Skip to main content

CHAMA CHA MADEREVA KUSINI PEMBA CHANG'AKA NAULI MPYA YA DALADALA

 



NA HANIFA SALIM, PEMBA

CHAMA cha Wamiliki wa gari za abiria na mizigo Mkoa wa Kusini Pemba ‘PESTA’ kimesema hakitambui uwepo wa nauli mpya wa gari za abiria, katika Mkoa huo kama wanavyofanya baadhi ya madereva na makondakta.

Kimesema, kwa sasa madereva wanapaswa kuendelea kuwatoza abiria wao nauli kongwe, na sio mpya kama ambavyo wanafanya baadhi yao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, Katibu wa chama hicho Pemba, Hafidh Mbarka Salim amesema, hana taarifa ya kuwepo kwa nauli mpya, kwa gari za abiria.

Alieleza kuwa, anachofahamu ni kuwa tayari ‘PESTA’ imeshapeleka maombi ya mchanganuo wa nauli mpya, kufuatia wamiliki wa gari hizo kukumbwa na changamoto kadhaa, ikiwemo kupanda bei ya mafuta.

‘’Kwa sasa hakuna mmiliki wa gari wala dereva, aliyeruhusiwa kupandisha nauli mpya, na badala yake zitumike nauli kongwe hadi pale tangazo litakapotolewa,’’ alisema.

Hafidh alifafanua kuwa, katika muongozo huo wa maombi walioutuma serikalini, pamoja na upandaji wa bei ya mafuta lakini, kuna ongezeko la kodi pampoja na gharama za bima.

Hivyo amewataka madereva na wamiliki wa gari za abiria kuendelea kuvuta subira, na waendelee kutumia nauli kongwe wanapokua kazini.

Mapema Afisa Mdhamini wizara ya ujenzi, mawasiliano na uchukuzi Pemba, Ibrahim Saleh Juma, amekiri kupokea maombi ya ongezeko la nauli mpya kutoka ‘PESTA’.

Alieleza kuwa, tayari vikao vimeanza kukaliwa kwa ajili ya kujadili uwezekano wa kupandisha nauli mpya, kufuatia nishati ya mafuta, kodi na bima kupanda.

‘’Madereva na wamiliki wa gari za abiria, waendelee kuwa watulivu wakati wowote Serikali itatoa tamko, kuhusiana na nauli mpya,’’ alisema.

Katika siku za hivi karibuni, kufuatia kupanda kwa bei za mafuta wapo baadhi ya abiria wamekua wakilalamikia ongezeko la nauli, kabla ya serikali kutangaza bei mpya.

Mmoja kati ya abiria hao Khadija Omar Muhene wa Chake chake alisema, alitozwa shilingi 2,000 badala ya shilingi 1700 ya kutoka Chake chake hadi Mkoani.

Nae Suleiman Abdi alisema kuwa, alitozwa nauli ya shilingi 500 badala ya shilingi 400, kutoka Chake chake mjini hadi Machomane.

‘’Nauli ninayofahamu mimi kutoka mjini Chake chake hadi Wawi ni shilingi 400, lakini juzi tu nilipopanda gari ya Vitongoji nilipishwa shilingi 500 kwa madai ya nauli mpya,’’alisema.

Abiria Omar Abdull-kadir Ali alisema hata eneo la Limbani Wete sasa imepanda kwa shilingi 100 na kuwa shilingi 500 badala ya shilingi 400 ya asili.

Nao baadhi ya madereva wamesema kuwa wamelazimika kupandisha nauli kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta kwa zaidi ya miezi miwili.

Dereva Haji Abdalla Omar anaefanyakazi barabara ya Chake chake Mkoani, alisema ni zaidi ya miezi mitatu sasa mafuta na gharama nyingine za gari zimepanda pasi na nauli kupandishwa.

Nae Hassan Suod alisema, kama mafuta yamepanda bei kwa haraka, hakuna sababu kwa nauli kuchelewa kupandishwa.

Kwa mara ya mwisho serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilipandisha nauli mpya za gari za abiria wakati wa awamu ya saba baina ya mwaka 2017 na mwaka 2018.

                                         MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch