Skip to main content

MVUTANO WA TAFSIRI NANI MTOTO KIKWAZO KUTOKOMEZA NDOA, MIMBA ZA UMRI MDOGO ZANZIBAR

 

 

Na Haji Nassor, PEMBA

“Moto ni mtu aliechini ya miaka 18’’ ndivyo sheria namba 6 ya mtoto ya mwaka 2011 ya Zanzibar inavyotoa tafsiri ya nani mtoto.

 

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, yenyewe imeridhia kuwa mtu hatoweza kupiga kuram kama iwapo hatotimizia masharti yaliopo likiwemo la kufikia umri wa miaka 18.

 

Nayo katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, imekwenda mbali zaidi kwamba mtu hatochaguliwa kuwa rais kama hajatimiza umri wa miaka 40.

 

Huku taifa la Tanzania likifatua katiba mpya, hata rasimu ya awali ya katiba hiyo iliotolewa Juni 3 mwaka 2013, pamoja na mambo mengine, imerudi ikitaja umri wa miaka 18 ndio wa mtu uzima ndani taifa hili.

 

Tafsiri hii, imekuwa ikiiumisha kichwa jamii ya Zanzibar ambayo asilimia 99, imekuwa ikifuata Imani ya dini ya kiislamu na kuwepo kwa tofauti kubwa.

 

Ingawa tasfsiri ya nani mtoto huja kutokana na mazingira yake, na ndio maana kumbu kumbu zinaonyesha kuwa hata wakati wa ukoloni baadhi ya sheria hazikutaja umri wa miaka 18 kama ndio mtu mzima, bali ni mbali zaidi.

 

Sheria namba 6 ya elimu Zanzibar ya mwaka 1982, kifungu cha 19 kimetamka kuwa ‘itakuwa ni lazima kwa kila mtoto aliefikia umri wa miaka saba (7) lakini hajafikia umri wa miaka 13, kuandikishwa elimu ya msingi, na kifungu kidogo cha (3) kuwa, haruhusiwi mwanafunzi kuoa au kuolewa kabla ya kumaliza elimu ya msingi au sekondari ya awali.

 

Kumbukumbu hizo zilionyesha kuwa, sheria ya watoto na vijana ya ‘cap’ 58 ya mwaka 1952, sheria hii ilikaribiana na kabisa na imani za waumini wa dini ya kiislamu, maana yenyewe ilimtambua mtoto ni yule aliechini ya miaka 14 na sio miaka 18.

 

Ingawa sheria hii ilifutwa na sheria na kanuni mbali ikiwemo, sheria namba 6 ya mwaka 2011 ambayo yenye ilimtambua mtoto ni yule aliechini ya umri wa miaka 18, jambo ambalo jamii ya Zanzibar inakinzana na sheria hii.

 

Sheikh Mohamed Adamu Makame kadhi wa wilaya ya Mkoani, alisema inaweza kuwawiya vigumu wananchi wa Zanzibar, kuona kama ni kosa kumuozesha mtoto aliechini ya miaka 18, kwa vile Imani zao hilo haliendani.

 

‘’Wazanzibar ambao wengi wao wanafuata Imani ya dini ya kiislamu, wanaamini kuwa mtoto kwao ni yule ambae hajabaleghe kwa mwanamme na wa kike ambae hajapata ukubwa, na sio vyenginevyo’’,alisema.

 

Nae sheikh Mohamed Said wa mji wa Chakechake, alidakiza kuwa kuwa, ni vigumu kuwakataza wazazi ambae mwanae ameshamaliza masomo na amepata mume akiwa na miaka 17, eti kumsubiria mapaka atimize miaka 18.

 

‘’Kama seikali inataka kutokomeza ndoa na mimba za utotoni, lazima sheria zetu zimwe na mahusiano na Imani za wananchi wake waliowengi, kama ilivyokuwa na sheria za Sultan za kumtambua mtoto akiwa chini ya maika 14’’,alishauri.

 

Mzazi Hassan Rajabu Jecha (54) wa shehia ya Tibirinzi, yeye haoni kwamba ni kosa kumpa mwanae wa kike mume, eti kwamba hajatimiza miaka 18, kama inavyotaka sheria.

 

Mzazi Bikombo Simai Juma (45) wa shehia Kichungwani wilaya ya Chakechake, kwa upande wake, aliishauri serikali na watungaji sera hasa ambazo zinaonekana na maslahi kwa mtoto, kuhakikisha hazipingani sana na Imani zao.

 

‘’Mimi wanangu watatu wote niliwaozesha chini ya miaka 18, maana mmoja hakutaka kwenda skuli, mwengine alinijia na ujauzito na mwengine alifeli darasa la kumi, lakini kidini hawa sio watoto tena’’,alifafanua

 


Hakimu wa Mahakama ya mkoa Chakechake Khamis Ramadhan Abdalla, alikiri kukumbana na changamoto kama hizo kwenye kesi za mimba kutokana na jamii kufuata zaidi Imani zao za dini.

 

‘’Chakufanya ili kuondoa mimba na ndoa za utotoni, ni kwa wahusika wa utungaji wa sheria, kuhakikisha kuna uwiyano baina ya sheria hizo na imani za walengwa wa sheria’’,alifafanua.

 

Mgongano huo wa tafsiri wa nani mtoto ulioanzia hata kabla ya taifa la Tanzania na Zanzibar kujitawala miaka ya 1963 na 1964, sio gumzo wala tatizo kwa waumini wa dini ya kiislamu eti kuoa au kuolewa mtoto aliechini ya miaka 18.

 

Lakini hata wataalamu wa magonjwa ya akina mama hawakubaliani na umri wa miaka 18, kwamba ndio mtu mzima na tayari kwa kubeba ujauzito.

 

‘’Sisi hushauri sana kwamba umri sahihi wa kubeba ujauzito ni kuanzia miaka 20 maana hapo ndio viungo na mwili wake umeshajitayarisha kwa kuhidhi kiumbe’’,alisema dk Namie Ali.

 

Umri wa miaka 18 sio ruhusa ya kufanya kila jambo, inawezekana ni kwa ajili ya mambo mengine ya kiserikali na shughuli za kijamii.

 

Wanaharakati mbali mbali wa kupinga mimba na ndoa za utotoni, kwamwe haiingilii Imani za kundi moja au jengine, huku kubwa zaidi wakisistiza elimu kwa mtoto wa kike.

 

“Lakini kwa nini jamii hiyo inayofuata Imani za dini ya kiislamu, ikimbilie zaidi kwenye sunna ya ndoa na kuacha faradhi ya elimu kwa watoto wao’’,alitamka Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari Wananwake Tanzania TAMWA afisi ya Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali.

 

Wasatini wa kesi 20 hadi 25 za mimba na ndoa za utotoni kwa mwaka mmoja, zimekuwa zikifuatiliwa kwa kina na TAMWA, na hasa hupata ushirikiano baada ya kuwapa taaluma familia na watoto wa kike.

 

 Jamii haina budi kuweka mkazo maalum wa kuwasomesha watoto wao wa kike, ili waweze kujikomboa na kufahamu haki zao na kuondokana na utegemezi katika familia zao.

 

Fatma Marzouk Kombo yeye ni  Makamu Mwenyekiti wa Jumuia kuelimisha Athari za madawa wa kulevya, ukimwi na mimba za utotoni ‘JUKAMKUM’ , alisema tokea walipoanzisha jumuia yao, wamekaa kwa muda wa zaidi ya miaka mitano bila ya kupata fedha za kufanya kazi zao.

 

‘’Sisi tunakusudia kuwafikia watoto wa kike zaidi ya 2,000 kuwapa elimu ya kujikinga na mimba na ndoa za utotoni na tuliomba mradi kwa asasi kubwa ya kiraia na tumefanikiwa’’,alisema.

 

Hapa aliiomba jamii kuhakikisha wanawaunga mkono, ili kutokomeza wimbi la watoto wa kike kupata ujauzito na wakiwa chini ya umri wa miaka 18.

 

Baadhi ya wananchi wa mkoa wa kusini Pemba, wametaja chanzo cha mimba na ndoa z autotoni kuwa ni pamoja na mporomoko wa maadili ambao umechangiwa na utandawazi.

 

Muathirika wa ndoa ya utotoni mwenye (16) mkaazi wa shehia ya Kichungwani Chakechake, alisema yeye alilazimishwa kuacha masomo na wazazi wake, baada ya kutokezea waume wawili mfululizo.

 

“Alikuja mume wa kwanza niko darasa la tisa, na wa pili alikuja naanza kuingia darasa la kumi mwaka 2011 skuli ya Madungu na babaka akasema niloewe, na sasa nimeshaachwa’’,alifafanua.

 


Kijana huyo ambae kwa sasa yuko kwao shehia ya Kichungwani, aliolewa Juni mwaka 2012 na mwezi Mei mwaka 2013 aliachwa, na kwa sasa anatamani kurejea masomoni.

 

Baba wa kijana huyo miaka (55) alisema hilo lilijitokeza baada ya kutalikiana na mke wake, na mtoto huyo alikuwa akilelewa na bibi yake na baada ya kuonekana amebadili tabia ndio alifikia uamuzi huo.

 

Nae sheikh Ahmad Said kutoka afisi ya Mufti Pemba, alisema suala hilo linahitaji nguvu ya pamoja, ili kutokomeza mimba kwa watoto.

 

Mchungaji Benjamin Kissanga wa kanisa katoliki la kilutheri Tanzania, liliopo Alikhamis Chakechake, alisema maandiko yanakataza kuwakatisha masomo watoto, kwa kuwaozesha waume.

 

Idadi ya kesi za mimba na ndoa za utotoni zinaokena kutisha ndani ya mkoa wa kusini Pemba, na ndio maana kitakwimu ndani ya miaka miwili iliyopita wanafunzi wenye uwezo kujaa madarasa matatu 196 walikumbwa na majanga ya kuolewa na kupewa ujauzito.

 

Uchunguuzi ukabaini kuwa katia hao, 122 wameripotiwa kupewa ujauzito na 74 kuolewa wakiwa chini ya umri wa miaka 18, kuanzia kipindi cha mwezi Januari mwaka 2021, hadi mwezi novemba mwaka huu mkoa wa kusini Pemba.

 

Mwaka mmoja  pekee, kesi za mimba za utotoni zilikuwa 73, wakati kipindi cha mwezi Januari hadi Oktoba mwaka 2013, ziliripotiwa kesi 49 za mimba kwa wanafunzi.

 

Kesi za ndoa kwa wanafunzi, kulikuwa na idadi ya 54, kwa mwaka 2020 na mwaka 2021 kulipripotiwa kesi 20 katika taasisi mbali mbali.

 

Wizara ya elimu pekee ilikusanya jumla ya kesi 67 za mimba na ndoa, ambapo kati ya hizo, mwaka 2012 kesi za ndoa zilikuwa 38, wakati kesi za mimba kwa wanafunzi zilikuwa 14, wakati mwaka huu kumesharipotiwa kesi 9 za ndoa na 6 za mimba.

 

Shehia za Tibirinzi, Kichungwani na Madungu wilaya ya Chakechake kwa kipindi cha mwaka 2020/2021 zilirpoti kesi 25 za mimba na ndoa za utotoni, ambazo zote uchunguuzi umegundua zilifikishwa kituo cha Polisi wilayani humo.

 

 Vyanzo mbali mbali vya habari, vilisema chanzo cha kujitokeza kwa matendo hayo husababishwa na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na uhuru mkubwa wa wazazi wanaowapa watoto wao wa kike.

 

Sheha wa shehia ya Madungu wilaya ya Chakechake, Mafunda Hamad Rubea, aliweka wazi kuwa, kwa karne hii wazazi wamejisahau na kuwapa uhuru mkubwa watoto.

 

“Idadi ya kesi za mimba za utotoni zinaweza kuendelea kukuka siku hadi siku, kama wazazi wataendelea kuwaogopa watoto wao na kuwapa kila watakacho’’,alifafanua.

 

Afisa Mkuu wa dawati la jinsi na watoto la Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba, Asha Talib alisema kesi za mimba na ndoa za utotoni, zimekuwa tatizo sugu, kutokana na watendaji, na waathirika kuwa ndugu wa familia.

 

“Hata sisi dawati wakati mwengine hupata ugumu mkubwa wa kuzishughulikia kesi hizi, maana utakuta aliempa ujauzito mtoto ni kaka, ami, baba wa kambu, au mwalimu wake, sasa wanakua wazito hata kutoa ushahidi”,alifafanua.

 

Mratibu wa kituo cha mkono kwa mkono, Chakechake Fatma Abdalla Ali alisema, chanzo cha kesi hizo, ni kutokana na Polisi kuzifanyia sulhu kesi hizo katika hatua za awali.

 

‘’Polisi wamekuwa kama wanazichechea kesi za ndoa na mimba za utotoni, maana wamekuwa wakijifanya mahakama kwa kutoa sulhu, wakati walipaswa wazipekeleke juu’’,alifafanua.

 

Katika kipindi cha mwaka 2020/2021 dawati la jinsia na watoto la mkoa wa kusini Pemba,  liliripoti kesi 13, wakati kituo cha mkono kwa mkono kiliripoti kesi 61, huku wizara ya uwezeshaji ustawi wa jamii maendeleo ya wanawake na watoto, ilipokea kesi zaidi ya 30.

 


Wakati hayo yakijiri utafiti uliofanywa shirika la Plan la Uengereza limebaini kuwa watoto 14 milioni kwa mwaka waliochini ya umri wa miaka 18 huingia katika ndoa za mapema.

 

Huku nchi za Nigeria ikiwa na asilimia 75, ikiwafuatiwa na Chad yenye asilimia 68 sawa na Afrika ya kati, ambapo nchi ya Bangladeshi ikiripotiwa kua na asilimia 66 ya watoto wanaoolewa wakiwa chini ya umri wa miaka 18 nchi nyengine ni Mali, Georgia, India, Turkey na Ukraine zikitaja na utafiti kua ndio zinazoongoza.

 

Ambapo pia asilimia 48 ya wanawake wote walioolewa Uguja mkoa wa Kaskazini, waliingia kwenye ndoa wakiwa na umri kati ya 12 hadi 18, ikitofauti na wale wenzao wa kisiwa cha Pemba ambao pia utafiti huo ulioangaza na ukabaini kuwa, wanawake wenye umri wa miaka 12 hadi 18 sawa na asilimia 62, yaani kila wanawake 100 wanaoloewa 62 hua na umri huo.

 

 Hata hivyo ndani mwaka huu, tayari mahakama ya mkoa wa Chakechake, imeshawahukumu washitakiwa wanne akiwemo Abuu-bakari Mkulu Bakari (28), aliefungwa miaka 60 jela kwa kuwabaka watoto wawili, na Ali Mohamed Ali (22) alietiwa kifungoni miaka 30 nae kwa kosa la ubakaji.

Wakati umefika kwa jamii kufanga kibwebwe na kuona kua suala la mimba na ndoa za utotoni haziwatendei haki watoto wa kike.

                                                     Mwisho

 

 

     

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch