Skip to main content

Posts

KESI YA DAKTARI PEMBA KUNGURUMA TENA LEO MAHAKAMANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MAHAKAMA ya Mkoa Wete, leo Juni 15, mwaka huu inatarajia kupokea mashahidi na kuwasikiliza kwenye shauri la daktari Is-haka Rashid Hadid, wa kituo cha afya Gombani, anayedaiwa kumbaka mara tatu, mtoto wa miaka 16. Shauri hilo linatarajiwa kuendelea leo, baada wiki mbili zilizopita (Juni 1, mwaka huu) kughairishwa, kufuatia upande wa mashataka, kutopokea mashahidi wa kesi hiyo. Awali daktari huyo, alipelekwa rumade kauanzia Mei 18, mwaka huu na kutakiwa kurudi tena mahakamani hapo Juni 1, ili kuwasikiliza mashahidi. Ingawa upande wa mashataka siku hiyo, haukupokea mashahidi, na mtuhumiwa huyo kulazimika kurejeshwa tena rumande, kama sehemu ya kuupa nafasi upande wa mashtaka kuwasilisha mashahidi. Awali, Juni 1, mwaka huu mara baada ya mtuhumiwa huyo kuwasili mahakamani hapo akitokea rumande, chini ya hakimu wa mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji, Mwendesha mashataka Juma Mussa, aliiomba shauri hilo kughgirishwa. Alidai kuwa siku hi...

ALIYEMLAWITI MTOTO WA MIAKA 15, AFUNGWA MIAKA 20 PEMBA

NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::-   MAHAKAMA ya Mkoa Wete imemuhukumu kijana Ali Sharif Ali miaka 19 mkaazi wa Pandani, kwenda kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 20 na kulipa fidia ya shilingi 100,000 baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto mwenye miaka 15.   Akisoma hukumu hiyo hakimu wa mahakama ya Mkoa B Wete Ali Abrahman Ali amesema, mahakama imemtia hatiani kijana huyo baada ya kupatikana na kosa hilo.   Alisema kuwa, mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka, kwani wamethibitisha shitaka pasi na kuacha chembe ya shaka na ndio maana mahakama imemuamuru kwenda kutumikia chuo cha mafunzo miaka 20 pamoja na kulipa fidia ya shilingi 100,000.   “Tumemtia hatiani mshitakiwa huyo chini ya kifungu 220 cha Sheria ya Mwenendo wa Jinai nambari 7 ya mwaka 2018 sambamba na kifungu cha 115 (1) cha Sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, Sheria za Zanzibar”, alisema hakimu huyo.   Mapema upande wa mashitaka ukiongozw...

ZAECA PEMBA: YASEMA JAMBO KUHUSU ASKARI WA JKU WANAEMSHIKILIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-                            MAMLAKA ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar 'ZAECA' Pemba, imesema iko katika hatua za mwisho za kukamilisha uchunguuzi, kabla ya kumfikisha mahakamani Askari wa Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar 'JKU' anayetuhumiwa kupokea rushwa, kwa hadaa ya kuwaajiri vijana. Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa ‘ZAECA’ mkoa wa kaskazini Pemba Nassor Hassan Nassir, alisema kwa sasa watendaji wake wako katika hatua za kumalizia uchunguuzi huo, kabla ya hatua nyingine. Alisema kuwa, lazima wajiridhishe kila eneo kwenye uchunguuzi wao, maana ‘ZAEC’A haikuanzishwa kwa lengo la kumuonea mtu, bali ni kufuata taratibu za sheria kama zilivyo. Alieleza kuwa, baada ya kumshikilia mtu yeyote, hawawezi kumfikisha moja kwa moja mhakamani, lazima kuna hatua za kiufundi na kisheria wazip...

‘KISIWA KHAMIS’ KIVUTIO KIPYA CHA UTALII PEMBA

NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-   Ni takribani dakika 25, kutoka katika ufukwe kwa bandari ya Tumbe, hadi kufikia kwenye kisiwa cha Ndege ‘Khamis’ kilichopo katika eneo la Tumbe ndani ya bahari ya Hindi.   Ilikuwa majira ya saa 3:00 asubuhi, boti iliyobeba maafisa wa wizara ya utalii na mambo ya kale, ikiwasili katika kisiwa Ndege kinachojulikana kwa jina la (kisiwa khamis).   Hali ya hewa ilikuwa ni ya mawingu mawingu, kutokana na mvua kubwa iliyonyesha usiku mzima wa kuamkia siku hiyo, boti hiyo aina ya mashua, ilibeba takribani ya watu 30.   Katika msafara huo, jemedari wa Wilaya hiyo Mgeni Khatib Yahya amekiongozana na mwenye dhamana ya Wizara ya utalii na Mambo ya Kale Pemba Zuhura Mgeni Othman, na maafisa wengine.   Safari hiyo, haikubeba maafisa hao, tu bali ilikua na watu ambao wanaipasha jamii habari, kutoka vyombo mbali mbali vya habari.   Ziara hiyo, iliyofanywa na Wizara ya Utalii, ilikua na lengo la kutembelea kisiwa hicho, ...

MATTAR AIPA TANO KAMATI MAANDALIZI SIKU YA MTOTO AFRIKA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amesema ameridhishwa na matayarisho ya awali, yaliyofanywa na wajumbe wa Kamati maalum ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, kisiwani humo. Alisema, kamati hiyo imeibua jambo kubwa la kutaka kufanya maadhimisho hayo, na kujipanga kwa kufanya shughuli mbali mbali, kabla na wakati wa kilele chenyewe ambacho ni Juni 16, mwaka huu. Alisema ameridhishwa na mpango huo wa maadhimisho na kuahidi kushirikiana nao, hadi kukamilika kwake siku ya kilele hicho kinachotarajiwa kufanyika uwanja wa Gombani. Mkuu huyo wa mkoa aliyasema hayo Juni 11, 2022 ofisini kwake Chake chake, wakati akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo, waliofika ofisini kwake, kuwasilisha mpango pendekezwa wa kilele hicho. Alisema, suala la kuwashirikisha watoto ambao ni wanafunzi na kuwaandalia michezo mbali mbali kama ushindani kwenye elimu, ni jambo linalofaa kuungwa mkono. ‘’Kwanza niwapongeze wajumbe wa kamati hii, kwa uamuzi...

RC SALAMA ATOA NENO KUHUSU WATOTO NI BAADA YA MATEMBEZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKUU wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, leo Juni 11, 2022 ameungana na vilabu vitatu vya mazoezi kikiwemo cha Gombani Fitness Club, na wadau wengine wa haki za mtoto wakiwemo TAMWA, kwenye matembezi maalum ya kuelekea kilele cha siku ya mtoto wa Afrika, hapo Juni 16, mwaka huu. Mkuu huyo wa mkoa, akiongozana na vilabu hivyo vya mazoezi, walianza matembezi yao Polisi Madungu na kumalizia uwanja wa michezo Gombani wilaya ya Chake chake. Baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, pia yaliohudhuriwa na wakuu wa wilaya za Chake chake na Mkoani, Mkuu huyo wa mkoa, aliwataka wanamazoezi hao, kuwa wazazi wema kwa watoto wao. Alisema, wapo baadhi ya wazazi wamekuwa wakijitoa mishipa ya fahamu, kwa kuwabaka watoto wao wa kuwazaa, jambo linalosikitisha. ‘’Kwanza nianze na nyinyi, muwe baba na mama wema kwa watoto wenu, maana sasa hali imekuwa ikitisha kwa majanga wanayofanyiwa watoto wetu,’’alieleza. Hata hivyo, amesema wakati ...

WALIOPO KIZUIZINI WANA HAKI YA KUPATA MSAADA WA KISHERIA?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- ‘’WATU wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria,’’ ndivyo inavyofafanua Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Maelekezo hayo utayafuma mara ukiifungua Katiba hiyo, kwenye kifungu chake cha 12 (1), ingwa suala la kupata msaada wa kisheria, haliguswi moja moja, lakini msingi wa hilo upo. Ndio maana hapo sasa, kwa kuzingia msingi huo wa sheria mama yaani Katiba (ground norm),  tunaweza kusema kwa kinywa kipana kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unamgusa kila mmoja. Nikuulize, msingi wa usawa mbele ya sheria kwenye kifungu hicho cha 12, kweli unaweza kuwa na maana, iwapo wenzetu walioko kizuizini, ambao pia uhuru wao umedhibitiwa wasiwe na haki ya kupata msaada wa kisheria? Kwa hakika, tena kwa jicho hata lisilokuwa na uwana sheria utagundua kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unawahusu, hata walioko kizuizini. AZIMIO LA HAKI ZA BINADAMU Haki ya mtu kuwa huru, n...