Skip to main content

TAMWA-ZANZIBAR: 'HAILALI HADI KUWA NA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

MOJA ya sheria kongwe na inayotajwa kutokwenda sambamba na uhuru wa vyombo vya habari, ni ile nambari 5 ya mwaka 1988 ya Magazeti, Vitabu na Mawakala wa Habari Zanzibar.

Ni miaka 34 sasa, sheria hii inaendelea kutumika Zanzibar, na kutajwa kuathiri na kutishia utendaji kazi wawaandishi wa habari visiwani.

HISTORIA

Sheria hiyo tokea mwaka 2010, ilianza harakati za kutaka kufutwa, kwa wadau wa habari kujikusanya pamoja, ili sasa iwe na sheria moya ya habari.

Kwa wakati huo, tasisi za Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ –ofisi ya Zanzibar, vyama vya waandishi wa habari, taasisi za haki za binadamu na wizara husika, zilianza harakati hizo.

Mara kadhaa, kulikuwa na taarifa kuwa, mwaka ujao au mwakani Zanzibar itapatikana sheria mpya ya habari, ambayo itakuja kufuta sheria ya Magazeti nambari 5 ya mwaka 1988 na ile ya Tume ya Utangaazji nambari 7 ya mwaka 1977.

Ilikuchakua takriban miongo miwili, kupita bila Zanzibar kuwa na sheria mpya, ingawa kwa Tanzania bara, wao walifanikiwa kufuta sheria ya Magazeti ya mwaka 1976, na kuwa na sheria ya Huduma ya vyombo vya habari ‘MSA’ ya mwaka 2016.

Aliyewaji kuwa Katibu mkuu wizara ya Habari Ali Mwinyikai, alisema iko siku Zanzibar, itakuwa na sheria bora na iliyorafiki kwa waandishi wa habari.

Hata aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa shirika la Magazeti ya serikali Zanziba Abdalla Mohamed Juma, aliwahi kusema, sheria ya magazeti, iliyopo sasa, haiendani na upevukaji demokrasia.

Kwa miongo miwili, wadau wa habari juhudi zao za kuwa na sheria mpya ya habari ziligonga ukuta, na harakati hizo zikaanza tena miaka ya 2018/2019.

YANAYOWASKUMA WADAU KUFUTWA KWA SHERIA YA MAGAZETI, VITABU NA MAWAKALA WA HABARI NO 5, 1988.



Sheria hii yenye vifungu 81 na sehem 10, sasa inatimiza miaka 34, tokea kutungwa kwake, na kwa maana nyingine, vipo vifungu zaidi ya 40, ambavyo vyengine vinahitaji kufutwa.

Vifungu vyengine vikihitajika kufanyiwa marekebisho na vyengine, vilivyobeba maneno makali kama uwezo wa waziri, waandishi kudhibitiwa na kufanya uchochezi.

Kwenye sheria hii, ambayo kwa sasa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar kwa ufadhili wa Internews, wanaharakishwa kufutwa kwa sheria hiyo.

VIFUNGU KANDAMIZI KWA UHURU WA HABARI

Moja ya kifungu ambacho, kwa sasa wadau wanataka kifutwe ni kile cha 43, ambacho chenyewe, kinaeleza ‘uwezo wa ofisa aliyeidhinishwa’.

Ambapo kwa mujibu wa sheria hiyo, ofisa aliyeidhinishwa ni Polisi mwenye cheo cha Msaidizi Ofisa Mkaguzi au mwenye cheo cha juu ya hapo.

Mchambuzi wa sheria za habari Zanzibar Hawra Shamte anasema, kwa sasa sheria hiyo na hasa kifungu cha 43 wanakiona, hakina mantiki.

‘’Makosa yote yanayotokana na waandishi wa habari yana sura ya madai na sio jinai, sasa iko wapi nafasi ya Polisi kuingia, kupekua kwenye vyombo vya habari,’’anahoji.

Ukali wa mchambuzi huyu wa habari, unajidhihirisha kwenye kifungu hicho cha 43 (1) na (2) ambavyo vimeeleza wazi mamlaka ya ofisi huyo wa Polisi.

‘’Mfano kifungu (2) (a) kinaeleza uwezo wa ofisi huyo kuwa ‘anaweza kuingia sehemu yoyote, jengo, chombo cha ardhini, angani ambamo anaamini kwa maoni kuwa, mna vifaa vya habari, vilivyopangwa au vitakavyopangwa kukusanyia habari,’’   

 Hata kifungu kidogo cha 2 (b) kikaongeza kuwa, ofisi huyo anaweza ‘kuchunguza mchakato wowote ambao unaonekana kuelekea kukusanya au kutoa habari yoyote ’.

Kubwa zaidi ambalo ni ukiukwaji wa uhuru wa habari, kifungu cha (c) kinampa uwezo ofisi hiyo ‘kumtaka mwandishi wa habari yeyote, kutoa vitendea kazi vyake, gazeti au waraka ambao, uko chini yake kukabdhi kwake’.

Kifungu 2 (d) ofisi huyo amepewa mamlaka ya ‘kunakili sehemu yoyote ya vitendea kazi vya waandishi wa habari au akiamiani tu kufanya hivyo, kuna uhusiano na uchunguuzi wake juu ya kosa chini ya sheria hii’.

Kubwa zaidi, pia ofisi hiyo kwenye kifungu hicho cha 43 (2) (e) anaweza ‘kuagiza taarifa zenye uhusiano na uchunguuzi wake kutoka kwa mtu yeyote, ambae anaamini aliajiriwa au ataajiriwa katika jengo alilokuwa akitunza kumbu kumbu’.

Pamoja na uwezo huo, ambao wadau wa haki za uhuru wa habari wanaona ni uminywaji wa haki za waandishi wa habari, sasa kifungu cha 44 kimekuja kumlinda.

Kifungu hicho 44 (1) kinaeleza kuwa, ‘mtu yeyote atakayempinga, kumzuia, au kumkwaza kwa ofisa huyo atakuwa ametenda kosa’

Na adhabu kwa kosa hilo lipo kifungu cha 73, ambapo ni faini ya shilingi 200,000 au kifungo cha miaka miwili chuo cha mafunzo au adhabu zote mbili kwa pamoja.

WADAU WA HABARI WANASEMA JE?

Meneja wa redio Jamii Micheweni Ali Massoud Kombo, anasema kifungu hicho sio rafiki, na hakitarajii kukiona kwenye sheria mpya ijayo ya habari.

Anasema, studio na vyumba vya habari ni ofisi nyeti kama zilivyonyengine, hivyo utaratibu wa kuingia, uwepo kama zilivyo ofisi nyingine.

‘’Mbona Ikulu, wodi ya wazazi, kambi za Jeshi na hata chuo cha mafunzo kuna utaratibu wake, na sio ofisa yeyote tu Polisi tena kwa maoni yake aweze kuingia,’’anahoji.

Mmiliki wa mawio tv online Suleiman Rashid Omar, anasema kifungu hicho hakifai kuwepo, maana kinahalalisha ukandamizaji wa uhuru wa waandishi wa habari.



Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ Kajubi Mukajanga wakati akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba wiki iliyopita, alisisitiza vyombo vya dola kuwaachia waandishi watekeleze kazi zao.

‘’Kuwapasha habari wananchi juu ya matukio ya ndani na nje ni haki kikatiba, sasa kama kuna sheria au kifungu kinampa uwezo mkubwa Polisi kuingia na kufanya atakavyo sio sahihi,’’anasema.

Mratibu wa TAMWA -Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, anasema uhuru wa waandishi wa habari ni mbolea kwa taifa kutimiza malengo yake.

‘’Lakini sheria yetu ya Mgazeti nambari 5 ya mwaka 1988 ya Zanziba na hasa kifungu cha 43 kinaipinga hata katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, iliyotoa haki ya kutoa maoni,’’anaeleza.

Mjumbe wa Kamati tendaji wa Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAZA’ Hidaya Mjaka Ali, anasema sheria bora ni chachu ya kupata waandishi wa habari bora.

Mkurugenzi wa vijana Pemba Ali Mussa anasema wanawategemea mno waandishi wa habari kuwaibulia changamoto za vijana na kuwaonesha njia.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kuskazini Pemba Juma Saadi Khamis anasema, sio maoneo kama vyumba vya habari kuwa ofisa, anaweza kuvamia ikiwa hakuna uhalifu.

Mdhamini wa Baraza la Habari Tanzania MCT-Zanzibar Shifaa Said Hassan, anasema sheria hiyo imeshapitwa na wakati na moja ya vifungu vibaya ni cha 43 na vifungu vyake vidogo.

‘’Haiwezekani suala la haki ya kikatiba ya kupata na kutoa habari, apewe uwezo wa kupindukia Polisi, juu ya kuingia na kupekua kwenye ofisi za waandishi wa habari,’’anasema.

Mchambuzi wa sheria za Habari Zanzibar Hawra Shamte anasema, kwenye nchi zinazojali kwa vitendo utawala bora na utawala wa sheria, suala la kupata na kutoa habari haliwekewi masharti mazito.




 Mkuu wa Chuo cha uandishi wa habari na Mawasiliano ya Umma Zanzibar Imane Duwe, anasema dunia ikisherehekea ukuaji wa teknologia kwenye eneo la habari, lazima waandishi wawe huru.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari Zanzibar ‘ZPC’ Abdalla Abudull-rahman Mfaume na mwenzake wa PPC Bakari Mussa Juma, wanasema vifungu ambavyo vinampa wasi wasi waandishi wa habari havina nafasi Zanzibar.

Mhariri wa habari wa shirika la Magazeti ya serikali Zanzibar Juma Khamis Juma aliwahi kusema kuwa, ukuaji wa maendeleo ya taifa lolote duniani, waandishi wa habari mchango wao upo.

NINI KIFANYIKE?

Kaimu Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Pemba Safia Saleh Sultan, anasema lazima kwenye sheria ijayo ya habari, kifungu hicho kifutwe.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wasioona ‘ZANAB ‘Pemba Suleiman Mansour, amesema lazima suala la vyumba vya habari au wao wenyewe kupekuliwa lisiwe la kila ofisa wa Polisi.

‘’Sheria ijayo ya habari, sitamani kurejeshwa kwa kifungu hichi, maana kwa upande mwengine ni kudhoofisha juhudi za waandishi katika kazi zao,’’anasema.

Afisa Mdhamini wizara ya Habari Pemba Mfamau Lali Mfamau, anasema ukandamizwaji wa waandishi wa habari, hudhoofisha maendeleo ya taifa.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, anasema sheria bora ya habari huchangia kuwa na jamii bora na inayofanya uamuzi sahihi.

Zuhura Juma Said mwandishi wa habari wa shirika la Magazeti Pemba, anasema sheria hiyo ya Magazeti, Vitabu na Mawakala wa Habari nambari 5 ya mwaka 1988, imekuwa kikwazo kwao.

Mwandishi wa habari wa kituo cha tv na redio cha Zenj fm Amina Ahmed, anasema sheria hiyo hasa kwenye upatikanaji wa kibali umekuwa shida.

Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzur Issa Ali, anasema ujio wa sheria mpya ya habari vifungu vinavyompa uwezo mkubwa waziri visiwmo.

Mratibu wa uchechemuzi wa upatikanaji wa sheria ya habari Zanzibar kutoka TAMWA-Zanzibar Muhammed Khamis, anasema wakati umefika Zanzibar kuwa na sheria rafiki.

‘’Ndio maana TAMWA -Zanzibar kwa kushirikiana na wafadhili wetu Shirika la Internews Tanzania tunaomradi wa miezi minne, ili kuwawezesha waandishi, kusukuma upatikanaji wa sheria mpya habari Zanzibar,’’anasema.

                                  Mwisho


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch