Skip to main content

PEMBE AWATAKA MAMA NTILE WAWE WABUNIFU KIBIASHARA

 

Na muandishi wetu

@@@@

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amewashauri wajasiriamali nchini, kuendelea kutumia ubunifu wao wa kupika vyakula mbalimbali kwa ajili ya biashara zao za mama ntilie ili waweze kujikwamua na umasikini.

Kauli hiyo ameitowa wakati akizungumza na wajasiriamali katika uwanja wa urafiki, Jimbo la Shaurimoyo, Unguja katika mashindano ya mapishi ikiwa ni shamrashamra za miaka 60 ya Mapainduzi ya Zanzibar. Mhe Riziki katika yeyete ile inahitaji ubunifu hivyo ni vyema mama ntilie wawe wabunifu katika mapichi mbali mbali katiba biashara ya chakula kwani hatua hiyo itasaidia kuongeza kipato na kujikwamua an umasikini.

Waziri Pembe amewataka wajasiriamali hao kuitumia fursa ya mikopo iliyopo  ikiwa ni juhudi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la  mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi ya kuwawekea mazingira wezeshi wajasiriamali kwa nia ya  kufikia malengo waliyojiwekea.

Aidha amesema Oryx Gas na Azania Group, wameamua kwa makusudi kuwasaid wajasiriamali  ili  kuhakikisha wajasiriamali wote nchini wanafanikiwa na wanakuwa mfano wa kuigwa katika kutoa huduma bora za vyakula popote nchini.



Naye Mwakilishi wa Jimbo la Shaurimoyo  ambae pia ni Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais  Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi Mhe.Hamza Hassan Juma, amesifu juhudi zinazofanywa na wajasiriamali wa Jimbo la Shaurimoyo kwa kuonesha ubunifu mkubwa wa vyakula mbalimbali ambao  utawasaidia kutambulika kitaifa na kimataifa.

Kwa upande wake Mwakilishi  kutoka Oryx Gas Bi Anjela Bitungwa amesema wameamua kuwapelekea nishati safi ya kupikia kwa lengo la  kulinda mazingira pamoja na afya kwa wajasiriamali wa jimbo la Shaurimoyo ili kuwaepusha na madhara ya kutumia kuni na mkaa na kuahidi kuendelea kuratibu  kwa kutoa  mitungi ya gesi 200, yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 25.

Naye msimamizi wa biashara ya Azania Group Bw Joel Laiser, amesifu hatua ya maendeleo iliyofikiwa hivi sasa chini ya Rais Dkt Mwinyi katika kuelekea  miaka 60 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, huku akieleza kuwa Azania Group itaendelea kushirikiana na viongozi wa Zanzibar kwa kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia nyenzo zote zinazozalishwa katika kampuni hiyo ili kuwasaidia wajasiriamali hao.



Washindi watatu wamepatikana na kupatiwa zawadi,  ambapo mshindi wa kwanza katika mashindano ya mapishi ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar amezawadiwa shilingi laki tano, Mchele, Unga wa Sembe, Unga wa Ngano kilo 50 kilo moja, Sukari  na Mafuta lita 20.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan