Skip to main content

WANAWAKE WATAJA MATAMU, MACHUNGU KAZI YA UBAHARIA-ZANZIBAR

 


NA ABDI SULEIMAN, PEMBA

KILA ifikapo Juni 25 ya kila mwaka, dunia huadhimisha siku ya bahari ulimwenguni.

Moja ya rasili za asili zenye matumizi lukiki, basi ni bahari iwe kwa usafiri, uvuvi, chanzo cha maji ya kunywa na dawa.

Wapo wanaoitumia bahari kuwa ndio chanzo chao kikubwa cha kuwapatia kipato, kutokana na shughuli zao mbali mbali ikiwemo uvuv.

Wakati juzi Juni 25, dunia iliadhimisha siku ya bahari, tunapaswa kujiuliza wale walioamua kujiingiza katika shughuli za ubaharia wako hali gani.

Ubaharia ni kazi kama zilivyo kazi nyengine, husikii baharia kugoma au kususia kazi kwa sababu moja au mbili tatu kutokea.

Miaka yote kazi ya ubaharia ilionekana ni kazi ya wanaume pekee, ingawa kwa sasa hali imekua ikibadilika na hata kwa wanawake kujiingiza.

 MABAHARI WANASEMAJE JUU KAZI HIYO

“Kwa sasa maisha yamebadilika, ubaharia ni kazi kama zilivyo kazi nyengine, chamsingi ni mtu mwenyewe kujiheshimu na kujitunza hapo utafanikiwa,”amesema bahari Zainab.

Zainab Ali Abrahaman mwanamke wa kwanza Zanzibar kuingia katika fani ya ubaharia wa meli, licha ya kazi hiyo kuwa ngumu aliweza kusema na moyo wake.

“Nilifanya kazi katika meli mbali mbali kama vile Ukombozi II, Mapinduzi II na hata Sea star, nilifika mafia kwa shughuli hizi za ubaharia wa meli,”anasema.

Shemsa Rajab Ali anasema kazi ya ubahari ni kazi kama zilivyo kazi nyengine, vizuri kufuata taraibu na kulinda thamani na kuthamini kazi husika.

KIPI KILIWAVUTA KWENYE UBAHARIA

Zainab anasema ni mapenzi na marafiki aliokuwa nao na kumitia moyo, na kuona anaweza kwaenda kufanya kazi kama mhudumu wa kawaida.

Baada ya mwezi mmoja na wiki tatu alikwenda kusomea mambo ya ubaharia (bahari) na uhandisi wa meli chuo cha ubaharia Dar es-Salam (DMI).

Shemsa anasema alikuwa akifanya kazi katika hoteli, baada ya kuona mafanikio madogo aliamua kwenda kusomea ubaharia, hii nikazi kama zilivyo kazi nyengine.

“Unaweza kufanya kazi miaka 20 ila kama haikua moyoni kuna siku utaiacha, ubaharia upo ndani ya moyo wangu na niliomba mungu siku moja kutimia ndoto yangu hiyo na imetimia,”amesema.

CHANGAMOTO GANI WANAKUMBANA NAZO

Shemsa anasema hakuna kazi ngumu kama ubaharia, waajiri bado wanaendelea kusimamia mishahara midogo, mpaka sasa wanalipwa shilingi 300,000 kwa mwezi.

“Vyumba vya kulala mabaharia wanawake kwenye baadhi ya meli ni shida, kutokana na kuwa vichache, ukichukulia maumbile ya mwanamke huwezi kumchanganya na baharia mwanamme,”amesema Shemsa.

“Baadhi ya meli vyumba ni sita au saba, wafanyakazi wengi ni wanaume unajikuta unalala chumba kimoja, meli ya Mpainduzi tu ndio mazingira mazuri kwa wanawake yalikuwemo,”amesema.

Zainab anasema mikataba ya kazi ni miezi sita au mwaka, hakuna kazi ya kudumu hiyo ni kawaida kwa mabaharia, ndio maana ikawa ngumu, kwa vile unatafuta maisha lazima ukubali tu.

“Fani yangu kwenye mashine ni vitu vinavyohitaji nguvu zaidi, ukiomba msaada kwa mwanamme unakumbana na masharti wewe ni mwanamke, nyundo nzito na lazima upige na unajikuta unachoka haraka lazima upambane nayo,”amesema.



MWAMKO WA WANAWAKE UKOJE KATIKA UBAHARIA

Kwa sasa mabaharia wanawake wameongezeka,  wengi wameamua kusoma ubaharia katika chuo cha ubaharia ‘DMI’, Zanzibar wapo zaidi ya 16 ambao wamejiingiza katika ubaharia.

Kwa sasa wanawake wapo nje hakuna aliyepo kazini, ni wazi Zanzibar bado hakujawa na uwelewa kujua umuhimu wa sekta ya bahari, hatujaitendea haki wengi wanaona ubaharia ni uhuni tu.

Aidha amewasihi wanawake na jamii kuachana na dhana potofu iliyozoeleka, kuwa kazi ya ubahari ni uhuni, akisema popote jambo hilo linaweza kufanywa au kuepukwa.

 

 USHAURI GANI KWA WANAWAKE

Wanawake wanapaswa kufahamua uchumi mkubwa ni bahari, wasitengemee kukaa nyumbani, na kumtegemea mume ama baba.

Aidha amewataka wazazi kuwasomesha watoto wao fani ya ubaharia, ni kama zilivyo nyengine, ili kazi hiyo isije ikavamiwa na watu kutokana nje ya Tanzania.

WANAUSHAURI GANI KWA SERIKALI

Wanasema kilio chao kikubwa ni serikali kuwaacha mkono mabaharia, wakati ndio sekta muhimu sehemu yoyote duniani.

baharia ndio wasimamizi wakubwa wa mizigo ndani ya meli baada ya kupakiwa kutoka sehemu moja kwenda nyengine, mfano dawa na chakula

Kuwaangalia kwa jicho la huruma mabahari wanawake kwa kuwasaidia, fani ya ubahari sio kama nyengine, vyeti vyao kila baada ya miaka minne wanatakiwa ukasome tena ili viweze kutumbulika.



 

MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI ZANZIBAR (ZMA)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri Baharini, (ZMA), Sheha Mohamed, amesema mabaharia wana mchango mkubwa katika kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii duniani.

 

Uchumi wa nchi unategemea usafiri wa baharini kwa kiwango kikubwa, hivyo ipo haja ya kuonekana uwepo wao na kuthaminiwa.

 

ZMA imekusudia kuleta mageuzi ya kiutendaji kwa mabaharia, ili wawe ni sehemu ya kuitangaza Zanzibar vyema wakati wanapotekeleza majukumu yao ndani na nje ya nchi.

 

Anasema mabaharia wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo, kukosa fursa za kielimu na kiuchumi hivyo hawana budi kushikana mikono.

 

 

‘’Tayari tumekua na mabaharia wanawake ambao wameonesha umahiri mkubwa katika kazi yao, tayari tumewaagiza wamiliki wa meli kuweka vyumba maalumu kwa ajili ya mabaharia wanawake,’’anasema.

 

CHUO CHA UBAHARIA TANZANIA (DP/PEA)

Makamu mkuu wa Chuo cha Ubaharia Tanzania Dk.Tumaini Shamban Gurumo, mabaharia wanapaswa kuthaminiwa kwani wanaitangaza vyema nchi yao, hivyo wanapaswa kujiongeza kielimu ili kufikia malengo zaidi.

“Niwakati wenu kujiongeza katika eneo moja kwenda jengine, kulingana na mabadiliko yaliyopo hivi sasa duniani,”amesema.

TAASISI YA WANAWAKE WANAOFANYA KAZI BAHARI AFRIKA MAHSARIKI NA KUSINI (WOMESA)

Mwenyekiti wa ‘WOMESA’ Fotnata Makoyi Kwakaya, amewataka wanawake kutokujiweka nyuma na kutumia fursa zilizopo katika bahari ili kushiriki ipasavyo kama ilivyo wanaume.

Ameitaka jamii kuwahimiza watoto wa kike kujiingiza katika sekta ya ubaharia, kwani dunia imebadilika kulingana na teknolojia kwani wanawake wanaweza kufanya kazi hizo kama ilivyo wanaume.

Mhandisi wa meli Farida Shambani, amesema sekta ya bahari ni pana zaidi zamani wanaume walikuwa wengi, ila sasa dunia imebadilika hata wanawake wamo.

Anasema mwanamke yoyote  anaweza kufanya kazi kama mwaname, inategemea na uwezo wa mwanamke wenyewe na jinsi gani alivyokubali na kuikubali mwenyewe.

“Fursa zipo nyingi meli nyingi zinajengwa, bado mabahari wanawake ni kidogo na mahitaji ni mengi, kila siku meli zinafanya safari,”amesema.

katika kipindi cha COVID 19 mabaharia walijitolea na kuweka roho zao rehani, ili kuhakikisha mahitaji yanapatikana duniani licha ya kuwepo mazuilio katika mipaka.

 TASAC INASEMAJE

Mwenyekiti wakala wa shirika la meli Tanzania (TASAC), Kepten Mussa Hamaza, anasema Tanzania ndio nchi pekee vyenye mabaharia wazuri katika meli za kimataifa, hivyo wanapaswa kuendelea kulinda heshima na tahamani yao wanapokua duniani katika harakazi zao za kazi.

Amesema mwaka 2019 dunia ilikubwa na ugonjwa wa COVID 19, lakini mabaharia waliendelea kufanya kazi zao duniani kote ili matifa yaendelee kupata huduma mbali mbali ikiwemo vyakula.

“Mabaharia waliacha familia zao na kuendelea kutoa huduma duniani, meli zilisafirisha dawa, vyakula hata misaada kwa nchi zilizokubwa na janga la Covidi 19, hii ni kuonyesha kuwa bado mabahari,”amesema.

VIONGOZI WA SERIKALI WANASEMAJE JUU YA UBAHARIA

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud, amesema usafiri wa baharini ni muhimu katika kufikia uchumi wa viwanda, hivyo mabaharia wanapaswa kuthaminiwa na kuheshimiwa kutokana na kazi yao wanayoifanya kila siku.

Amesmea bado wanawake ni changamoto katika ubaharia, lazima taasisi husika zitowe nafasi kubwa kwa wanawake kuingia katika fani ya ubaharia kwani nifani kama zilivyo fani nyengine.

Waziri ujenzi na Uchukuzi Tanzania Profesa Makame Mbarawa Mnayaa, amesema asilimia 90 ya usafirishaji wa bidhaa duniani hutumia usafiri wa baharini, Zanzibar tayari imeshaanza ujenzi wa bandari ya kisasa itakayorahisisha usafiri.

Kujengwa kwa bandari ya Mangapwani, itaweza kubadilisha maisha ya uchumi wa Zanzibar kupitia baharini.

Amesema sekta ya bahari mara nyingi wafanyakazi wake ni wanaume, ila anaamini wanawake wanauwezo mkubwa na wanaweza kwani wanapoingia huko wataweza kuhamasisha na wanawake wenzao.

MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch