Skip to main content

HII HAPA HAKI ILIYOJIFICHA YA WATUMISHI WA UMMA WANAUME ZANZIBAR

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

AMA kweli, ukitaka kukificha kitu, kitie kwenye maandishi.

Wengi wamekuwa wakiyasema hayo, wakiwa na maana kuwa, ule utamaduni wa kusoma, sasa umeondoka.

Kumbe kwenye maandishi kama ya sheria, kanuni na sera zilizotungwa kwa ajili ya kundi fulani, hukosa kutekelezwa kwa waliotungiwa, kwa kutosoma.

Aliwahi kuwapa chagamoto wananchi Mkoani Pemba, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar Jaji Mashibe Ali Bakari, alipotakiwa kujibu juu ya sheria za Zanzibar kuwa lugha ya kigeni.

‘’Sheria za Zanzibar tunatungiwa sisi wananchi ambao lugha yetu mama ni Kiswahili, lakini zipo kwa lugha ya kugeni, hapa si mnataka kutufunga,’’alihoji Mohamed Abass sheha mstafu wa Kinyasini.

Jaji Mshibe akawambia kuwa, utamaduni wa kusoma hata kwa nyaraka zilizoandikwa kwa lugha ya kiswahili sasa haupo, na ukitaka kukificha kitu kitie kwenye nyaraka.

SHERIA NA KANUNI YA UTUMISHI WA UMMA 2014

Sasa ni miaka 19 imeshapita, tokea serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itunge Kanuni ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2014.

Kanuni hiyo yenye vifungu kadhaa, lakini vipo vifungu muhimu na adhimu, hasa kwa watumishi wa umma wanaume kuvijua, kwa kina.

Na hap unaweza kujifunza jambo kuwa, mwajiri maisha haoneshi haki za mwajiriwa, kama hakufanya juhudi za maksudi yeye mwenyewe kujisomea.

Inaweza wapo wanaume, ambao ni watumishi wa umma, wamekuwa wake zao wakijfungua na pengine kuhadithi ofisini kwake, lakini mwajiri akakaa kimnya.

LIKIZO LA MUME WA MKE ALIYEJIFUNGUA

Ili kuimarisha utawala bora na utawala wa sheria, sambamba na kujali umuhimu wa muume, mara mke wake anapojifungua, sheria na kanuni ya Utumishi wa umma, haikukaa kimya.

Maana imempa haki ya likizo muume huyo, mara tu mke wake anapojifungua, hata kama mke sio mtumishi wa umma.

Kwa mfano kifungu cha 62 (1) kinaeleza kuwa, mtumishi wa umma ambae mke wake amejifungua, ataruhusika kupewa likizo kwa muda wa siku tano (5) za kazi.

MASHARTI YA LIKIZO HILO KWA MUUME

Kanuni ikafafanua kuwa, likizo hilo litachukuliwa ndani ya siku saba, baada ya mtoto kuzaliwa, na halitoathiri lile likizo lake analolichuma kwa miezi 12.

Ingawa, likizo hilo la siku tano za kazi kwa mtumishi mwanamme, litatolewa kila baada ya miaka mitatu, ambapo hapa, kwa wale wasiokuwa na uzazi wa mpango hawatoangaliwa.

Maana, wapo wanandoa kila mwaka, mke hujifungua au kila baada ya mwaka mmoja na nusu, hivyo kinachozingatiwa sio uzazi tu, bali ni kila miaka mitatu.

Taarifa ya kustahili likizo hilo kwa muume huyo mtumishi wa umma, iwasilishwe kwa mkuu wake wa kazi, iambatanishwe na kitambulisho cha kuzaliwa cha mtoto.

JE MTUMISHI MWENYE MKE ZAIDI YA MMOJA?

Kanuni ya Utumishi wa Umma, wala haikuwasahau wanaume wenye mke zaidi mmoja, hata kama wake zake hao sio watumishi kama alivyo yeye.

Maana, kifungu cha 62 (2) kimebainisha kuwa, mwenye mke zaidi ya mmoja, atastahiki kupata likizo kwa kila mke wake atakapojifungua.

Hata hivyo, endapo atakejifungua kila mwaka ni mke huyo huyo mmoja, atastahiki likizo hilo kila baada ya miaka mitatu, na sio kila anapojifungua mke wake.

LIKIZO LA UZAZI KWA MKE MTUMISHI WA UMMA

Kanuni hii ya utumishi wa Umma ya mwaka 2014, imetoa haki na masharti kwa mzazi wa kike, ambae nae amejifungua na hilo limeanishwa kifungu cha 61 (1).

‘’Mtumishi wa umma anapojifungua, anastahiki likizo ya miezi mitatu (siku 90 za kazi) kwa siku za kalenda,’’inaeleza sehemu ya Kanuni hiyo.

Likizo hiyo ya uzazi ya miezi mitatu, itatolewa mara moja, kwa kila baada ya maika miwili na miezi tisa, kwa mtumishi mwanamke.

Kama ilivyo kwa mtumishi mwanamme ambae mke wake amejifungua, nae pia kwa mtumishi wa umma mwanamke, likizo lake hilo, halitoathiri lile likizo lake la kawaida.

Kanuni ikafafanua kuwa, pindi mtumishi huyo wa kike atajifungua kabla ya kutimiza muda uliotajwa (miaka miwili na miezi tisa), atastahiki kupata mapunziko ya wiki sita tu.

Lakuzingatia hapa, taarifa za kujifungua kwake, inaweza kutolewa na yeye mwenyewe, au mtu wake wa karibu mfano muume na ziende kwa Katibu mkuu au mkuu wa tasisi.



Kanuni ikaenda mbali zaidi, na kueleza kuwa ikiwa mtumishi huyo, amejifungua mapacha, kipindi cha likizo kitaongezwa mpaka kufikia siku 100 za kazi.

Kubwa zaidi, ikiwa mimba hiyo imeharibika, au kufa kwa mtoto, mtumishi huyo atapewa likizo ya wiki sita, tokea tarehe ya kujifungua au kuharibika kwa ujauzito huo.

Kanuni ikisema kuwa, iwapo likizo lake ilikatishwa kwa sababu ya kufa kwa mtoto wake mchanga, akipata ujauzito kabla ya kutimiza miaka miwili na miezi tisa, kuanzia tarehe ya kujifungua au kuharibika mimba.

Basi Kanuni hiyo ya Utumishi wa umma, imeweka wazi kuwa, mtumishi huyo atastahiki likizo ya miezi mitatu kwa siku za kazi.

JE HAKI YA MTOTO KUNYONYA IKOJE KWA MAMA MTUMISHI WA UMMA?

Mtumishi huyo atapewa saa moja kila siku, kwa ajili ya kunyonyesha mtoto wake kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo.

Lakini Kanuni imemtaka mtumishi huyo kuchagua, aidha kuitumia nafasi hiyo asubuhi kabla ya kuja kazini au mchana saa moja, kabla ya muda wa kawaida ya kuondoka kazini, yaani saa 9:30.

JE WATUMISHI WA UMMA WANAUME WANAYAJUA HAYA?

Omar Hassan Khalid wa wizara ya elimu, anasema mke wake ameshajifungua watoto saba akiwa kazini, lakini hakumbuki hata siku moja, kupewa mapumziko hayo.

Mohamed Jafu Said mstaafu wizara ya Mawasiliano, anasema licha ya kuwahi kuwa na wake wanne, wakati akiwa mtumishi wa umma, ingawa haki hiyo hakuwahi kuipata.

‘’Inawezekana mimi kama mtumishi wa kawaida hili jambo sikuwa nalijua, lakini je ofisa utumishi wangu kama anajua, mbona sikuwahi kuaelezwa,’’anahoji.

Hassan Ali Hassan ambe ni mfanyakazi wizara ya Afya anasema, aliwahi kupewa mwaka 2016, baada ya kusikia kwenye redio, juu ya uwepo wa haki hiyo, na kuidai.

‘’Kuanzia hapo, niliwahi kuomba tena mwaka 2020, na wakati huo wake zangu wawili walijifungua kwa wakati mmoja, lakini niliambiwa nisubiri, na sikupewa tena,’’anasema.

Ingaa Hidaya Hassnuu Omar na Asha Mbarouk Omra watumishi wa wizara ya Elimu, wanasema haki ya mapumziko baada ya kujifungua huipata,,



WIZARA YA KATIBA, SHERIA, UTUMSHI NA UTAWALA BORA

Afisa sheria wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Pemba Bakari Omar Ali, anasema wamekuwa wakieleza maafisa utumishi, ili wawelimisha watumishi wao.

‘’Wakati mwengine tasisi za umma wanatuita na kuwasomesha watumishi wao, juu ya sheria na kanuni za utumishi, na hili suala la mapunziko ya siku tano za kazi tunaligusa,’’anasema.

Anaona wapo baadhi ya watumishi wanaume wamekuwa wakizitumia siku hizo, ingawa wengine ijapokuwa wanajua lakini hawaziombi.

NINI KIFANYIKE?

Mtumishi Issa Haji Khamis na mwenzake Khaija Hija Othman, wamependekezwa elimu zaidi hasa ya kuifahamu kanuni ya utumishi wa umma, izidi kutolewa.

Afisa Mdhamini wizara ya Katiba na sheria Pemba Halima Ali Khamis, amesema lazima watumishi wajiongezea kwa kuzisoma sheria wanazozifanyia kazi.

Aliyekuwa ofisa Utumishi wizara ya Habari Mohamed Juma, anasema ni jukumu la mtumishi, kujua kanuni zinazogusa haki na wajibu wake.

                                   Mwisho

 

      

   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch