendeshwa na Chuo cha Utawala wa Umma ‘IPA’.

Alisema, wapo baadhi ya watumishi wa umma kwa kule kutokujua nafasi zao, wamekuwa wakiungana au wakati mwengine kuanzisha mijadala ya kudhoofisha mikakati ya serikali.

Alieleza kuwa, kiutumishi hilo ni kosa, kwani kuajiriwa kwake katika kitengo anachofanyakazi, anamwakilishi kiongozi wa nchi, kama muajiri mkuu.

‘’Wapo watumishi wengine kwa mfano, wanakebi suala la kupanda vyakula na sera ya uchumi wa buluu, au kusema serikali haijafanya lolote, haya na mengine yanayofanana na hayo, hayafai kwa mutumishi umma,’’alisema.

Kati hatua nyingine Ofisa Mdhamini huyo, amewataka watumishi hao wakawe watumishi bora wenye kutunza sira za ofisi, matumizi sahihi ya lugha na kufanyakazi, kwa moyo wa kiuzalendo.



Hata hivyo alisema, anaamini kwa elimu walioyoipata kwa siku hizo tatu, watakuwa mfano wa kuigwa na wenzao kwa kule kuzifuata kwa vitendo sheria na kanuni za utumishi wa umma.

Akizungumza kabla ya kufungwa kwa mafunzo hayo, Mkuu wa ‘IPA’ tawi la Pemba Juma Haji Juma, alisema mafunzo hayo yamewafungulia milango watumishi hao.

‘’Moja ya faida kubwa ya mafunzo haya, mtaweza kuthibitishwa kazi, ruhusa za likizo au kwenda masomoni sasa mtakuwa na haki, na hasa baada ya ofisi zenu kuridhishwa na baadhi ya mambo,’’alieleza.

Hata hivyo Mkuu huyo wa ‘IPA’ tawi la Pemba, aliwasisitiza watumishi hao, kama wanataka kufika mbali kiutumishi, waziheshimu na kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo hayo.



‘’Mafunzo haya mjue kuwa, ni sehemu ya utekelezaji wa sheria na kanuni ya utumishi wa umma ya Zanzibar ya mwaka 2014, hivyo muone thamani yake, katika kazi zenu,’’alieleza.

Mapema akiwasilisha mada ya sheria ya Utumishi wa Umma Zanzibar ya mwaka 2014, mwanasheria Suleiman Omar Makame, alisema sheria hiyo ni nzuri, ikiwa itatekelezwa kama ilivyoandikwa.

‘Kwa mfano, sheria imetoa amri ya likizo kila mwaka, na fedha zake kila baada ya miaka mitatu, lakini hata namna ya upandishwaji madaraja na haki ya matibabu kwa mtumishi wa umma,’’alieleza.



Baadhi ya watumishi hao akiwemo Abass Omar Abass wa wizara ya Habari, alisema sheria ni nzuri, ikiwa muajiri atayatekeza ipasavyo haki za muajiriwa.

Nae Wahida Kombo Khamis kutoka Baraza la mji Chake chake, alipendekeza mafunzo hayo, yashirikishe na maafisa utumishi, ili kupata ufafanuzi zaidi.




Katika mafunzo ya siku tatu, mada 10 zilijadiliwa ikiwa ni Mfuko wa Hifadhi wa Jamii Zanzibar ‘ZSSF’, sheria ya ZAECA, uzalendo na umuhimu wake kwa taifa, sheria ya Utumishi ya umma na kanuni zake pamoja na sheria ya Afya na usalama kazini.

                             Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...