Skip to main content

SENSA MWARUBAINI KUMALIZA CHANGAMOTO ZA WATU WENYE ULEMAVU, WAOMBWA KUSHIRIKI

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imepanga kufanya sensa ya watu na makaazi, ifikapo Agosti 23, mwaka huu wa 2022.

Sensa hufanyika kila baada ya miaka 10, na ya mwisho ni ile iliyofanyika mwaka 2012, ambapo hii ya mwaka 2022 itakuwa ni ya sita kufanyika.

Zilizowahi kufanyika ni zile za mwaka 1967 kisha mmwaka 1978, 1988, 2002 na ile ya mwisho 2012.

Maana ya Sensa ya Watu na makaazi

Ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua, kutathmini, kuchapisha na kusambaza takwimu za kidemografia.

Lakini pia ni kiuchumi na kijamii kuhusiana na watu wote na makaazi yao katika nchi kwa kipindi maalum.

Wapo wanaosema kuwa sensa ni zoezi maalumu lenye lengo la kupata idadi ya watu wote katika nchi, kwa umri na jinsia, mahala wanapoishi na hata hali yao ya elimu.

Takwimu hizo za msingi, ndizo zinazoanisha mahitaji halisi ya wananchi yakiwemo makundi maalum, yenye mahitaji maalumu, kwa mfano watu wenye ulemavu, wanawake, watoto, vijana na wazee.



Watu wenye ulemavu na sensa

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wasioona Wilaya ya Chake Chake (ZANAB) Suleiman Mansour anasema, watanufaika kwa sababu ni agizo la Serikali lenye lengo la kujenga.

Anasema, Serikali ni chombo ambacho kinahudumia watu wake kwa idadi waliyonayo, hivyo wao watakaposhiriki zoezi hilo itajulikana idadi yao na kuweza kutafutiwa mahitaji yao yanayotosheleza.

“Sisi ni watu wenye mahitaji maalum, Serikali ndio yenye dhamana kwa watu kama sisi, hivyo bila kujua idadi yetu halisi watafanya kitu kwa usahihi,’’anasema.

Anaamini serikali inapojua idadi ya watu, ni sawa na kujua mahitaji ya binadamu, kwa hiyo ikiwa wazazi na walezi watawaficha watu wenye ulemavu, watawakosesha haki zao za msingi.



Said Omar Said ambae ni Mwenyekiti wa Viziwi wilaya ya Chake Chake anasema, sensa itasaidia watu wenye ulemavu, moja ni kujua idadi yao kamaili.

“Tutajulikana ni watu wangapi wenye ulemavu na tunahitaji kitu gani, hivyo itakuwa ni rahisi kutatuliwa changamoto zinazotukabili”, anasema.

Anaishauri jamii kushirikiana pamoja, katika kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kushiriki zoezi la sensa kwa lengo la kufanikisha, kwani ni muhimu katika maisha yao.

Sahia Seif Salum wa Jumuiya ya wasioona ‘ZANAB’ Chake Chake anasema, sensa itawasaidia hata mgawanyo wa rasilimali elimu na afya.

Kubwa anasema ili kufanikisha hilo, sasa ni jukumu la wazazi na walezi kuwafichua watu wenye ulemavu wakati utakapofika.

“Watu wenye ulemavu watakapojitokeza kwenye zoezi la sensa ya watu na makaazi, sasa changamoto zetu ni kuzinyooshea njia kumalizika,’’anasema.

Hafsa Yussuf Abdul-rahman mkaazi wa Kifumbikai Wete ambae ni kiziwi anasema, watakapohesabiwa wanaamini kwamba changamoto zao nyingi zitatatuka.

‘’Nasoma chuo cha Mwalimu Nyerere Chake Chake lakini sioni huduma hata moja zinazotuwezesha sisi viziwi, nimezoea kumuangalia mwalimu mdomoni tu, hivyo naamini hii sensa itakuja na suluhgisho,’’anaeleza.



Mratibu wa Baraza la Taifa la Watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk anasema, hana shaka bali senda itakuja na matokeo bora kwa watu wenye ulemavu.

 “Lengo ni kupata idadi ya watu katika nchi na kuweza kuandaa na kupanga mikakati thabiti ya maendeleo, hivyo watu wenye ulemavu ni sehemu ya jamii”, anasema.

Anazidi kuanisha faida ya sensa kwa kundi hilo, ni kuwa na idadi kamili, kujua mahitaji yao ya msingi, aina ya ulemavu wao.

Kupitia sensa Serikali itajua kwamba wanahitaji vitimwendo vingapi au kuna wasomi wangapi na hivyo hata katika masuala ya ajira wanaamini kwamba watapata fursa ya kuajiriwa kutokana na idadi ya wasomi waliopo.  

Mratibu huyo anaeleza kuwa, sensa itapunguza changamoto kwa watu wenye ulemavu kwa sababu wataingizwa katika mpango wa maendeleo ya nchi, jambo ambalo litasaidia kutapata mahitaji yao.

“Ikiwa watu wenye ulemavu watafichwa, hawatojulikana idadi yao na wala hakutojulikana kwamba wana uhitaji wa vitu gani na gani, hivyo wanaweza kukosa haki zao za msingi”, anaeleza Mratibu huyo.

Aziza Alawi Mussa ambae ni Mjumbe wa Shirikisho la Jumuia za watu wenye Ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ Pemba, anasema, walipewa taarifa katika Jumuiya yao, juu ya uwepo wa zeozi hilo.

 Kwa ngazi ya awali tayari viongozi wao kwa kushirikiana na viongozi wengine wa Jumuiya za watu wenye ulemavu, wameingia kwenye maeneo ya kamati za wilaya mpaka mkoa na tayari zimeshafanya kikao cha awali.

Anataja athari inayoweza kujitokeza iwapo watu hao hawakupata fursa ya kuhesabiwa kuwa ni, Serikali haitakuwa na takwimu sahihi za kupanga mipango yake ya kila siku.

Khalfan Amour Mohamed kutoka Jumuiya ya Watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar ‘ZAPDD’ anasema, sensa inaweza kuwasaidia watu wenye ulemavu katika nyanja tofauti.

‘’Kwa watu wenye ulemavu ni kwamba, baada ya zoezi hilo serikali itajua kuwa, katika nchi kuna watu wangapi wenye ulemavu na kujua aina ya mahitaji yao,’’anasema.

 Yeye anaona itakapofanyika sense, Serikali itajua na itajipanga kuweza kuleta yale mahitaji maalumu ambayo yamekuwa yakililiwa kwa siku nyingi na watu wenye ulemavu wa akili.

Jumuiya yao imejipanga kuhakikisha wanatoa elimu ya kuhamasisha, watakutana na viongozi wa matawi ya Jumuiya zao ambapo kwa Pemba ni 30, ili kuwaelimisha na wao wachukue juhudi ya kuwahamasisha wazazi na walezi.

Raya Mohamed Nassor mwenye ulemavu wa viungo anasema, ni muhimu kwa watu wenye ulemavu kuhesabiwa kwani Serikali itaona kwamba wapo na wanahitaji kutatuliwa changamoto zinazowakabili kwa mujibu wa idadi yao.



Halima Bakar Ali ambae ni mkaazi wa Wete anasema kuwa, sensa ni muhimu sana kwa wananchi, kwani inaisaidia Serikali kupata taarifa za msingi ambazo zitapelekea kuchapuza maendeleo katika nchi.

Ali Omar Ali mkaazi wa Ole Wilaya ya Chake Chake anasema, kuna watu wenye ulemavu wengi ambao hawajajiunga na jumuiya zinazoshughulikia watu hao, hivyo idadi yao halisi haijulikani.

‘’Watakapohesabiwa itajulikana kuna watu wa aina hiyo wangapi, wanaosoma na wasiosoma wanagapi na ndipo Serikali itakapojua kunatakiwa kitu gani cha kuwasaidia na idadi yake’’, anaeleza Ali.

Mkurugezi wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar Ussi Khamis Debe amewasisitiza watu wenye ulemavu kuchangamkia zoezi hilo.

‘’Hakuna mahali ambapo sasa kuna taarifa rasmi juu ya idadi na mahitaji ya watu wenye ulemavu, lakini ujio wa sense hii yam waka 2022, itakuwa ndio suluhisho,’’anasema.

“Nitoe wito kwa wazazi na walezi pamoja na watu wenye ulemavu kujitokeza kuhesabiwa na wasione kwamba ni mkosi au nuhsi hapana, hiyo ni mitazamo potofu”, anaeleza.

Mkurugenzi huyo anasema, watu wenye ulemavu ni sehemu ya jamii na ni sehemu ya wananchi wa Zanzibar, hivyo ni vyema wakajitokeza, wahesabiwa.

Sensa ni muhimu kwani husaidia kupata taarifa za idadi ya watu, katika mamlaka za Wilaya kwenye utekelezaji wa mipango ya maendeleo ambayo huakisi matakwa ya watu katika ngazi husika na kusaidia kwenye mgawanyo wa rasilimali.

                                                 MWISHO.

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch