Skip to main content

WALIOPO KIZUIZINI WANA HAKI YA KUPATA MSAADA WA KISHERIA?

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-

‘’WATU wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria,’’ ndivyo inavyofafanua Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Maelekezo hayo utayafuma mara ukiifungua Katiba hiyo, kwenye kifungu chake cha 12 (1), ingwa suala la kupata msaada wa kisheria, haliguswi moja moja, lakini msingi wa hilo upo.

Ndio maana hapo sasa, kwa kuzingia msingi huo wa sheria mama yaani Katiba (ground norm),  tunaweza kusema kwa kinywa kipana kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unamgusa kila mmoja.

Nikuulize, msingi wa usawa mbele ya sheria kwenye kifungu hicho cha 12, kweli unaweza kuwa na maana, iwapo wenzetu walioko kizuizini, ambao pia uhuru wao umedhibitiwa wasiwe na haki ya kupata msaada wa kisheria?

Kwa hakika, tena kwa jicho hata lisilokuwa na uwana sheria utagundua kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unawahusu, hata walioko kizuizini.

AZIMIO LA HAKI ZA BINADAMU

Haki ya mtu kuwa huru, na kutokamatwa au kuwekwa kizuizini kumbe ni kinyume na sheria, na miongozo kadhaa iwe ya kimataifa, kikanda, Afrika na hata kwetu Tanzania, haikubali.

Huko ni kumnyima mtu huyo haki yake ya kibinadamu, ambapo imewekwa kwenye Azimio la Dunia la Haki za Binadamu, lile la mwaka 1948.

Ieleweke kuwa, utu wa mwanadamu, unahitajika kuthaminiwa kama haki muhimu, ya mwanadamu yeyote ambayo huipata, kwa kule kuwa yeye ni mwanadamu tu.

TANZANIA

Kwa mfano taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar, zinatambua na zinaendelea kutambua haki hii ya mtu kwenda atakapo, pasi na kuvunja sheria.

Lakini kwa hili aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar Jaji Mshibe Ali Bakari, alikuwa akitoa ufafanuzi juu ya haki, akisema kukamatwa ndani ya kambi ya Jeshi, hakuna utetezi.



‘’Haiwezekani ukaingie kwenye kambi ya Jeshi la wananchi wa Tanzania, au Chuo cha mafunzo, kinga iwe una haki ya kwenda, utakapo, hapo sio sahihi,’’anafafanua.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari Pemba PPC, Said Mohamed Ali, amekuwa akisema hakuna uhuru usio na mipaka.

‘’Kila mmoja anakumbuka alipokuwa na miezi sita, mwaka mmoja hadi miwili, akiweza kulala na wazazi wake, ingawa kila umri ukiongezeka, alikuwa anatengwa,’’anasema.

KATIBA YA ZANZIBAR YA MWAKA 1984

Kwa bahati nzuri mno, Katiba hiyo inatambua kuwa mtu anapowekwa kuzuizini kwa taratibu za kisheria, haitohesabiwa kuwa ni ukiukwaji wa katiba.


Inatambua kuwa, kila mtu yupo huru na hivyo kimsingi analindwa dhidi ya kukamatwa, kufungwa, kuwekwa kizuizini, kuhamishwa, kunyang’anywa uhuru wake.

MSINGI WA KUPATA MSAADA WA KISHERIA UNAPOKUWA KIZUIZINI

Haki hii imewekewa msingi na nyaraka za kisheria kabisa 'legal documents', ikiwemo Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Sheria ya Msaada wa Kisheria nambari 13 ya mwaka 2018 na hata Sera ya sheria hiyo ya mwaka 2017.

SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA NAMBARI 13 YA MWAKA 2018

Zanzibar imekuwa ikihakikisha, suala la utawala bora linaimarika, ambapo kabla ya ujio wa sera na sheria hii, suala la upatikanaji wa msaada wa kisheria, iwe kwa walio huru ama kizuizini, halikutambulika rasmi.

Ndio maana, Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, akasema sasa hakuna sababu kwa wananchi, kuonewa kwa kutokujua sheria.

‘’Idara hii imeanzishwa kwa ajili ya wananchi wanyonge, wasiojiweze na hata wenzetu wenye mahitaji maalum, ili kupata msaada, ushauri na elimu ya sheria bila ya malipo,’’anasema.



Lakini hili sasa, sheria hiyo imekuja kama vile ni mwarubaini wa kuimarisha utawala bora na utawala wa sheria Zanzibar, kwa kule kuweka wazi kwa makundi mbali mbali.

Mfano sheria hiyo, imeweka wazi haki ya msaada wa kisheria kwa watoto na watu wengine, waliopo vizuizini katika vyuo vya mafunzo, Polisi au nyumba nyingine za mahabusu ya watoto.

Kwa mfano vifungu vya 41 (1(i), 34 na cha 35 vya sheria hiyo, vimeweka msingi wa upatikanaji wa haki hiyo, kwa mtu aliyepo kizuizini, kwa kutambua mahitaji yake.

Zuri la uwepo wa sheria hiyo, imekwenda usoni, kwa kule kuweza kushurutisha hata Chuo cha Mafunzo, Jeshi la Polisi au nyumba ya mahabusu ya watoto, kweka mazingira ya upatikanaji wa msaada huo.

Azma hii, imewalazimisha wakuu ya maeneo hayo ya uwekaji watuhumiwa kizuizini, mara wawaekapo kuwapa taarifa kwa upana, juu ya haki yao ya upatikanaji wa msaada wa kisheria.

Hivi karibuni Mkurugenzi wa Jumuiya wa wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Nassor Bilali Ali, aliwaambia wananchi wa shehia ya Michungwani, kuwatumia wasadizi wa sheria.

‘’Wapo ambao wameshanufaika na msaada wa kisheria na wengine walikuwa kizuizini, kwa zaidi ya saa 24 wanazopaswa kushikiliwa, lakini kisha walipata dhamana,’’anaeleza.

Humud Is-haka Ngwali wa Pujini, ni mmoja wa wanufaika wa msaada wa kisheria, wakati alipokuwa na tuhuma za kuvamia shamba la mtu mwaka 2020.

‘’Pengine kama sio uwepo wa sheria hiyo, mimi ningeshikiliwa Polisi, mpaka upelelezi ukakamilika, lakini zilipopita saa 24, niliombewa na msaidizi wa sheria,’’anakumbuka.

JE MAWAKILI WA KUJITEGEMEA WANA NAFASI GANI?

 Ilishazoeleka kuwa, kazi hii wenyewe ni wale wasaidizi wa sheria, ambao wapo kila Jimbo la uchaguzi la Zanzibar, kwa wastani kati ya wawili hadi wanne.

Lakini, kumbe hata Mawakili wa kujitegemea na hasa kupitia Jumuiya yao ya Mawakili iliyosajiliwa Zanzibar, wanayo haki, na fursa ya kutoa msaada wa kisheria kwa waliopo vuzuizini.

Maana, yapo mashauri ‘kesi’ ambazo ni nzito na pengine wasaidizi wa sheria, wanaweza kuwa wepesi, lakini uwepo wa mawakili hao, huweza kuwasaidia wananchi waliopo vuzuizini.

JARIDA LA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA

Ingawa kwa mujibu wa jarida nambari 003 na Julai hadi Disemba mwaka 2021, linalotolewa na Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar, limetaja uwepo wa Wakili mmoja.

‘’Mpaka sasa ni wakili mmoja pekee, aliyejitokeza kusajiliwa kutoa msaada wa kisheria, na hivyo ni dhahiri kuwa, waliopo kuzuizini hawatonufaika na huduma hiyo,’’linafafanua jarida hilo.

Kwenye andiko lake hilo ukurasa wa 11, linatoa rai kwa mawakili wa kujitegemea, pamoja na jumuiya yao kuhamasisha wengine zaidi kujitokeza kuwasadia walioko kizuizini.

WANANCHI NA WADAU WA HAKI ZA BINADAMU

Khadija Hassan Omar wa Wawi mwenye ulamavu wa viungo, anasema, haki ya kupatiwa msaada wa kisheria kwa waliopo vizuizini, lipewe kipaumbele.

Khamis Issa Haroun wa Wambaa Mkoani, anasema kama sheria inatambua kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria, suala la walioko chini ya ulinzi kupata msaada wa kisheria, litambuliwe.

Mtoto Mayasa Himid Othman maiaka 16 wa Mchanga mdogo, anasema suala la upatikanaji wa msaada wa kisheria, sasa linatakiwa kuwa na sheria yake.



‘’Wapo watoto wenzetu wamekuwa wakiwekwa kizuizini kinyume na sheria, sasa lazima mawakili na hata wasaidizi wa sheria, wapewe meno ya kutoa msaada huo,’’anasema.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, anasema Pemba hakuna chuo cha Mafunzo kwa ajili ya watoto, hivyo lazima msaada wa kisheria, wanapokuwa kizuizini liangaliwe.

Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar, Khadija Shamte Mzee, anasema hawatosita kuzifanyia marekebisho, sheria ili ziende sambamba na matakwa ya wakati uliopo.

Wakili wa watoto wanaokinzana na sheria kutoka Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Pemba Siti Habib Mohamed, anasema haki ya msaada wa kisheria iendelee kuwanufaisha walioko kizuizini, kwa vile nao ni bindamu.



Mara baada ya kuwaapisha Makatibu wakuu, rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliwataka kuzifanyia marekebisho sheria ambazo zimepitwa na wakati.

                                               Mwisho   

   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch