Skip to main content

BITEKO AWEKA JIWE LA MSINGI OFISI, MAAKAZI YA UHAMIAJI MKOANI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

NAIBU Waziri Mkuu, ambae pia ni Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Doto Mashaka Biteko, amesema kitendo cha kufanyika kwa mapinduzi ya Zanzibar, kilikuwa chema, kwani kililenga kuwapa uhuru wa wananchi, kusafiri nje ya mipaka kadiri wapendavyo.

Naibu Waziri huyo Mkuu, aliyasema hayo Disemba 6, mwaka 2024 uwanjwa wa Umoja ni nguvu Mkoani Pemba, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi, wa ofisi na makaazi ya maafisa wa Uhamiaji, wilayani humo, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi.

Alisema, mapinduzi hayo, yalikuwa yanafaa mno kuona wazanzibari na wananchi wote, wanatumia haki yao kwenda watakako kwa mujibu wa sheria, uhuru ambao hawakuwa nayo, kabla ya mapinduzi.

Alieleza kuwa, mapinduzi hayo kupitia viongozi na wakuu wa nchi tokea mwaka 1964 hadi leo, wanaendelea kusimamia haki hiyo, ili kuhakikisha wananchi, wanasafiri zaidi nje ya mipaka ya Tanzania.

‘’Kila mmoja ni shahidi, baada ya kufanyika kwa mapinduzi haya na kisha kuundwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, viongozi waliendelea kusimamia masuala ya safari, chini ya idara ya safari na pasipoti, ili kila mmoja kupata haki hiyo,’’alieleza.



Aidha Dk. Biteko alieleza kuwa, mapinduzi hayo si tu kwamba yamempa uhuru mzanzibari, lakini yamemuonesha njia ya kufika mbali, kwa ajili ya kiuchumi, ili kutatua changamoto zake.

Alieleza kuwa, matunda ya mapinduzi hayakuishia hapo, kwani April 26, mwaka 1964 viongozi na waasisi wa mapinduzi hayo, akiwemo Rais wa kwanza wa Zanzibar Abeid Amani Karume na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, waliziunganisha nchi, na kuzaliwa Tanzania.

‘’Lengo la Muungano, pamoja na mambo mingine, lakini pia ni kuimarisha huduma mbali mbali kwa wananchi, ikiwemo upatikanaji wa vibali vya kusafiria nje ya nchi,’’alifafanua.

Aidha alieleza kuwa, huduma za uhamiaji kisha zilisambaa nchi nzima, ambapo kwa wilaya ya Mkoani, zilianza mwaka 1979, ambapo ofisi yake, haikukidhi vigezo kwa wakati uliopo.



‘’Leo tukiwa ndani ya miaka 60 ya mapinduzi, tumeanzisha safari mpya kwa kuwa na ofisi ya kisasa na makaazi ya maafisa wa Uhamiaji hapa wilaya ya Mkoani,’’alieleza.

Hivyo amewataka wananchi wa Zanzibar, kuendelea kuyaenzi, kuyalinda na kuyaheshimu mapinduzi ya Zanzibar, ambayo matunda yake sasa, yanaonekana kila sekta,

Wakati huo huo Naibu Waziri huyo Mkuu na Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Doto Mashaka Biteko, ameushauri uongozi wa Idara ya Uhamiaji, kuiga aina ya ujenzi wa ofisi hiyo, ili kujenga nyingne nchi nzima.




Mapema akisoma taarifa ya kitaalamu, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, (sera, uratibu na Baraza la Wawakilishi), Zanzibar Seif Islam Salum, alisema ujenzi huo, utakapokamilika utakuwa na makaazi ya maafisa sita, pamoja na ofisi zenye huduma zote.

Alieleza kuwa, ujenzi huo ulianza mwezi August 2022, ambapo ulitarajiwa kumalizika mwaka mmoja baadae, ingawa kwa sababu mbali mbali, ulimalizika mwezi Disemba mwaka jana.





‘’Ujenzi wa jengo hili, kwa hakika unaakisi na fedha ambazo zilitengwa kwa kazi hiyo, maana jengo limetimiza viwango vinavyotakiwa,’’aliafafanua.

Nae Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jumanne Sagini, alisema mapinduzi ya Zanzibar, ndani ya Idara ya Uhamiaji, imeweka historia mpya, kwa ujenzi wa jengo hilo la ofisi na makaazi ya maafisa wa Uhamiaji.



Hata hivyo, alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluh Hassan, amekubali kutoa fedha za kuimarisha utendaji kazi wa Idara ya uhamiaji, ikiwemo ujenzi wa ofisi za wilaya na mkoa nchi nzima.

‘’Na kwasasa, serikali imeridhia ajira 1,741 za Idara ya Uhamiaji, pamoja na upandisha vyeo maafisa mbali mbali wa Uhamiaji 2,824  kwa nchi nzima,’’alifafanua.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Anna Peter Makakala, alisema Idara hiyo inaendelea kutekeleza maagizo ya kiongozi wa nchi, ili kuona wanatoa huduma za kileo.



Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema ujenzi wa ofisi hiyo na maakazi ya maafisa wa Uhamiaji, ni moja ya matunda ya muungano, yalioasisiwa na mapinduzi.




Jengo hilo la ghorofa limegharimu shilingi bilioni 1.53, ambalo lilikuwa na mkandarasi kampuni ya Bench Mark Engerneering na kusimamiwa na wakala wa majengo Zanzibar ‘ZBA’

                         Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch