Skip to main content

MATTAR AIPA TANO KAMATI MAANDALIZI SIKU YA MTOTO AFRIKA PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-


MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amesema ameridhishwa na matayarisho ya awali, yaliyofanywa na wajumbe wa Kamati maalum ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, kisiwani humo.

Alisema, kamati hiyo imeibua jambo kubwa la kutaka kufanya maadhimisho hayo, na kujipanga kwa kufanya shughuli mbali mbali, kabla na wakati wa kilele chenyewe ambacho ni Juni 16, mwaka huu.

Alisema ameridhishwa na mpango huo wa maadhimisho na kuahidi kushirikiana nao, hadi kukamilika kwake siku ya kilele hicho kinachotarajiwa kufanyika uwanja wa Gombani.

Mkuu huyo wa mkoa aliyasema hayo Juni 11, 2022 ofisini kwake Chake chake, wakati akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo, waliofika ofisini kwake, kuwasilisha mpango pendekezwa wa kilele hicho.

Alisema, suala la kuwashirikisha watoto ambao ni wanafunzi na kuwaandalia michezo mbali mbali kama ushindani kwenye elimu, ni jambo linalofaa kuungwa mkono.

‘’Kwanza niwapongeze wajumbe wa kamati hii, kwa uamuzi wao wa kutaka kushirikiana na kuiunga mkono serikali yetu, katika kutetea na kulinda haki za mtoto,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa mkoa, aliitaka kamati hiyo, wawasiliana nae kila wakati, na ikiwa kuna jambo limekwa, kuona njia gani ya kulitatua.

‘’Kwenye usafiri, majukwaa na hata kikundi cha brass band na gharama nyingine, nitaangalia uwezekano wa kushirikiana na wenzangu kuzitekeleza,’’alifafanua.

                                                                                                                      
                                                

                                                                               


Mwenyekiti wa muda wa kamati hiyo Nassor Bilali Ali, alimpongeza mkuu huyo wa mkoa, kwa uamuzi wake, wa kuzibeba gharama za utekelezaji wa sherehe hizo.

‘’Kwa niaba ya wajumbe wa kamati, tunakupongeza kwa hatua zako na kuona sherehe hii ya kutetea haki za mtoto zinafanyika kwa ufanisi,’’alieleza.

Mwenyekiti mwenza wa kamati hiyo, Mwanaisha Ali Massoud, alisema mfano wa viongozi kama Mkuu wa mkoa, ndio ambao wanaweza kufanikisha mambo kadhaa.

‘’Kwa hakika ilionekana dhahiri tumeshakwa kuiadhimisha siku hii, lakini kutokana na umahiri, utayari na kuumwa kwake na haki za watoto, ndio maana ameamua kusaidia eneo kubwa,’’alieleza.

Wajumbe wa kamati hiyo akiwemo Siti Habib Mohamed kutoka Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, alisema watoto lazima waandaliwe zawadi maalum.

‘’Kwa vile tumeamua kuweka michezo kama ya kuokota mbatata, kuvuta kamba, mbio za magunia, masuali ya papo kwa papo, ni vyema washindi wakatunzwa,’’alipendekeza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba TUJIPE, Tatu Abdalla Msellem, alisema moja ya changamoto zinawazowakabili watoto, ni janga la udhalilishaji.

‘’Hivyo kama tumepanga tutakua na masuali ya papo kwa papo, basi hata kuwauliza nini maana ya udhalilishaji, hatua gani utazichukua ukimkuta aliyedhalilisha na mengine yanayofanana na hayo,’’alishauri.

Awali Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, aliitaka kamati hiyo, kuyafanya maadhimisho hayo kuwa ya kitaifa kisiwani Pemba badala ya kuadhimishwa kiwilaya.

Kamati hiyo inaundwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria Pemba ‘JUWASPE, Jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba TUJIPE, na Zanzibar Social Workers Association ZASWA.

                           MWISHO   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch