Skip to main content

INSPEKTA KHALFAN: ATAKA UDHIBITI MAJANGA YA MOTO

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

 

MKAGUZI wa shehia ya Pandani wilaya ya Wete Pemba, Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi, amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kujikinga na majanga mbali mbali yanayoweza kutokea ikiwemo ya moto.

 

Alisema kuwa, ni vyema kufuata utaratibu nzuri, wakati wanapoamua kujenga nyumba katika maeneo yao, kwa kuweka nafasi ya kutosha baina ya nyumba moja na nyingine, ili linapotokea janga la moto lisiweze kuathiri nyumba nyingi.

 

Aliyasema hayo wakati akikabidhi msaada wa vifaa vya skuli, kwa watoto wa familia ya mzee Mwalimu Kombo Said wa kijiji cha Madebeni shehia ya Pandani wilaya ya Wete, kufuatia tukio la moto lililounguza nyumba yao Novemba 11 mwaka jana.

 

Alisema kuwa, familia hiyo ilipata janga la moto ambao uliunguza nyumba yao na kuteketeza kila kitu kilichokuwemo ndani, hali iliyomfanya kuiahidi familia hiyo kuwanunulia watoto vifaa vyote vya kusomea.

 


"Nawapongeza wananchi kutafsiri kwa vitendo dhana ya ushirikishwaji wa jamii, kutokana na ushirikiano wao wa pamoja katika kuisaidia familia hiyo kwa hali na mali, baada ya kufikwa na tukio hilo la kuhuzunisha," alisema Mkaguzi huyo.

 

Aidha Inspekta huyo aliwataka wananchi hao, waendeleze umoja na upendo, kwani majanga kama hayo, hayachagui bali yanaweza kumfika mtu yeyote na wakati wowote, hivyo kila mmoja ni muathirika hawana budi kusaidiana.

 


Katika hatua nyengine, Mkaguzi huyo aliwaasa wazazi na walezi wa shehia hiyo, kuwahimiza na kuwasimamia vijana wao, washughulikie masomo yao zaidi, ili kujitengenezea maisha bora ya baadae, sambamba na kujiepusha na makundi maovu.

 

‘’Msingi bora na imara wa kumjengea mtoto wetu, ni kuwatenga mbali majanga mbali mbali ya udhalilishaji na kila wakati kuwahimiza, ili washugulike na masomo yao,’’alieleza.

 

Kwa upande wao wanafamilia, iliyoathirika kwa janga la moto pamoja na wanakijiji, walimpongeza Mkaguzi huyo, kwa kuonesha moyo wake wa upendo kwa kuisaidia familia hiyo, jambo ambalo limewafanya wajenge imani kwake.

 


Walieleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, limewakabidhi mtu muhimu na adhimu anaejali watu mbali mbali, jambo ambalo wamekuwa wakiridhia kila anachoweleza katika kuzuia uhalifu.

 

Aidha wananchi hao, wamemuahidi Inspekta huyo kuwa, watawasimamia vijana wao katika kuhakikisha wanapata elimu bora na kufuata maadili yaliyo mema, ili wajengeke vizuri na kupata mafanikio katika maisha yao ya kila siku.

 

Miongoni mwa vifaa vilivyotolewa na Mkaguzi huyo ni fomu za skuli, viatu, mabuku, kampasi pamoja na vifaa vyengine vya kusomea ambavyo vimegharimu kiasi cha shilingi 230,000 huku watoto wawili wakifaidika na msaada huo.

 

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan