Skip to main content

DK. MWINYI AZINDUA BARABARA YA LAMI BIRIKAU, AWAPA NENO MADEREVA

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali ya awamu ya nane, itaendeleza kwa vitendo, malengo ya mapinduzi ya Zanzibar, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya kisasa, kama vile barabara.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo Disemba 4, mwaka 2024, uwanja wa mpira wa Birikau shehia ya Michungwani, wilaya ya Chake chake Pemba, mara baada ya kuizindua barabara ya Kijangwani- Birikau, yenye urefu wa kilomita 4.2, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi Zanzibar.

Alisema, kwa vile ujenzi wa miundombinu ya barabara za kisasa, ni miongoni mwa matunda ya mapinduzi, hivyo serikali anayoingoza imedhamiria kufanya jitihada za makusdi, za kuimarisha miundombinu hayo, katika maeneo ya mijini na vijijini kwa Unguja na Pemba.




Alieleza kuwa, malengo hasa ya serikali ni kuziimarisha barabara zote zilizopo na kujenga nyingine mpya, katika maeneo ambayo barabra hazijafika, ili kuimarisha mtandao wa barabara hapa Zanzibar.

Dk. Mwinyi alisema Zanzibar yote inamtandao wa barabara usiozidi kilomita 1,344, na wakati anagia madarakani, kulikuwa na wastani wa asilimi 40 ya barabara zilizojengwa kwa kiwango cha lami, na asilimia 60, zilizobakia zilikuwa na kifusi na udongo.

‘’Lakini serikali hii ya awamu ya nane, iliamua kuweka mkakati imara na madhubuti, wa kuimarisha mtandao wa barabara, kwa kuzijenga barabara za mjini na vijijini, ili zipitike na wananchi waendeleza miradi yao ya kiuchumi,’’alifafanua.

Rais huyo wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alifahamisha kuwa, Zanzibara inapoadhimisha miaka 60 ya mapinduzi, na miaka mitatu ya serikali ya awamu ya nane, kwa mipango hayo imefanikiwa.

Alieleza kuwa, mipango na mikakati iliyowekwa sasa, inatekelezwa kwa vitendo nchi nzima, na tayari wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, imeshaingia mikataba na makapuni mbali mbali, kwa ajili ya ujenzi wa bara bara hizo.

‘’Kwa mfano, kampuni kutoka Uturuki, imedhamiria kuzijenga barabara za ndani, kwa kiwango cha lami zenye urefu wa kilomita 275 kwa Unguja na Pemba, ambazo baadhi yao ujenzi umeshaanza,’’alifafanua.





Aidha alifafanua kuwa, tayari serikali imeshaingia mkataba na kampuni moja, kwa ajili ya ujenzi wa barabara kuu zenye urefu wa kilomita 130, ikiwemo ya Chake chake- Mkoani, Tunguu- Makunduchi, pamoja na Fumba- Kisauni, ambapo mkataba umeshainiwa kati ya serikali na Mkandarasi.

‘’Kwa sasa serikali, inaendelea na utaratibu wa kukamilisha ulipaji wa fidia kwa majengo na vipando, ili ujenzi huo uanze wakati wowote kuanzia sasa,’’alieleza.

Alifahamisha kuwa, mbali na hatua hizo, tayari serikali imeshatiliana mkataba na kampuni ya ‘CCECC’ kwa ajili ya ujenzi wa barabara zote za mjini Unguja, zenye urefu wa kilomita 100.

Aidha alisema, mazungumzo yanaendelea, baina ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na serikali ya watu wa China, kwa ajili ya ujenzi wa bara bara, zenye urefu wa kilomita 277, zilizoko Unguja na Pemba.

‘’Kama serikali ya awamu ya nane, itafanikiwa kukamilisha ujenzi wa barabara hizo, itakuwa tumejenga kilomita 800, wakati mtandao wa barabara hapa Zanzibar, ni kilomita 1,300,’’alifafanua Dk. Mwinyi.

 Katika hatua nyingine, Rais huyo wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliipongeza taasisi ya Zanzibar Milele Foundation, kwa mchango wa shilingi milioni 982, walazozitoa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kijangwani- Birikau.

Alisema, jumuia za aina hiyo, ndizo zinazofaa kuungwa mkono na kuigwa na nyingine, ili kuhakikisha wanashirikiana kwa vitendo, na serikali, katika mipango na mikakati ya kuijenga nchi.

Alieleza kuwa, taasisi hizo ilianza ujenzi wa barabara hiyo kwa uwekaji wa kifusi tabaka tatu, ujenzi wa daraja ndogo ‘culvert’ pamoja na misingi ya kupitisha maji ya mvua.

‘’Kama kuna shirika lisilo la kiserikali hapa Zanzibar, ambalo linafanyakazi kubwa na ya kupigiwa mfano, katika kuisadia jamii na serikali, ni Milele Ifraji Foundation,''alifafanua.

Wakati huo huo Rais huyo wa Zanzibar, amewaonya madereva nchini, kuacha kuendesha mwendo wa kasi, kwani unaweza kuzaa majanga yanayoweza kuepukika.

Alisema, barabara ni kichecheo kikubwa cha maendeleo, na kisigeuzwe chanzo cha ajali kwa mwendo kasi, ambapo aliwaomba askari wa usalama barabarani, kusliimamia jambo hilo.

Kwa upande wake Katibu wa wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Khadija Khamis Rajab, alisema barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 4.2, imejengwa na serikali kwa kushirikiana na taasisi za Milele na Ifraji Foundation.

Alieleza kuwa, barabara hiyo, imejumuisha barabara zilizokwenda kwenye vijiji vya Tondooni urefu wa mita 560, kijiji cha Kiwandani urefu kilomita wa 440, Makaange mita 100 na barabara iliyongia skuli ya Birikau, yenye urefu wa mita 200.

Katibu mkuu huyo alifafanua kuwa, ujenzi wa barabara hiyo, ulianza Febuaru 3, mwaka 2021, baada ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupata ufadhili, kutoka kwa taasisi za Milele na Ifraji Zanzibar Foundetion, kupitia ofisi ya Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba.

‘’Uwekaji wa lami wa barabara hii, kazi hiyo ilikamilishwa Wakala wa barabara Zanzibar, kwa kutumia fedha za serikali, kupitia Mfuko wa Barabara Zanzibar, na ina upana wa mita 5.5,’’alifafanua.

Barabara hiyo ambayo imegharimu shilingi bilioni 1.411, ambapo kati ya fedha hizo, shilingi mlioni 982 zimetolewa na taasisi hizo, na shilingi milioni 429.6 zimetolewa na serikali, ambapo itakuwa na uwezo wa kupitwa na gari zenye uzito usiozidi tani 10.  

Mapema Waziri wa wizara hiyo, Dk. Khalid Salum Mohamed, alisema ndani ya kipindi kifupi cha serikali ya awamu ya nane, wamedhamiria kujenga kilomita 854 za barabara kwa kiwango cha lami, Unguja na Pemba.

‘’Kwa kisiwa cha Pemba pekee, tunazo wastani wa kilomita 371, ambazo zinaendelea na ujenzi wake, kupitia kampuni mbali mbali, ambapo kwa muda mfupi ujao, Pemba itang’ara,’’alieleza.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema kazi ya ujenzi wa barabara hiyo imekamalika, sasa ni jukumu la wananchi kuitunza.

               Mwisho.  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch