Skip to main content

MAKAMU WA PILI AZINDUA BANDARI YA MKOANI, ASEMA NYINGINE TATU KUJENGWA PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, amesema, serikali inampango wa kuzijenga bandari za Wesha, Wete na Shumba, ikiwa ni miongoni mwa maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kukifungua kisiwa cha Pemba kiuchumi.

Alisema kwa kuanzia, tayari shughuli kadhaa zimeshafanyika kwa awamu ya kwanza, kuelekea ukamilishaji wa upanuzi wa bandari ya Mkoani, ikiwemo ujenzi wa njia za kupitia abiria, ujenzi wa eneo la kuwekea makontena pamoja na ununuzi wa mashine za kushushia makontena hayo.

Makamu huyo wa Pili, aliyasema hayo Disemba 7, mwaka 2024, bandarini Mkoani Pemba, mara baada ya uzinduzi wa bandari hiyo, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964,

Alisema, ili kuelekea uchumi mzuri, serikali inayodhamira ya kweli ya kuhakikisha bandari nyingine za kisiwani Pemba, zinajengwa na zinakuwa za kisasa, ili wananchi watanue wigo wa usafiri na usafirishaji.

Alieleza kuwa, kazi hiyo inatarajiwa kuanza wakati wowote, kwani baadhi ya kazi za muhimu kuelekea ujenzi wa bandari hizo, zimeshafanyika, kwa lengo la kukifungua kisiwa cha Pemba kiuchumi.






‘’Leo (jana), tukiwa ndani ya miaka mitatu ya uongozi wa Dk. Mwinyi samba mba na maadhimisho ya miaka 60 ya mapinduzi, bandari yetu ya Mkoani, iliyoasisiwa mwaka 1925, inaelekea kuwa ya kimataifa,’’alieleza.

Akizungumzia upanuzi wa bandari hiyo, alisema lengo la serikali ni kuona, bidhaa zinapotoka nje ya nchi, zinaletwa moja kwa moja katika badari hiyo kwa kushushwa.

Alieleza kuwa, mwisho wa wafanyabiashara wa kisiwani Pemba, kukumbana na changamoto ya uingaji wa bidhaa zao na kugharimu fedha nyingi, unaelekea kuwa mwisho, mara baada ya kumalizika kwa mradi huo.

Alifahamisha kuwa, kinachotakiwa kwa wananchi ni kuamini na kuipa nafasi serikali, kukamilisha awamu nyingine ya upanuziu huo wa bandari ya Mkoani, kama ilivyoahidi na Rais wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi.

‘’Lengo la upanuzi wa bandari ya Mkoani, ni kuwaondolea adha wasafiri, wasafirishaji wanaotoa a kuingiza bidhaa, ili kuona haziwagharimu, na kisha kuuza bei ya juu kwa walaji,’’alieleza.





Akizungumzia usafiri wa baina ya Unguja, Tanzania, Tanga na Pemba, Makamu huyo wa Pili, alisema tayari serikali iko katika hatua za mwisho, za ununuzi wa boti mbili za mwendo kasi.

Alieleza kuwa, boti hizo zinatarajiwa kufanya safari zake, baina ya miji hiyo, ili kuona wananchi wanakuwa na usafiri wa uhakika, pamoja na ile Meli ya M.V Mapinduzi II, iko katika hatu za mwisho ya kukamilika kwake.

‘’Kwa sasa meli hiyo, iko mbioni kukamilika, na serikali imeshaidhinisha ununuzi wa boti mbili, kwa ajili ya miji hiyo, na ziko hatua za mwisho kukamilika ujenzi wake,’’alieleza.

Akizungumza miaka 60 ya Mapinduzi, alisema yanashabihiana na kuasisiwa kwa bandari hiyo, kuanzia mwaka 1925, ambapo kisha mwaka 1989 bandari hiyo ikafanyiwa matengenezo.

‘’Tunapogusa maana halisi ya mapinduzi, ni maendeleo kupitia miradi mikubwa, ambayo inamgusa kila mmoja kwa alipo, na Dk. Mwinyi anakoleza mwendo wa kasi,’’alifafanua.

Mapema Mkurugenzi mkuu, wa Shirika la Bandari Zanzibar Akfu Khamis, alisema bandari ya Mkoani, imewekwa kama njia kuu ya kukifungua kisiwa cha Pemba kiuchumi, na hasa kupitia sera ya uchumi wa buluu.





Alisema kuwa, serikali, imedhamiria kuipanua bandari hiyo na kuiwezesha kumiundombinu, ili iweze kupokea meli za kimataifa moja kwa moja, kutoka nje ya nchi.

Mkurugenzi huyo Mkuu, alieleza kuwa, mradi huo mkubwa wa bandari, ulikuwa na awamu kadhaa ikiwemo ya kuweka kwa vikalio vya meli, na ujezi wa eneo la kuwekea makontena lenye upana wa skweya mita 4,200 .

Alieleza kuwa, awamu ya pili ni ujenzi wa njia kwa ajili ya kupita zana nzito, njia maalum ya watembea kwa miguu yenye upana wa mita 2.5 na uwekaji wakivuli kwenye njia hizo.

‘’Gharama za mradi huo, kuanzia awamu ya kwanza hadi ya pili, umeshatumia shilingi bilioni 6.77, pamoja na ununuzi wa mashine ‘crane’ tatu, mbili zikiwa na ujanzo wa tani 45 na moja tani 90, kwa ajili upakuzi wa makontena na mezani ya kidigitali,’’alieleza.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Dk. Khalid Salum Mohamed, alisema Dk. Mwinyi ameweka vipaumbele vinne, ikiwemo cha Uchumi wa buluu, utalii, miundombinu ya usafiri na usafirishaji, pamoja na huduma za kijamii.



‘’Kwenye miundombinu, Dk. Mwinyi amedhamira ujenzi wa kiwanja cha ndege, ujenzi wa bandari za Wesha, Mkoani, Shumba na Wete, ili kuongeza huduma za kijamii na kukuza uchumi,’’alisema.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema kila mmoja ni shahidi, juu ya miradi mikubwa iliyotekelezwa baada ya mapinduzi, ikiwemo upanuzi wa bandari ya Mkoani.

                                               Mwisho

 

  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan