Skip to main content

RC KUSINI PEMBA 'KADA YA SHERIA ITABAKI NGUZO MUHIMU KWA JAMII'

 



 

MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amesema kada ya sheria itaendelea kuwa eneo muhimu katika jamii.

Alisema, kwa kulitambua hilo Serikali, iliamua kutunga sheria mahusisi ya msaada wa kisheria nambari 13 ya mwaka 2018, na kuanzishwa Idara ya Katiba na Masada wa Kisheria, ili kuwafia wananchi kuwapa elimu, ushauri na msaada wa kisheria.

 Alisema idara hiyo imekua ikifanya kazi kubwa katika masuala mbali mbali ya msada wa kisheria Zanzibar, ili kuona wananchi wasio na uwezo wanapata haki zao za kisheria.

Mkuu huyo aliyasema hayo Mei 12, mwaka 2022 wakati akiyafungua mafunzo ya kwanza ya siku 15 kwa wasaidizi wa sheria 15 wa majimbo yote kisiwani, yanayoendelea Gombani Chake chake.

Alisema kada ya wasaidizi wa sheria, inasaidia kwa kiasi kikubwa  kuwafahamisha wananchi hususani wa ngazi za chini katika jamii, juu ya haki zao za kisheria na namna ya kufuatilia.

“Mafunzo haya ni muhimu kwenu washiriki, ili mukitoka hapa muweze kwenda kutekeleza majukumu yenu kwa uweledi na malengo yaliokusudiwa, hizi sheria mutakazofundishwa mukazifanyie kazi,”alisema.

Kwa upande wa rushwa alisema matukio mengi yanafanywa katika jamii, wanaoathirika ni wananchi hivyo wasaidizi wa sheria wanapaswa kwenda kuwafahamisha juu ya suala hilo.

Mkuu huyo aliipongeza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, skuli ya sheria ya Zanzibar kwani kuwepo kwa skuli hiyo ni faraja kwenye kada ya sheria nchini.



Kwa upande wake Afisa Mdhamini Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais katiba sheria utumishi na Utawala bora Pemba, Halima Khamis Ali, alisema Idara, inajukumu la kusimamia masuala ya kisheria, hivyo wasaidizi hao wamechaguliwa kwa mahitaji ya jamii husika.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanizbar Hanifa Ramadhan Said, aliishukuru shirika la ‘LSF’ kwa kuendela kuwaunga mkono katika masuala mbali mbali ya kisheria.

Alisema mchakato wa kuwapata wasaidizi hao, ulikuwa mkubwa Unguja maombi yalikua zaidi ya 400 kwa Unguja na wanaohitajika ni wasaidizi 32, ambapo kwa Pemba maombi yalikuwa zaidi ya 200 wasaidizi wanaohitajika ni 18, hivyo wasaidizi hao wanapaswa kuthamini nafasi waliopatiwa.



Aidha alisema licha ya kupatikana kwa wasaidizi 32 Unguja na Pemba 18, lakini bado kunahitajika wasaidizi wa sheria wengi ili kufikia shehia zote za Zanzibar.

“Kwa sasa tuna shehia 888 ila wasaidizi wa sheria tulionao ni 205 Zanzibar nzima, tuna shehia 141 hazina wasaidizi wa kisheria Unguja 106 na Pemba 35,” alisema.

Naibu Mkuu wa skuli sheria Zanzibar kitengo cha taaluma Msemo Mavare, aliwataka wasaidizi hao wa sheria kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo hayo, ili jamii iweze kunufaika juu ya uwepo wao.

Akitoa neno la shukurani Mwanasheria kutoka Idara ya Katiba na msaada wa kisheria Zanzibar Ali Haji, alisema mafunzo hayo ni muhimu sana, kwani jamii iliyokubwa inachangamoto nyingi juu ya masuala ya kisheria.



Mada kadhaa zitawasilishwa ikiwa ni pamoja na dhana ya wasaidizi wa sheria, katiba, sheria, sheria ya ushahidi, uashauri nasihi, sheria ya mtoto pamoja na miiko ya wasaidizi wa sheria.

MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch