Skip to main content

MADAKTARI WAIBUA JANGA JIPYA KWA WAGONJWA WANAWAKE PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-


KELELE zinazopigwa na Serikali na jumuiya mbali mbali za kukemea vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa watoto, bado wapo wanaotia pamba za masikio.

 Cha ajabu na chakusikitisha, wapo hata wazazi na walezi, waalimu na sasa hata kumeibuka wale watoa huduma wa afya, kutajwa katika hilo.

Mwaka 2019, kama ilikuwa kisirani kwa watoto na wanawake, kufanyiwa ukatili na udhalilishaji na madaktari kisiwani Pemba.

Mfano Novemba 21, mwaka 2019, katika hospitali ya Chake chake, daktari wa kitengo cha Atrasaund, alishikiliwa na ZAECA kwa tuhuma za kuomba rushwa ya ngono kwa mjamzito, kama sharti la kumpa huduma.

Kisha kesi hiyo baada ya uchunguzi na kuhojiwa, alifikishwa mahakamani, ingawa Januari 1, mwaka jana aliachiwa huru, kwa sababu mbali mbali zikiwemo ushahidi kutoumuunganisha na kesi

Aidha Disemba 18, mwaka 2019, TBC 1 iliripoti Afisa Muuguzi msaidizi wa kituo cha Afya Mamba mkoani Katavi kushikiliwa na Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kumbaka mjamzito, wakati alipokuwa akimsaidia kujifungua.

April 21, tena mwaka huu wa 2022, daktari mwengine anaefanyakazi kituo cha afya Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba.

 

Nae, kama walivyokuwa kwa madkatari wengine, wasiotekeleza wajibu wao vyema, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16.

 

Daktari huyo miaka 35, ni mkaazi wa Kangagani, Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake.

 

Kisha alimpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani, akidai kuwa kuna dawa alizozikosa hospitali, anaweza kumpatia huko.

 

Mtoto anasema kuwa, April 21 mwaka huu, alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu.

 

Ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms), kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo, alizikosa hospitalini hapo.

 

"Nilikwenda hospitali kutibiwa, ugonjwa mapele sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje daktari mwengine, kwa hiyo kesho (siku ya pili yake), atakuja kunichukua, ili ukanipe dawa nyingine", anasimulia mtoto.

 

Siku ya pili wakati yupo skuli, daktari huyo alimpigia simu na kumeleza kuwa, akirudi skuli, amsubiri kwa rafiki yake, mpaka atakapotoka kazini daktari huyo, ili akamchukue kwa ajili ya kumpatia dawa nyingine.

 

‘’Alikuja kunichukua, nikijua anaenda kunipa dawa nyingine, kumbe alinipeleka hadi nyumbani kwake na kisha baada ya kunipima Ukimwi alinibaka,’’anasimulia.

 

‘’Usiwe na wasi wasi wowote wewe uko salama na mimi niko salama, hatuna maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, na kisha aliniletea futari na,’’anafafanua.

 

 

Mtoto huyo alieleza kuwa, daktari huyo (mtuhumiwa) anapokwenda kazini, alikuwa anamfungia mlango, ingawa baa ya siku ya tano alimtoa na kuandoka eneo hilo.

 


Mama mzazi anaeleza kuwa, mwanawe aliondoka kwenda skuli, ingawa alikuja kupata wasiwasi kuona ilipofika saa 9:00 jioni, kuwa hajarudi na kuanza kupiga simu kwa ndugu na jamaa wa karibu.

 

Aliporudi mumewe (baba mzazi wa mtoto) akamueleza kuwa mtoto wao, hajarudi na ndipo walipochukua uamuzi wa kwenda kituo cha Polisi Chake Chake kutoa taarifa.

 

"Ilipofika siku ya tano nilimpigia simu nikampata, nikamtaka  arudi, na alitii agizo hilo na alipofika nilimpeleka kituo cha Polisi Chake chake, ambapo awali walipeleka malalamiko,’’anasimulia.

 

ATHARI YA MATENDO

Vitendo hivyo dhidi ya watoto ni suala zito linalowanyima haki zao za kibinadamu ambalo humkosesha haki zake za msingi ikiwemo kuishi, kupata elimu  na afya bora.

Watoto wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji ikiwemo ukatili na unyanyasaji hushindwa kufurahia utoto wao kwani kuwaletea madhara makubwa kiakili, kihisia na kimwili.

Hali hii isipokomeshwa ni wazi kuwavitendo hivyo vitaendelea kuongezeka na hata kusababisha umasikini katika jamii zetu.

Bila shaka kila mmoja amepitia hatuwa ya utotoni kama tafsiri ya mtoto inavoolekeza kuwa mtoto ni mtu yoyote mwenye umri chini ya miaka 18.

Tafsiri ambayo imetokana na mkataba wa kimataifa wa haki za watoto,mkataba wa afrika  kuhusu haki na ustawi wa mtoto pamoja na sharia ya Mtoto nambari 6 ya mwaka 2011 ya Zanzibar.

UTOAJI USHAHIDI

Suala la kutowa ushahidi limekuwa kikwazo kikubwa kwa jamii zetu na ndio maana wanaoshughulikia kesi hizo hupata mwanya wa kujificha na mwisho wa siku kufutwa kwa kesi hizo kwa ubwete kabisa.

Tumekuwa tukisikia ama kushuhudia mara kwa mara juu ya maamuzi mbalimbali ya kimahkama kutupwa kwa sababu ya kukosekana kwa ushahidi ama ushahidi kutotosheleza jambo ambalo linarejesha nyuma juhudi za mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji.

Wakati mwengine hata mahakama za juu wakisikiliza rufaa za mahakama za chini zimekuwa zikiyabadilisha maamuzi ya mahakama za chini kwa sababu mbalimbali ikiwemo ya kutokuzingatia taratibu za kisheria za upokewaji ushahidi.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sharia wilaya ya Mkoani Nassor Hakim, anasema ni jukumu la jamii kufanya kila mbinu kuhakikisha wanafika mahakamani kutowa ushahidi.



‘’Waliowengine wanadhani hakimu na mwendesha mashataka, ndio wanaweza kumaliza kesi zote na msitakiwa kufungwa, wakati sio sahihi,’’anasema.

Mwanaharakati Omar Haji Omar Anasema si vyema kutovunjika moyo kwa kikwazo chochote kwani kufanya hivyo ndio kutoa mwanya wa kuzizimishwa kesi hizo.

Mratibu wa wanawake na watoto Shehia ya Mchanga mdogo Siti Khatib Ali anasema lazima jamii iungane  katika kutoa ushahidi.

Anasema wanaotenda matendo ya udhalilishaji wamekuwa wakifuatilia watu iwapo kama wanafika mahakamani  kutoa ushahidi ,na kama wanachoka na wao hupata nguvu ya kuyaendeleza matendo hayo.

Sheha wa shehia ya Kiungoni Wilaya ya Wete Omar Khamis Othman, anasema ushahidi mahakamani ndio kigezo cha mtuhumiwa kutiwa hatiani.

Anasema katika shehia yake wanajipanga kuhakikisha wanasaidiana nauli ili kufika mahakamani kutowa ushahidi.

Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Wete Haroub Suleiman Hemed anasema ni wajibu wa jamii katika kupambana na  kutokomeza udhalilishaji wa kijinsia jambo ambalo kabla walidhani ni la kazi ya taasisi fulani tu.

Arafa Abdi wa Mkoani anasema ni vyema kukapitiwa vyema sheria ya ushahidi, kwani haimtendei haki mtoto aliyefanyiwa udhalilishaji kwa vile hutowa ushahidi kwa alilofanyiwa na mwisho wa siku kesi hufutwa.

 “Tena maneno ya mara ya mwanzo ya mtoto aliyedhalilishwa ni bora yakarekodiwa kwani hakutokuwa na udanganyifu,”anasema.

WAATHIRIKA WA VITENDO VYA UDHALILISHAJI  

Baadhi ya watoto kuanzia miaka 5 hadi 17 ambao ni waathirika wa udhalilishaji, wanasema, elimu ya kujengewa ujasiri wa kutoa ushahidi mahakamani, imewasaidia.

 Bado kundi la watoto linakumbana na kadhia inayofanywa na baadhi ya watendaji wa vyombo vya sheria kwa kuchukuwa rushwa ya pesa na vitu vya thamani kwa lengo la kupotosha ushahidi.

“Sisi kama waathirika wa vitendo vya udhalilishaji hasa wenye hali ngumu ya kimaisha, hiyo tabia imekuwa ni changamoto kubwa yenye kutupa wakati mgumu,’’anasema mmoja.

Watoto hao walivitaka vyombo vya sheria kufanya kazi kwa uadilifu ili haki itendeke kwa pande zote  mbili ,na kuondosha tatizo hilo katika visiwa vya unguja na Pemba.



Hata hivyo walliiomba seikali kuwa kesi za udhalilishaji zisiwe na mawakili kwani ndio kichaka kikubwa wanachotumia upande wa mtuhumiwa  kwa wale wenye pesa zao  na uwezo  fulani  wa kifedha ama madaraka fulani .

VYOMBO VYA SHERIA

Mwanasheria dhamana ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Pemba Ali Haidar, anasema hakuna mashitaka ambayo mtu anatiwa hatiani, bila ya kuwepo mashahidi.

“Sisi waendesha mashtaka ,hatufahamu lolote  iwapo kuna kosa limefanyika vijijini ,sasa kama wakija watu kutoa ushahiodi au kupinga juu ya tendo fulani ,sasa hapo ndio ukweli hupatikana,”alieleza.

Hakimu wa mahakama ya Mkoa Chakechake Luciano Makoye Nyengo  anasema mashahidi wote wanaofika mahakamani wamekuwa wakipewa nauli zao kama kawaida .

Anasema kukosekana kwa nauli hiyo kusiwarejeshe nyumbani mashahidi, maana suala la kutowa ushahidi ni haki yao, hasa katika kuusaidia  muhimili wa mahakama , kufanikisha kazi zake.

“Jamii ijipange vyema kuhakikisha wanakuwa na hamu kufika mahakamani kutowa ushahidi ,kwani hakuna kesi ambayo itafikia tamati ,pasi na kuwepo kwa mashahidi, ”alisema.

                                        Mwisho                  

 

Comments

  1. Mzee baba unajitahidi kuchochea moto kwenye hiyo kesi ya Is-haka..!! Kheri!

    ReplyDelete

Post a Comment

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch