Skip to main content

WAKULIMA MAZAO YA BIASHARA MKOANI WAAHIDI KULITUMIA SOKO JIPYA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WAKULIMA wa mazao ya kilimo cha biashara ikiwemo ndizi, chungwa na muhogo, wa shehia za Mtambile, Mizingani, Chumbagaeni na Wambaa wilaya ya Mkoani Pemba, wamahidi kulitumia soko jipya la Mtambile, ili kuongeza thamani ya biadhaa zao.

 Walisema, kwa sasa wamepata mkombozi wa bidhaa zao, na hwenda ikiwa ndio mwisho wa kulanguliwa na wachuuzi wa bidhaa mbali mbali wanaosafirisha nje ya Pemba, kw akule kuwalalia kibei.

Wakizungumza na mwandishi wa habari mara baada ya kufunguliwa kwa soko hilo, na Waziri wa Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis, walisema kwa vile wameshakabidhiwa, sasa ni kulitumia kwa kuuzia bidhaa zao.

Mmoja katuia ya wakuliuma hao anaejishughulisha na kilimo cha ndizi za mtwike, pukusa na koroboi Haji Kassim Khamis wa Mtambile, alisema sasa baada ya kuvuna atakimbila kwenye mdana sokoni hapo.

‘’Kwa vile tumeshaelezwa kuwa, mnada wa bidhaa kama za ndizi utakuwepo, sitouza tena ndizi zangu chochoroni na kulaliwa kibei, kama ilivyokuwa zamani,’’alieleza.

Nae mkulima wa mihogo kwa ajili ya biashara Issa Hamdu Ali wa Mizingani alisema, imekuwa ni kawaida soko lao wao, limo mikononi mwa wachuuzi na wakati mwingine kuwadanganya.

‘’Anakwambia Unguja muhogo hauna bei, maana umeingia mwingine kutoka Tanga, lakini kumbe huwa ni waongo, hivyo sasa watatufuata sokoni Mtambile,’’alisema.

Nae Mwanaisha Omar Mkubwa wa Wambaa alisema hata chungwa anazolima sasa hatozipeleka tena soko la Chake chake na atalitumia soko jipya la Mtambile.

‘’Tunaomba tua masharti ya vibali na matozo mingine yawe chini kwa sisi wafanyabiashara wadogo, ili tusijetukalikimbia soko letu, na kurudi kwa wachuuzi wetu,’’alisema.

Mkurugenzi Baraza la mji wa Mkoani Yussuf Kaiza Makame, aliwaahakikishia wakulima wa mazao mbali mbali, kuwa watawekewa mazingira rafiki, ili kuwavutia kulitumia soko hilo.

‘’Kwanza waanze kulitumia soko hili, na kisha kama kuna changamoto zozote tukae chini kwa pamoja, na kuona jinsi ya kuzitatua na mwisho wa siku muendelee kulitumia, maana ni kwa ajili yenu,’’alifafanua.

Kwa upande wake, Katibu mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Issa Mahafudhi, alisema ujenzi wa soko hilo, ni utekeleza wa ahadi ya Rais wa Zanzibar, wakati alipokutana na wajasiriamali.

Hata hivyo alisema, mji wa Mtambile umekuwa na ongezeko la watu kila mwaka, na sasa kuchukua nafasi ya tatu kwa idadi ya watu, baada ya Chambani yenye wakaazi 7,460, Kengeja 7,202 na Mtambile 7,000.

‘’Hivyo uwepo wa soko hili, limeandana na mahitaji ya wananchi kwa muda mrefu na hasa suala la changamoto, iliyopo ya wafanyabiashara kuendesha shughuli zao pembezoni mwa barabara,’’alifafanua.

 Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema serikali inampango wa kujenga soko jingine kama hilo, katika eneo shehia ya Kengeja, ili kukidhi mahitaji ya wajasiriamali.



Soko hilo la matunda na mboga la Mtambile inavyo vikuta 40, milango 13 ya maduka, ujenzi wake ulianza mwishoni mwa mwaka 2022, na kumalizika mwezi Julai mwaka huu.

Ujenzi huo, umegharimu zaidi ya shilingi milioni 5.88 ambapo ni fedha zinazotokana na makusanyo ya baraza la mji Mkoani, kupitia serikali kuu.

                           Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch