Skip to main content

WAZIRI SHAMATA AZINDUA OFISI YA ELIMU MKOANI ATAMANI UFAULU UPAE

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Shamata Shaame Khamis, amesema kukamilika kwa ofisi ya kisasa ya elimu wilaya ya Mkoani Pemba, iwe chachu ya kuongeza ufaulu na ufuatiliaji wa masomo, wilayani humo.

Waziri Shamata aliyasema hayo Disemba 2, 2024 mara baada ya ufunguzi wa ofisi hiyo, ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964.

Alisema, tokea kufanyika kwa mapinduzi hayo, hakujawahi kuwa na ofisi mpya na ya kisasa ya elimu ya wilaya, ambapo wakati huo watendaji hao walikuwa wakifanyakazi katika mazingira magumu.

Alieleza kuwa, kama sasa imeshajengwa ofisi ya kisasa na yenye vifaa vipya, iwe chachu ya kuongeza ufaulu na suala la ufuatiliaji wa masomo kwa wilaya ya Mkoani.

‘’Leo (jana) tumeshaifunfua ofisi mpya na ya kisasa, hivyo ni matumaini yangu kuwa, itakuwa chachu ya kuongeza ufaulu, lakini pia suala la kufanya ufuatiliaji kwa skuli mbali mbali wilayani humo,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Waziri huyo, alisema suala la elimu kabla ya mapinduzi ya Zanzibar, lilikuwa likolewa kwa ubaguzi, na mtoto wa mnyonge, hakuwa na haki ya kupata elimu.

Alieleza kuwa, jambo hilo liliwakera mno waasisi wa taifa hili, na ndio maana hatua zilichukuliwa, na kufanya mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964, ili kuondoa utawala wa kidhalimu.



‘’Tukiwa nashuhudia miundombinu ya kisasa ya elimu, tukumbuke kuwa huko nyuma, wazazi wetu hawakupata haki hii, maana ilikuwa wanaosoma ni watoto wa watawala pekee, leo tunashukuru,’’alifafanua.

Akizungumzia suala la miaka 60 ya mapinduzi Zanzibar, Waziri huyo alisema kila mmoja, anayohaki ya kuyalinda, kuyaenzi kwani ndio mkombozi wa maisha ya wazanzibari.

Mapema Katibu Mkuu wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said, alisema ujenzi wa ofisi hiyo, walikabidhiwa na Halmashauri ya wilaya ya Mkoani, ili kuendeleza ujenzi wake.

Alisema kuwa, kisha wizara iliridhia kukamlisha ujenzi huo, ili watendaji wa wizara ya elimu ngazi ya wilaya, wapate ofisi ya kisasa ya kuendesha shughuli zao.

Alieleza kuwa, walitumia shilingi milioni 182.882, kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo pamoja na kazi nyingine, kama ya utiaji umeme, maji, madirisha, milango, marekebisho ya maktaba, ujenzi wa ukuta pamoja na rangi.

Katibu huyo alieleza kuwa, ndani ya ofisi hiyo wameshaweka kompyuta za kisasa, mashine ya fotokopi ya kisasa yenye uwezo wa kufanya muunganiko wa kutoa kopi.

Aidha alieleza kuwa, kazi hiyo ya ukamilishaji ujenzi huo, imefanya na kampuni ya United Ram Construction, na kusimamiwa na mshauri ambae ni kampuni ya kizalendo ya AE&Q.

‘’Kazi ya kukamilisha ujenzi huu, ulianza Septamba 2023, na kumalika mwanzoni mwa mwaka huu, ambapo ndani yake, mna vyumba vitano, maktaba na vyoo pamoja na stoo,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Khamis Abdulla Said, alisema ujenzi huo ni eneo moja wapo, la utekelezaji wa mageuzi makubwa ya elimu, yalioridhiwa na serikali ya awamu ya nane.

‘’Serikali, imedhamiria kuwa na ofisi ya elimu za wilaya ya kisasa, na tayari tumeshajenga katika wilaya saba na nne zilizobakia ujenzi utafanyika kabla ya mwaka 2025,’’alifafanua.

Wakati huo huo, aliwapongeza waalimu, wanafunzi na wazazi wa wilaya ya Mkoani, kwa kuongoza katika mitihani ya taifa ya darasa la saba, kufuatia matokeo yaliotolewa hivi karibuni.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Dk. Mwinyi, wameshajengewa madarasa 381 pamoja na ajira za waalimu 596 kwa wilaya za Chake chake na Mkoani.

Hata hivyo, amewataka wazazi, walezi na waalimu kuendelea kushirikiana, ili kuona watoto wanapata elimu katika mazingira rafiki, na hasa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa ofisi ya elimu ya wilaya ya Mkoani.

Naibu Waziri wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Ali Abdull-ghulam Hussein, alitaka kuendelea kutunzwa kwa ofisi hiyo mpya na ya kisasa, ili iwasaidie na wingine hapo badaae.

Shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, zitaendelea tena leo kwa uwekaji wa jiwe la msingi skuli ya Utaani Wete, ufunguzi wa kituo cha afya cha mama na mtoto Tironi Mkoani na uzinduzi wa barabara ya Kijangwani- Birikau wilaya ya Chake chake.

                           Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch