Skip to main content

POLISI LATAJA SABABU KUMPA DHAMANA DAKTARI MTUHUMIWA UBAKAJI PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

JESHI la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, limekiri kumpa dhamana ya kipolisi daktari wa kituo cha afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, ambae ni anatuhumiwa kwa kumtorosha na kisha kumbaka mgonjwa wake, ambae ni mtoto.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Juma Sadi Khamis, wakati akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari, alisema sababu za kumpa dhamana, ni kufuatia mtoto huyo kutaja watu wawili tofauti.

Alisema, mtoto huyo alimtaja daktari huyo na mtu mwengine ambae kwa sasa, wanaendelea kumtafuta, hivyo wameona wampe dhama mtuhumiwa huyo hadi wote wawili watakapopatikana.

Alieleza kuwa, mtoto huyo alimtaja daktari kwa sababu alikwenda kupata huduma, ingawa yuko mtu mwengine aliyemfanyia kitendo hicho.

‘’Kwa sasa baada ya kuona mtoto huyo anafanya ubabaifu, daktari ambae tulikuwa tunamshikilia tumeshampa dhamana kwa muda,’’alifafanua Kamanda huyo.

Aidha Kamanda huyo, alieleza kuwa kwa sasa suala hilo linaendelea kupelelezwa kwa kina, na kisha Jeshi hilo litatoa taarifa nyingine rasmi.

‘’Ni kweli yule daktari ambae tulikuwa tunamshikilia, kwa sasa tumeshampa dhamana, maana muathirika aliwataja watuhumiwa wawili tofauti akiwemo daktari,’’alieleza.

Wakati hayo yakifanyika, Chama cha waandishi wa habari wanawake wanawake Tanzania -TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, kimeshtushwa na taarifa ya Jeshi la Polisi, kumpa dhamana mtuhumiwa huyo.

TAMWA kimesema, kama muathirika ameshamtaja mmoja kati ya watuhumiwa wawili, haingii akili, kumpa dhama mtuhumiwa nambari moja, kwa madai ya kumtafuta mwengine.

‘’Kama mtuhumiwa mmoja ameshapatikana, ni vyema sasa hatua nyingine zikaendelea, lakini unapompa dhamana ni kuivizisha kesi hiyo,’’alisema Mratibu wa TAMWA Fat-hiya Mussa Said.

Aidha Mratibu huyo alisema, kama kesi za udhalilishaji zimetajwa na sheria hazina dhamana, iwe kwa watuhumiwa wote, na sio kwa baadhi yao.



Kwa upande wake Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Kangagani wilaya ya Wete, Awena Salim Kombo, alisema ameshangaazwa na hatua ya Jeshi la Polisi, la kumpa dhama mtuhumiwa huyo.

Alisema, kila siku rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amekuwa akisisitiza, juu ya kutotoa dhamana kwa kesi hizo, ingawa utekelezaji haupo.

Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Wete Haroub Suleimna Hemed, alisema kwa familia anayotoka mtuhumiwa ‘daktari’ ni kubwa, na ndio maana, kesi hiyo inakwenda ndivyo sivyo.

Alisema, analishangaa Jeshi la Polisi mkoani humo, kumpa dhamana mtuhumiwa, huku akihoji sheria ipi waliyoitumia kumtoa daktari huyo, wakati watuhumiwa wengine huikosa haki hiyo.

‘’Watuhumiwa wengine wakitajwa tu na mtoto, basi huwa sheria inafanyakazi, lakini kwa huyu ambae ametajwa, sasa nashangaa kusikia yuko nje kwa dhamana,’’alieleza.

‘’Sasa sisi wanaharakati na tunaotetea haki za watoto tutashindwa kutekeleza wajibu wetu, maana tunagongana kiutendaji, wengine hawapewi dhamana na wengine wanapewa,’’alilalamika.

 Kuanzia Mei 1, mwaka huu, Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, lililazimika kumshikilia daktari wa kituo cha Afya Gombani Chake Chake, Is-haka Rashid Hadid, kwa tuhuma za kumbaka mgonjwa wake.

 

Kisha baina ya Mei 5 na Mei 6 mwaka huu, mtuhumiwa alipata dhamana, kwa madai ya mtoto huyo, kutaja watu wawili tofauti.

 

Ambapo Kamanda wa Polisi, alisema walilazimika kumpa dhamana daktari huyo, hadi hapo atakapopatikana mtuhumiwa mwengine, huku akisisitiza kwa waandishi habari hiyo, isiripotiwe.

 

Awali mtoto huyo aliyefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, Aprili 21 mwaka huu, alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu, na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu.

 

Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms), kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo, alizikosa hospitalini hapo.

 

"Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje daktari mwengine, kwa hiyo kesho (siku ya pili yake), atakuja kunichukua, ili ukanipe dawa nyingine", alisema mtoto.

 

Alieleza kuwa, kisha alimchukua hadi kijiji cha Kangagani wilaya ya Wete, na kumfungia kwa siku tano, na kabla ya kumbaka alimchunguza virusi vya Ukimwi.

 

Tukio linalofafana na hilo, liliwahi kutokea Novemba 21, mwaka 2019, hospitali ya Chake chake, baada ya daktari wa kitengo cha Atrasaund, kudaiwa kuomba rushwa ya ngono kwa mjamzito, kama sharti la kumpa huduma.

Aidha Disemba 18, mwaka mwaka 2019, TBC 1, iliripoti Afisa Muuguzi msaidizi wa kituo cha Afya Mamba mkoani Katavi kushikiliwa na Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kumbaka mjamzito, wakati alipokuwa akimsaidia kujifungua.

                   Mwisho

 

 

 

                     

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch