Skip to main content

WAZAZI WAONESHWA NJIA KUFANIKISHA MAENDELEO YA ELIMU KWA WATOTO

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

JAMII imetakiwa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika zoezi zima la ufundishaji na ujifunzaji kuanzia kwenye ngazi ya familia kwa kuwasaidia watoto na kumtengenezea mwanafunzi mazingira rafiki ya kujifunza kwa urahisi.

Hayo yameelezwa na Meneja Mwandamizi wa Uratibu na Programu katika mradi wa Boresha Elimu ya Sekondari Zanzibar, John Masenza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu wa Hesabati, Sayansi na Kiengereza.

Alisema kuwa, ikiwa jamii itashiriki kikamilifu katika ufundishaji na ujifunzaji itasaidia wanafunzi kupata maarifa kwa urahisi hususani katika masomo ya Hesabati, Sayansi na Kiengereza ambayo kwa sehemu kubwa yameonekana kuwa na changamoto kwa elimu ya Sekondari.

“Mradi huu tunautekeleza Zanzibar na tunakududia kuwafikia walengwa 220,000 wakiwemo walimu, wanafunzi, kamati za skuli, wakaguzi na wadau wengine wa vituo vya walimu kwenye HUB”, alisema Meneja huyo.

Alisema kuwa, katika kufanikisha malengo ya mradi wanakusudia kuboresha uwezo wa walimu wa Sekondari katika kutekeleza mtaala unaolenga kwenye ujuzi, uwezo na umahiri wa wanafunzi unaosaidia zoezi la ufundishaji na ujifunzaji, ambao unatakiwa umlenge mwanafunzi zaidi.



Aidha alieleza kuwa, mradi unakusudia kuimarisha mifumo na mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kwa kuvijengea uwezo vituo vya walimu na kuhamasisha ushiriki wa jamii katika kufuatilia maendeleo au ubora wa elimu kwenye skuli zinazoizunguka jamii.

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzio ya Amali Pemba, Kaimu Mratibu Idara ya Mafunzo ya Ualimu WEMA Mzee Ali Abdalla alisema, alilipongeza sana Shirika la good Neighbors kwa kutoa mafunzo hayo, yenye lengo la kuboresha elimu ya Sekondari Zanzibar.

Alisema kuwa, kwa dunia ya leo mfumo wa elimu unaotakiwa ni wa ujifunzaji kwa kuzingatia yanayofundishwa darasani yaendane na uhalisia katika maisha, ili watakapomaliza kidato cha nne waweze kujua pakuanzia kutokana na mbinu pamoja na ujuzi ambao wamefunzwa wakiwa skuli kwa miaka minne.

“Tunataka ufundishaji huu umguse kila mwanafunzi kwa kutumia mbinu mbali mbali na ujuzi ili kufikia malengo, mtaala wa sasa tunapendekeza kumfikia mwanafunzi na tunampa elimu ili aweze kuja kuakisi katika maisha ya kawaida”, alisema.

Kwa upande wao walimu waliopata mafunzo (resources trainers) hayo walisema kuwa, kupitia mafunzo hayo wanaamini kwamba wanafunzi watabadilika na kuongeza ufahamu pamohja na kiwango cha ufaulu kwa masomo hayo.

Mwalimu wa skuli ya Sekondari Madungu Chake Chake Hasanati Said Suleiman alisema, amejifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kubaini kuwa mwanafunzi anaweza kujifunza kwenye njia tofauti, mbali na ile waliyoizoea.

“Kuna hii teknolojia ya kujifunza lakini hatuitumii, kwa hiyo katika mafunzo haya nimepata kujua kuwa teknologia ni kitu muhimu katika kuwafunza watoto wetu”, alisema mwalimu huyo.



Aliishauri Wizara ya Elimu kujaza vifaa bora kwenye vyumba vya maabara ambavyo vitawasaidia wanafunzi kufanya kwa vitendo sambamba na kujengwa HUB mbali na skuli, ili kuepusha usumbufu kwa wanafunzi wakati wanapoendelea na masomo.

Mwalimu wa skuli ya Sekondari Msuka Seif Juma Said alisema kuwa, mafunzo hayo yatakuwa na tija kwa walengwa wote, kwani kupitia yeye atafikisha ujumbe huo ambao hapo awali haukuwepo katika skuli hiyo.

“Mafunzo haya yana tofauti kubwa na yale tunayofundisha kawaida, kwa sababu tuliamini kuwa mwalimu ndio anajua kila kitu na mwanafunzi hakuwa na nafasi yeyote kwenye ufundishaji, lakini kumbe mwanafunzi ana mengi anayoyafahamu na alipaswa atawale kwa asilimia 100”, alifafanua.

Mhadhiri wa chuo cha elimu kutoka UDOM Dk. Francis William ambae alikuwa mkufunzi wa masomo ya hesabati alisema kuwa, lengo ni kuhakikisha walimu wanajenga uwezo na umahiri mkubwa katika kuhakikisha wanafuata mtaala ambao unahitaji walimu wanavyosaidia wanafunzi kujifunza, waweze kujenga mahiri kwenye maeneo ya maarifa, stadi na mielekeo, ili kile wanachojifunza wakitumie katika maisha yao ya baadae.

“Tumekuwa hapa kwa siku sita za kufundisha na tunatengeneza resources trainers hivyo tutakuwa na wataalamu ambao wamebobea katika masomo haya ya sayansi, hesabati na kiengereza”, alisema.

Mradi huo wa miaka minne unatekelezwa na Shirika la Good Neighbors Tanzania chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Korea (Koica) ambao unakusudia kuwafikia walengwa 220,000.

                                             MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch