Skip to main content

CFP, CFI, ‘GLOBAL AFFAIRS CANADA WAWATANGAAZIA NEEMA WANAOLIMA KILIMO MSITU

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ 

….kilimo ni maji, na maji ni kilimo…

Maji ndio mama wa taifa wa kilimo, bila ya maji hakuna kilimo.

 Ni maneno ya mtafiti wa kilimo kutoka Afrika Kusini, Mr. Rugeng Mjinja Zuma, wakati akiwasilisha utafiti wa kilimo mwaka 1999, chuo cha kilimo, nchini humo.

 

Akasema, kama mataifa yana baba wa taifa, basi kwenye kilimo, baba wa taifa ni maji.

 

Kelvin John Musetepe wa Burundi mtaalamu wa kilimo cha umwagiliaji, mwaka 2000, alimwambia Waziri wa kilimo nchini humo, kama hakuna maji, basi hakuna kilimo.

 

Waziri huyo, alikuwa ameshaondolewa kwenye nafasi ya uwaziri wa maji, miezi mitatu iliyopita, jambo lililomkasirisha.

 

Rais wa awamu ya nane ya Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, wakati akilihutubia Baraza la Wawakilishi, aliiagiza wizara husika, kuhakikisha huduma ya maji, iko vizuri.

 

‘’Sasa huduma ya maji sio tu kwa ajili ya matumizi ya ndani, kama kupikia na kunywa, sasa ni kwa ajili ya kuendeleza kilimo kwa manufaa mapana,’’akafafanua.

 


Akaenda mbali zaidi kuwa, bila ya kuwa na maji endelevu, hakuna kuvuna matunda na mazao ya uhakika Zanzibar.

 

Mpaka mwaka 2025, kupitia mradi wa uhuishaji na uimarishaji wa huduma za maji Zanzibar, matangi 15 yenye uwezo wa kuhifadhi lita milioni 134 yalishajengwa.

 

Taarifa ikafafanua kuwa, eneo jingine ni uchimbaji wa visima 64 yenye uwezo wa kuzalisha lita 177,000,000 kwa saa, vinaendelea kutumika Zanzibar,

 

Taarifa ya wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar ya mwaka 2022/2023 ilisema, visima vitano katika bonde la wakulima Cheju, vimeshachimbwa, kwa ajili ya umwagiliaji.

 

Ikafafanua kuwa, visima vyingine 20 katika mabonde ya wakulima ya Kibokwa, Kilombero na Cheju, vimewekewa pampu, kwa ajili ya kusukumia maji, kwenye mashamba yao.

 

Kimataifa, lengo la sita, kati ya yale Malengo Endelevu 17 ya dunia, linagusia maji safi na salama, kama lilivyo la 14, lililosisitiza, kuendelea uhai wa katika maji.

 


WAKULIMA KILIMO MSITU UNGUJA NA PEMBA WANASEMAJE

Wanaufaika 2,749 wakiwemo wanawake 2,086 na wanaume 663 wa mradi wa kukabiliana na mabadiliko tabianchi, ‘ZANZ ADAPT’ wanaendesha kilimo msitu.

 

Shehia ambayo ilitoa wanufaika wingi ni Uzi Unguja kuwa na 636, wakiwemo wanawake 508 na wanaume 128, ikifutiwa na Unguja Ukuu, iliyobeba wanufaika 385, ikiwa na wanawake 222 na wanaume 163.

 

Shehia ya Kambini Pemba, inao wanaufaika 374, Mchanga mdogo 253, Kiuyu Minungwini 305, Chwale 271, Ng’ambwa 266, na Bungi wanufaika 259.

 

Mradi huo wa ‘ZANZ ADAPT’, wa miaka mitano, utatia nanga mwaka 2029 utekelezaji wake, umekusanya wanufaika wanawake 2, 086 na wanaume 663 kwa Unguja na Pemba.

 

Ambapo awali, walishapewa mafunzo kwa miezi zaidi ya 18 iliyopita, na Jumuiya ya Uhifadhi ya Misitu Pemba ‘CFP’ wakishirikiana na Jumuiya ya kimataifa kama hiyo ‘CFI’.

 


Mkurugenzi wa ‘CFP’ Mbarouk Mussa Omar, baada ya mafunzo hayo ya kilimo msitu, walengwa hao wa mradi walitakiwa kwenda kuanza uotesha wa miti ya chakula na biashara.

 

Mradi huo upo kwa wananchi wa shehia nane, za Uzi, Bungi, Unguja Ukuu na Ng’ambwa kwa Unguja na Mchanga mdogo, Kambini, Chwale na Kiuyu Minungwini kwa Pemba.

 

WAKULIMA WALITII AGIZO HILO?

Makala hii ilizungumza na wakulima wanufaika wa shehia ya Mchanga mdogo wilaya ya Wete, akiwemo Fatma Bakari ambae kwa sasa, anayomashamba matatu.

 

‘’Baada ya mafunzo, kweli niliingia shambani na kuanza kupanda mitondoo 500, migomba 200, minanasi 200, miparachichi 50, na nimeshaanza kuvuna ndizi,’’anasema.

 

Kwake, jambo la shilingi 50,000 hadi shilingi 100,000 wala sio jambo la kuutesha moyo wake, kama ilivyo kabla ya kujiingiza kwenye kilimo hicho.

 


Mkulima Mtumwa Makame Shaame wa kijijini hapo, anasema ameitikia wito huo, akiamini kwanza atapata fedha za baada ya kuuza bidhaa zake, huku akikabiliana na mabadiliko tabianchi.

 

‘’Kwa hakika mradi huu, umekuja kutupa uwezo na mbinu za kukabiliana na mabadiliko tabianchi, huku tukijihakikishia chakula na fedha,’’anaeleza.

 




Mwenyewe amepanda mitondoo 50, migomba 150, minanasi 80, mihogo mashina 200 ambapo ameshaanza kuuza na kujiingizia fedha.

 

‘Sasa najiona mwanamke shujaa, maana najiendesha kwa kipato cha kilimo msitu, na huku nikijihakikishia chakula na matunda,’’anasema.

 

Sasa amekuwa hana hofu na michango ya familia, fedha za akiba na matumizi madogo madogo, mana suala la shilibgi 40,000 hadi shilingi 50,000 sio ajenda kwake.

 

Hata Zaituni Hassan Ali, anasema sasa anaona njia ya kujihakikishia kipato imeshachomoza, baada ya kupewa mafunzo na kuanza kilimo msitu.

 

‘’Na mimi nalima kilimo msitu ‘mchanganyiko’ faida yake, yamo mazao ya muda mfupi kama ndizi na muhogo, ya muda wa kati, kama mananasi na yale wa muda mrefu, kama miti ya ujenzi,’’anaeleza.

 

‘’Kwangu sasa kumiliki shilingi 30,000 hadi shlingi 200,000 najiamini maana kila siku 90, naingia shambani kuvuna mazao,’’anafafanua.

 

Wao wanaona kizinngiti kubwa, kwenye kilimo chao ni ukosefu wa huduma ya maji ya umwagiliajai, licha ya ahadi waliopewa na CFP, kwamba bado haijawafikia.

 

Wanakiri kuwa, kipindi cha jua, miti husinyaa na kupoteza mwelekeo, jambo linalowafanya baadhi yao kukata tamaa, kuendelea na kilimo hicho.

 

CHANGAMOTO YAO YA UKOSEFU WA MAJI ‘CFP’ WANAYO?

 

Uongozi wa Jumuiya ya uhifadhi wa misitu Pemba ‘CFP’ umeanza kutekeleza ahadi ya uchimbaji wa visima, kwa ajili ya wakulima wa kilimo msitu, kama walivyowaahidi.

 


Mkurugenzi Mtendaji ‘CFP’ Mbarouk Mussa Omar, anasema, tayari wameshaanza zoezi la uchimbaji wa visiwa, unaolenga kuwasaidia wakulima hao.

 

Tena, wameanzia katika shehia ya Kiuyu Minungwini, na kwa hatua za awali, kisima kimoja, chenye kuzalisha wastani maji lita 50,000 kwa saa kimeshakamilika.

 

Kisima hicho, kimeshajengewa mnara wenye urefu wa mita nne, ambao utakuwa na matenki manne, yenye kuhifadhi maji ujazo wa lita 20,000 ni lita 5,000 kwa tenki.

 

Kisima hicho kwa sasa wanaendelea kufanya mazungumzo na Shirika la Umeme Zanzibar ‘ZECO’ kwa ajili ya kuwahakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme.

 

‘’Ni kweli uongozi wa ‘CFP’ wakati waziri wa Kilimo alipowatembelea wakulima wa kilimo msitu shehia ya Mchangamdogo, tuliahidi kuwapatia huduma ya maji, na sasa tumeshaanza kutekelez ahadi hiyo,’’anafafanua.

 

Anaelekeza kuwa, kwa hatua za awali, utahusisha kisima kimoja kimoja, kwa shehia zote nane za Unguja na Pemba, ambazo mradi wa uhifadhi wa mazingira ‘ZANZ ADAPT’ unatekelezwa.

 

Ingawa baada ya kupata mwelekeo wa visima vya awali vinane, mradi utaendelea na uchimbaji tena wa visima vyingine kama hivyo.

 

‘’Kama mradi utakwenda vyema, lengo ni kila shehia zinazotekeleza mradi huu, kuwachimbia visima vitatu vitatu na miundombini yake, ili wakulima wa kilimo msitu, wawe na umwagiliaji wa uhakia,’’anafafanua.

 

TAMWA WALIFANYAJE KWENYE MRADI HUU

Kaimu Mratibu wa Chama cha waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, Amina Ahmed, anasema kwanza waliwajengea uwezo wanaufaika kuzungumza na vyombo vya habari.

 

‘’Hapa lengo lilikuwa ni kuwawezesha wanufaika hao, kuzungumza na vyombo vya habari, iwe pale wanapokumbana na changamoto au manufaa ya kazi zao waweze kujitetea,’’anaeleza.

 

Eneo jingine waliwawezesha waandishi wa habari, ili kuandikia fursa zilizomo kwenye mradi huo, ikiwemo wanufaika wakati wanakabiliana na mabadilikotabia nchi, kujiongezea kipato.

 

Anaeleza kuwa, ndani ya vikundi walivyovianzisha wanufaika, suala la uongozi, nafasi ya wanawake, njia ya kujiingizia kipato na kukabiliana na uchafuzi wa mazingira, liliandikwa.

 

MCHANGO WA SERIKALI KUU KWENYE KILIMO

Aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Shamata Shaame Khamis, akisoma bajeti ya mwaka 2025/2026, alisema mwaka 2021, sekta ya kilimo, imechangia asilimia 24.6 ya pato la taifa, ikilinganishwa na asilimia 22.8 iliyoripotiwa mwaka 2020.

 


Akafafanua, kwa mwaka 2024, sekta hiyo ilichangia asilimia 24.3 ya pato la taifa, ikilinganishwa na asilimia 24.9 iliyoripotiwa mwaka 2023, ambapo hiyo inaonesha kuimarika kwa sekta nyingine zinazohudumiwa na sekta ya kilimo.

 

Ingawa akafafanua kuwa, uzalishaji wa mazao ya kilimo umepungua kwa tofauti ya tani 144,870.8, kutoka tani 527,800 mwaka 2023, ikilinganishwa na tani 382,929.2 mwaka 2024, upungufu huo umetokana na kuwepo kwa vipindi virefu vya mvua na jua visivyotabirika.

 

Akabainisha kuwa, wizara imekuwa ikifanya jitihada za kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji, toka mwaka 2017, ambapo hadi sasa eneo lililowekewa miundombinu hiyo, imefikia ekari 5,750, sawa na hekta 2,300.

 

Kwa upande wa mazao ya misitu, takwimu zinaonesha kuwa mwaka 2024, matumizi ya kuni yamepungua kutoka mita za ujazo 25,909.7 mwaka 2023, hadi kufikia mita za ujazo 18,764.5 mwaka 2024.

 

Eneo jingine ni uzalishaji wa nguzo kubwa za miti, umepungua kutoka mita za ujazo 2,084.8 mwaka 2023 hadi kufikia mita za ujazo 1,259 mwaka 2024.

 

Aidha Waziri huyo, amaesema kwa ujumla, matumizi ya kuni yamepungua, kutokana na juhudi zinazochukuliwa ya kuhamasisha wanajamii, katika uhifadhi misitu inayowazunguka na matumizi ya gesi.

                            Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...