Skip to main content

‘KISIWA KHAMIS’ KIVUTIO KIPYA CHA UTALII PEMBA




NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-

 

Ni takribani dakika 25, kutoka katika ufukwe kwa bandari ya Tumbe, hadi kufikia kwenye kisiwa cha Ndege ‘Khamis’ kilichopo katika eneo la Tumbe ndani ya bahari ya Hindi.

 

Ilikuwa majira ya saa 3:00 asubuhi, boti iliyobeba maafisa wa wizara ya utalii na mambo ya kale, ikiwasili katika kisiwa Ndege kinachojulikana kwa jina la (kisiwa khamis).

 

Hali ya hewa ilikuwa ni ya mawingu mawingu, kutokana na mvua kubwa iliyonyesha usiku mzima wa kuamkia siku hiyo, boti hiyo aina ya mashua, ilibeba takribani ya watu 30.

 

Katika msafara huo, jemedari wa Wilaya hiyo Mgeni Khatib Yahya amekiongozana na mwenye dhamana ya Wizara ya utalii na Mambo ya Kale Pemba Zuhura Mgeni Othman, na maafisa wengine.

 

Safari hiyo, haikubeba maafisa hao, tu bali ilikua na watu ambao wanaipasha jamii habari, kutoka vyombo mbali mbali vya habari.

 

Ziara hiyo, iliyofanywa na Wizara ya Utalii, ilikua na lengo la kutembelea kisiwa hicho, kukitangaza rasmi kiutalii, kikiwa ni kivutio kipya.

 

Kwani, kwa miaka zaidi ya miaka 70 iliyopita, hakikuwemo kwenye orodha ya vivutio, ambavyo vimetambuliwa Kisiwani Pemba.

 

Kilipo kisiwa ‘Khamis’ ni takribani ya kilomita 3, hadi ilipo bandari ya Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

 

Kisiwa hicho chenye urefu wa wastani wa viwanja viwili vya mpira wa miguu ‘mita 230’ kikiwa na upana wa kiwanja kimoja na nusu cha mpira wa miguu ‘mita 160’.

 

Miti mirefu mchanganyiko, iliyotawala ubichi iliyojengeka kwa vichaka na hali ya hewa mwanana, huku ukikaribishwa na miito ya ndege aina 12, ndio mandhari inayowavutia wageni na wenyeji.

 

AINA YA NDEGE WALIOPO KISIWA KHAMIS

 Kisiwa Khamis, umaarufu kisiwa ndege, kimechota aina 12 ya ndege 12 wakiwemo Yangeyange, Makoho, Vijafara, Membe, Chozi, Mwewe, Jimbi msitu, Visengenya na Chozi jabiri.

 


Aina hii ya ndege 12 waliopo katika kisiwa hicho, wala sio rahisi hata kidogo kuwakuta ndani eneo jengine pasi na kisiwa hicho.

 

IDARA YA MAKUMBUSHO NA MAMBO YA KALE PEMBA

 

Khamis Ali Juma, ambae ndie Mratibu wa Idara hiyo, anakiri kuwa, upya wa ugunduzi wa kisiwa hicho, bado ni mapema kuelezea sababu ya kuitwa kisiwa ‘Khamis’.

 

Ijapo kuwa wakaazi wa eneo la Tumbe na hasa wavuvi walikipachika jina la ‘Kisiwa ndege’ kutokana na kuzagaa kwa idadi kubwa ya ndege.

 

Mratibu Khamis anasema, ugunduzi wa kisiwa hicho ni kuelekea kuengeza idadi ya vivutio vya utalii Kisiwani Pemba.

 

‘’Ni mwaka huu wa 2022 tu, ndio tumekigundua kisiwa hichi, na rasmi sasa tumeshakiingiza kama ni kivutio kipya cha kiutalii Kisiwa Pemba,’’ anasema.

 

Anaainisha kuwa, kuwa juhudi zikiendelea za ugunduzi wa vivutio vya utalii kama ‘kisiwa ndege’ ni ile dhana ya kuongeza idadi ya utalii Pemba, haitokua mbadala.

 

Historia ya Pemba, imeanza kukatika kutoka kisiwa cha Bara zaidi ya miaka milioni 5 iliyopita, ilijigawa na kupatikana visiwa vidogo vidogo ikiwemo cha Pemba.

 


Kisiwa cha Pemba nacho, kimeanza kukatika na kutengeneza visiwa vidogo vidogo kama vile Mkumbuu.

Ingawa kuna nguvu iliyotumika ya kujengwa daraja la kuungaisha mto uliopita, vyenginevyo eneo hilo lingekua tayari ni kisiwa.

 

“Licha ya daraja na mto uliopo, lakini kutokana na mazingira yaliyopo baada ya miaka kadhaa, Mkumbuu wilaya ya Chake chake, itakuwa kisiwa ambacho kitajitegemea,’’anasema.

 

Hili Mratibu huyo anasema, kwani sasa hivi tayari kuna mito miwili inayoingiliana baina ya upande mmoja na mwengine.

 

ASILI YA KISIWA NDEGE

Ni ndege wa aina tofauti, ambao wanaingia na kutoka sehemu mbali mbali za dunia.

 

Eneo moja ni kama vile Ulaya na kwenda kuishi kwa muda ndani ya kisiwa hicho na kuondoka.

 

“Kuna ndege wa pwani, wao wanatumia bahari kwa kutafuta chakula chao, kuna ndege aina ya Yangeyange, Makoho, Kunguru, Vijafara, Membe pamoja na Njiwa ambao wanakipamba kisiwa hichi”, anasema.

 

Ndege aina ya Membe ni ndege ambao wanalia kuashiria maji kutoka na kuingia, na mara nyingi wavuvi wanawatumia kujua maji yanapoingia au kutoka.

 

WIZARA YA UTALII NA MAMBO YA KALE

 Mwenye dhamana ya ofisi hiyo Pemba, Zuhura Mgeni Othamn anasema, ndege waliopo ndani ya kisiwa hicho pekee ni utalii wa kutosha, achia mbali kisiwa hicho.

 

‘’Ndege ni sehemu ya utalii, wapo wageni ambao ni wanafanya utafiti, ambao hupenda kuona ndege au kuwinja, ndipo wizara ilipoamua kutembelea, ili kukitangaza kisiwa hicho,’’ anasema.

 


Anasema kuwa, ndege waliopo katika kisiwa hicho hawapatikani kwengine popote duniani, ambapo hilo ni jambo la kujivunia.

 

Licha ya rasilimali ya ndege iliyopo kwenye kisiwa hicho, lakini pia ardhi yake ni ya mwamba wa mawe na udongo wa aina ya tifu tifu.

 

Kwa upande wa wizara, imejipanga vyema kwa kukiimarisha  kisiwa hicho, ili kiweze kuleta faida kubwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

 

MKUU WA WILAYA

Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, aliwataka wananchi kukitunza kisiwa hicho, kwa kurejesha msitu ambao ulikuwepo awali.

 

Anasema, kisiwa hicho ni moja kati ya vivutio muhimu cha utalii kwa Wilaya hiyo, hivyo aliwataka wananchi ambao wanafanya shughuli za kilimo, kulima kilimo kinachoendana na mabadiliko ya tabia nchi.

Anaeleza, kisiwa hicho endapo jamii itashindwa kukitunza, kitaathirika na ndege ambao wanaishi humo, wataondoka na kupoteza historia.

 


‘’Mandhari, uzuri na utamu wa kisiwa ndege ni kuwepo kwa ndege aina 12, kama ilivyo sasa, endapo shughuli za binaadamu zitawakimbiza ni kupunguza utamu wa historia,’’ anaeleza.

 

Binafis alifarajika kukitembelea kisiwa hicho, ambacho kina mandhari nzuri na haiba ya kuvutia, na kina mazalio ya ndege tofauti.

 

Mkuu huyo, aliwataka wananchi wa Pemba kujenga utamaduni wa kutembelea maeneo ya kihistoria, ili kujifunza na kujionea utalii ambao upo ndani ya kisiwa chao.

 

AFISA MAZINGIRA WILAYA YA MICHEWENI

 

Afisa Mazingira Wilaya ya Micheweni Salum Mjaka Ali anasema, kisiwa hicho kwa sasa, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi kimeathiriwa na shughuli za kibinaadamu.

 


"Hichi kisiwa kama tutaendelea kukitunza kitaendelea kubakia kutumika kwa shughuli za kiutalii, tutakapofanya uharibifu tunajiharibia maisha yetu,’’ anaeleza.

 

Aliwashauri wananchi ambao wanafanya shughuli za kilimo ndani ya kisiwa hicho, kufanya kilimo endelevu ambacho kitaimarisha hali ya kisiwa hicho kwa kupanda miti itakayodumu kwa muda mrefu.

 

Kisiwa Khamis (kisiwa ndege) kipo upande wa Mashariki wa bandari ya Tumbe, kikiwa ni moja ya visiwa vidogo vidogo vinavyomegeka siku hadi siku kutokana na mabadiliko ya tabia nchi kwa zaidi ya miaka milioni 5 iliyopita.

MWELEKEO WA UTEKELEZAJI BATIKU KUU YA WIZARA 2022/2023

Akiwasilisha hutuba ya bajeti ya wizara ya Utalii na Mambo ya Kale waziri wa wizara hiyo Simai Mohamed Said, alisema kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023, wizara imepangiwa jumla ya shilingi zaidi ya shilingi bilioni 17.289.

Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 7.500 zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Kuimarisha Maeneo ya Kihistoria mfano wa kisiwa Khamis (kisiwa ndege). 

 

                                            MWISHO. 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch