Skip to main content

DK. MWINYI AWEKA JIWE LA MSINGI NYUMBA ZA MADAKTARI MKOANI, AAHIDI UJENZI WA HOSPITAL YA RUFAA KILA MKOA

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema ujenzi wa nyumba za madaktari karibu na hospitali, kutaondoa adha kwao na wagonjwa, kwa kumudu kutoa huduma saa 24.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo Disemba 3, mwaka 2024, uwanja wa mikutano bandarini Mkoani, mara baada ya kuziwekea jiwe la msingi, nyumba za madaktari zilizopo hospital ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, ikiwa ni shamra shamra za kuelekea miaka 60 ya mapinduzi Zanzibar.

Alisema, nyumba hizo zitakapokamilika, zinatarajiwa kuondoa usumbufu kwa madaktari hao na wagonjwa wanaokwenda hospitali, kwa kule kuwa karibu na sehemu zao za kazi.

Alieleza kuwa, serikali pia itapunguza gharama za kuwafuata madaktari kwenye maakazi yao ya uraiani, pale inapotokezea wagonjwa wa dharura, hasa nyakati za usiku.

‘’Leo (jana) tumeshaziwekea jiwe la msingi nyumba za madaktari wetu, ni matumaini yetu sasa huduma zote za kitabibu, zitapatikana saa 24, kwa vile madaktari watakuwa wanaishi karibu na hospitali,’’alisema.

Aidha Rais huyo wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema ujenzi wa nyumba hizo ambao unafanywa na serikali ya watu wa China, ni kuendeleza historia yao na Zanzibar.

Alieleza kuwa, ushirkiano huo ulianzia pale China, kwa kuwa nchi ya kwanza kuyatambua mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, na kuanzia hapo, walianza kuiunga mkono Zanzibar, hasa katika huduma za afya.

Alifafanua kuwa, kuanzia mwezi Aprili mwaka 1969, serikali ya watu wa China, walijenga hospitali ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani, na kuanza kutoa misaada na madaktari mbali mbali wa fani tofauti.

Alisema kuwa, katika kuendeleza dhamira yao hiyo, kisha mwaka 2016, serikali hiyo ya Jamhuri ya watu wa China, iliifanyia ukarabati mkubwa hospitali hiyo.

‘’Kutokana na vifaa na uwezo iliyonayo hospitali hiyo, na msaada mkubwa wa wataalamu kutoka China, kwa sasa inatumika kama hospitali ya rufaa, hapa kisiwani Pemba,’’alifafanua.

Aidha Dk. Mwinyi alieleza kuwa, msaada wa kuimarisha huduma za matibabu hospitalini hapo, ulikuja tena mwezi Novemba mwaka 2021, ambapo China, iliiahidi serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuifanyia ukarabati wa baadhi ya maeneo na ujenzi wa nyumba za madaktari.

‘’Leo nimefurahishwa kujionea mwenyewe, mwenzetu hawa wametekeleza kwa vitendo, kile waliochokiahidi na kuendeleza ushirikiano wa dhati, uliopo miaka 54 iliyopita, kwa ujenzi wa nyumba hizi,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Rais huyo wa Zanzibar, alisema serikali kwa upande wake, itajenga nyumba nyingine za madaktari, katika hospitali za wilaya za Kinyasini, Micheweni, Vitongoji kwa Pemba na Kitogani, Pongwe, Panga tupu na Kivunge kwa Unguja.

Alifafanua kuwa, matayarisho ya ujenzi wa nyumba hizo yameshaanza, na matarajio yake ni kuona, miradi hiyo inakamilika kwa wakati, kama ilivyopangwa hapo awali.

Hata hivyo alisema, baada ya kukamilika kwa miradi hiyo, itakuwa kumeendelezwa kwa vitendo, mafanikio ya sekta ya afya nchini, kwa kuondoa kukosekana kwa madaktari, kutoa huduma za dharura.

Wakati huo huo, Rais huyo wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, akijibu maombi ya Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, juu ya uwepo wa hospitali ya rufaa Pemba, alisema matayarisho yake yameanza.

Alisema, serikali inampango wa kujenga hospitali ya moja kila mkoa, ambayo itakuwa na hadhi, vifaa na wataalamu, ambapo kwa mkoa kwa kusini Pemba, itajengwa Chake chake.

‘’Pamoja na kuwa na hospitali za rufaa za kila mkoa, lakini serikali inatarajia kujenga hospitali nyingine ya rufaa ya ujumla kwa Zanzibar, eneo la Binguni Unguja,’’alieleza.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Hassan Khamisb Hafidh, alisema wananchi 129,141 walitibiwa katika hospitali ya Abdalla Mzee, ambayo kwa sasa, inatumika kama hospitali ya rufaa kisiwani Pemba.

Alieleza kuwa, ndio maana kwa mwaka jana pekee, kulikuwa na wagonjwa 50,479 wa nje walitibiwa na waliolazwa kwa mwaka huo ni 633,464.

‘’Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, inapokea wagonjwa kutoka Pemba na Unguja, kwani sasa ndio hospitali ya rufaa kwa kisiwani Pemba, kutokana na matibabu yake,’’alifafanua.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa nyumba za madaktari, Meneja mradi wa ujenzi huo Zhang Ligen, alisema kuwa, kuna majengo manne ya ghorofa nyenye nyumba zaidi ya 65 kwa ajili ya madaktari.

Alieleza kuwa, mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Julai mwaka huu, na kuishukuru serikali na watendaji wa wizara ya Afya, kwa ushirikiano wao, wakati huu wakiendelea na ujenzi.

Mkurugenzi mkuu wizara ya Afya Zanzibar Dk. Amour Suleiman Mohamed, alisema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ilisaini makubaliano na serikali ya Jamhuri ya watu wa China, August 13, 2021 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo.

Alisema nyumba hizo zinajengwa kwa msaada wa serikali ya watu wa China, chini ya mkandarasi kutoka kampuni ya Zhengtai group na shilingi bilioni 16.481 zitatumika hadi kukamilika kwake.

‘’Mradi huu utakapokamilika, utandoa kilio cha muda mrefu cha madaktari, cha kutokuwa na makaazi karibu na sehemu zao kazi, jambo lililokuwa likizorotesha utendaji,’’alifafanua.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, awali alimuomba Rais wa Zanzibar na Mwenyeiki wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuangalia uwezekano wa kujenga hospitali ya rufaa kisiwani Pemba.

Aidha aliwataka wananchi, kuendelea kuyalinda na kuyaenzi mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, kwani ndio funguo ya maendeleo na uwepo wa miradi mikubwa.   

                                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch