NA ASHA SALIM- WKUMM, PEMBA@@@@
SEKTA ya kilimo Zanzibar, inaendelea kutumia nyezo muhimu na mipango
thabiti, katika kunyanyua wakulima waweze kujikimu na kunufaika kupitia shuhuli
za kilimo.
Katika kuhakikisha hilo, ushirikiano wa karibu kupitia washirika mbalimbali
wa maendeleo na miradi inayosainiwa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kusaidia
utekelezaji wa sekta hiyo zinaonekana.
Juhudi hizo, zinaendelea kwa ushirikiano wa karibu, kupitia idara zake,
zinazotekeleza majukumu yake chini ya wizara hiyo, na sasa serikali kujivunia
kufikia mafanikio makubwa ya kiuchumi.
Eeneo ambalo, serikali imekuwa na mfano mzuri wa utendaji kazi, ni
kushughulikia kwa karibu msitu wa hifadhi ya Ngezi Micheweni.
KWANI MSITU WA NGEZI ULIANZIA WAPI
Taarifa zilizopo kwenye tovuti ya ‘Ngezi
Vumawimbi Heritage Organization, zinaeleza
kuwa, maeneo yanayozunguka msitu wa
Ngezi, kumbe yamekaliwa kwa muda mrefu sana na Waarabu au Waajemi waliowahi
kuishi.
Infaghamika kuwa, kupitia tovuti
hiyo, mabaki ya misikiti na makaburi katika eneo hilo, yanaanzia karne ya 11
hadi ya 14.
Tena ambapo baaadhi ya miundo
inaonekana kutumika kama makao makuu na Waarabu au Waajemi, ambao waliishi hapo
zamani.
Kuanzia mwaka 1923, ndani ya msitu wa Ngezi, mpango wa kwanza wa usimamizi, maana mataifa
ya kikoloni ya Uingereza, yaliandaa mpango wa kwanza wa hesabu (takwimu za
msitu Ngezi).
Ambapo mpango na usimamizi, uliolenga
matumizi ya kibiashara ya bidhaa za misitu huo, wakijua kuwa kuna miti mipevu
na madhubuti kwa matumizi.
Kuingia mwaka 1957, mfanyabiashara wa
kihindi alieitwa V.R. Joshi, aliweka mashine ya kupasulia mbao, katika msitu
huo.
Maana mashine hiyo wala haikukaa
burea, na kuanza kupasua miti ya mbayo yenye thamani, ukiwemo mti wa Misaji.
Inaelezwa kuwa, baada ya zoezi hilo
kukamilika, mfanyabishara huyo, alisafirisha mbazo hizo za Msaji na kwenda nazo
nchini India, na sehemu nyingine za bara la Asia.
Ingawa
inaaminika kuwa, wazo la kuufanya msitu wa hifadhi, iliashaanza na ndio maana
inafahamika kuwa, mwaka 1959 uvunaji wa misitu ulifikia kikomo na Ngezi, ilipotangazwa
kuwa ni msitu rasmi wa hifadhi.
Baada
ya Zanzibar kufanya mapinduzi, inaarifiwa mashine maalum na za kisasa, zilitaifishwa
na serikali ya Rais Karume, na hapo ilipofika mwaka 1959, uvunaji ulisimamishwa
rasmi.
Mwaka
1996, serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini jemedari Abeid Amani Karume, ilianza
mpango mpya wa usimamizi, ambao ulizingatia usimamizi endelevu wa
rasilimali za msitu.
Hadi
mwaka 2004, serikali kupitia wizara husika, ilifanya juhudi kubwa za kulipanua
na kujumuisha Vumawimbi, kama sehemu ya msitu wa Ngezi ulioko wilaya ya
Micheweni Pemba.
Msitu
huo umepakana na bahari ya hindi kwa kaskazini na imezungukwa na vijiji 10,
vilivyomo pia shehia za Mkangale na Mkia Ng’ombe, katika upande wa mashariki,
magharibi, na kusini na una ukubwa wa hekta 2,900.
Ingawa hifadhi hii msitu wa Ngezi,
zipo taarifa nyingine zikihalalisha kuwa, inahusika na eneo la hekta 1, 440
(acre 3 600), nyingi ikijumuisha msitu wa msingi, ambayo ilianzishwa
mwaka wa 1959.
UFUNGAJI KAMERA ZA ULINZI MSITU WA NGEZI
Kupitia Idara ya misitu, mafanikio yanaonekana katika uhifadhi wa msitu
wa Ngezi Vumawimbi, kiteknologia kwa kushirikiana na mradi wa Oikos.
Hii ni baada ya kufunga kamera hivi karibuni, zinazosaidia kuona
wahalifu pamoja na kuona wanyama wanaohifadhiwa katika msitu huo.
Anasema ambao miaka ya nyuma hawakuwepo, sambamba na kuimarisha utoaji
wa elimu ya utunzaji wa misitu, na matumizi sahihi ya msitu huo kwa jamii.
Anaeleza kuwa, hata wanafunzi katika skuli zilizopo karibu na msitu inayowazunguka
kutoka idadi ya waliofikiwa na elimu ya misitu watu 1,600 mwaka 2020 hadi
kufikia 2200 kwa mwaka 2025/2026.
Anafafanua kuwa, ufungaji huo wa kamera, unalenga zaidi kuhakikisha usalama
wa msitu, ili kuona unazidi kunawiri na kuendelea kuwa tenuri la mapato kwa
serikali kuu.
Kumbe, wahalifu wa kuwinda wanyama na ukataji wa majengo, walikuwa
wakitumia nafasi ya uhaba walinzi na kupora mali za msitu huo.
Ndio maana serikali kuu, kupitia wizara husika, ilikuja na wazo ya
kufunga kamera ndani ya msitu huo, ili kuulinda kisasa zaidi, na kuona unawanufaisha
walio wingi zaidi.
Anasema, serikali imekuwa ikijivunia hifadhi hiyo, ambayo kwa sasa
inatimiza miaka 67, tokea kuasisiwa kwakwe mwaka 1959, na wakoloni waliokuwepo.
Akawataka wananchi, kuendelea kuilinda rasimali hiyo, ambayo imekuwa ikikitangaaza
kisiwa cha Pemba kiutalii, kwa kuwepo miti, ndege na wanyama adimu duniani.
Mkuu wa hifadhi hiyo Khamis Ali Khamis, anasema kamera zilizofungwa ni
24 na mbili ya kati ya hizo ni kwa ajili ya ulinzi wa wahalifu masitu na
zilizobakia ni kwa ajili ya kufuatilia wanyama.
‘’Hizi kamera za ulinzi zintasaidia mno kubaini wahalifu wa miti, lakini
hizi 22 kwa ajili wanyama, zimetusaidia kubaina aina nyingine za wanyama,’’anafafanua.
Hata Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, amekuwa akielezea
kukerwa kwake, na baadhi ya wananchi, wanaouhujumu msitu huo.
‘’Wakati mwingine hata wapika pombe haramu, wavunaji mbao na majengo nao
walikuwa kero, ingawa kwa sasa, baada ya kufungwa kamera hujuma sio sana,’’anasema.
Lakini akawataka wananchi, kuendelea kuisadia serikali, katika ulinzi wa
rasimali za msitu huo, ambao ni urithi kutoka kwa watawala.
WANAOZUNGURUKA MSITU HUO WANASEMAJE
Nassor Kassim Rashid ni mwananchi wa karibu ya eneo la msitu, anasema
hazina hiyo ni tunu, ambayo ni muhimu kwa maisha yao na wanyama na hata
serikali katika kuengeza pato.
‘’Hatuna budi kuulinda huu msitu, ni hazina kwa maisha ya viumbe hai,
watalii wanakuja kutoka mbali, kuona wanyama na miti adimu,’’anasema.
Issa Haji Machano, anasema wamekuwa walinzi wakubwa wa msitu huo, hata
kabla ya serikali kufunga kamera, maana upepo, mbolea na mvua wanazopata anaamini
ni uwepo wa hifadhi hiyo.
‘’Unajua sisi ambao tupo pembezoni mwa msitu huu, hata afya zetu
zimeimarika, maana tunaishi na kijani kibichi ambacho ndio nembo ya kisiwa cha Pemba,’’anasema.
Hidaya Ali Said, anasema wamekuwa wakiwapeleka wageni wao, wanaokuja
kuwatembelea, na kuondoka na mzigo wa elimu na maajabu mingine yaliomo hifadhini.
Hafsa Issa Haji, anasema hupeleka bidhaa wanapokuja wageni kuutembelea
msitu huo, na kuuza kwa thamani kubwa, kama vile mikoba ya ukindu na mikeka.
‘’Kwa sasa sijawahi kushuhudia wala kusikia uwepo wa wahalifu wa msitu
huo, au wawindaji haramu, maana serikali imeshafunga kamera maalum,’’anasema.
Msitu wa Ngezi ni miongoni mwa
mifumo muhimu ya ikolojia, na wanadamu hupata faida nyingi kutoka katika msitu,
ikiwemo ya kiuchumi, kiutalii, kiutamaduni na kimazingara.
Mwisho .




Comments
Post a Comment