Skip to main content

WANAWAKE MGELEMA SASA WASHUSHA PUUMZI NI BAADA YA...............

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAWAKE wa shehia ya Mgelema wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara yao kwa kiwango cha lami, roho zao zimewatua na hasa inpotekezea kutaka kwenda hospitali kuu, kufuata huduma za mama na mtoto.

Walisema, kwa karne zaidi ya moja, hawakuwa na furaha na wakielewa na machungu, inapotokezea wamepewa rufaa ya kwenda hospitali ya wilaya ya Chake chake, kutokana na shida ya barabara yao, ilivyokuwa.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, mara baada ya kufunguliwa kwa barabara yao ya Kipapo-Mgelema, na Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, walisema sasa joto limewatua.

Mmoja kati ya wanawake hao Maryam Mohamed Issa, alisema ijapokuwa ni mgeni kijijini hapo, lakini ameshatimiza miaka tisa ya mateso, shida na tabu ya kuitumia barabara hiyo.

‘’Binafsi, mara mbili nilipokuwa mjamzito, nilitakiwa niripoti hospitali ya wilaya ya Chake chake, kwa uchunguuzi zaidi, lakini nilishindwa kutokana na uchakavu wa barabara ulivyokuwa,’’alieleza.




Nae Mayasa Hassan Abdalla, alisema kwa mateso waliyokuwa nayo, hawakutarajia kuwa iko siku, wengepata barabara nzuri na ya kisasa, kama iliyofunguliwa hivi karibuni.

‘Tulishazoea sisi wajawazito hali ikiwa ngumu, na hasa kwa siku za mvua, ni kubebwa kwa magunia au gari za Ng’ombe, hadi bara bara kuu Kipapo,’’alifafanua.

Hata hivyo alisema, kwa sasa wamepata faraja ya kuongezewa thamani ya utu na heshima yao, kutokana na kuwepo kwa bara bara hiyo, ya kisasa.

Kwa upande wake Hassina Shehe Ussi na mwenzake Raya Hamad Naasor walisema, kwa sasa wana hakika hakuna dhiki ya usafiri na hasa kama ikitokezea, mwenzao amepata na hitilafu ya huduma za mama na mtoto.

Wakati huo huo wanawake hao, wameiomba wizara husika kuangalia uwezekano wa kuwekewa matuta katika maeneo ya mikusanyiko ya watu, ambapo bara bara hiyo imepita.

Kwa upande wa Omar Iddi Hassan, alisema barabara hiyo sio tija kwa wajawazito pekee, hata wao kwani ndio wasafirishaji wakubwa, ikitokezea mjamzito kupelekwa hospitali.

‘’Hakukua na tajiri aliyethubutu kuleta gari yake Mgelema, tena kwa bei yeyote, hivyo ilikuwa akitokezea mazazi amepata changamoto, ilikuwa ni dhiki mara mbili,’’alieleza.

Nae Omar Ussi Ali alisema, kilichobakia kwa sasa ni kwa watumiaji wa barabara hiyo, na wananchi wingine, kila mmoja kuwa mlinzi kwa mwenzake.

Akizungumza hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, alisema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imekuwa inatekeleza kila inachokiahidi.

Wakati huo huo Mkuu huyo wa wilaya, alisema wajibu wa kuitunza barabara hiyo sio jukumu la wizara husika pekee, bali kila mmoja na kwa nafasi yake.




Awali barabara hiyo ilifunguliwa hivi karibuni na Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, ambae nae aliwataka wananchi hao, kuhakikisha wanaitunza barabara hiyo.

Katibu Mkuu wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Khadija Khamis Rajabu, alisema ujenzi wa barabara hiyo ya Kipapo- Mgelema yenye urefu wa kilomita 5.3, ujenzi wake uligawika katika awamu mbili, ambapo moja wapo ni ujenzi wa Kipapo –Mgelem.

Aidha Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa, barabara hiyo ina upana wa mita sita, na mabega {road shoulder} yenye upana wa mita 0.5 kwa kila upande, na ujenzi wake umetumia mfumo wa lami moto.

Alieleza kuwa, kama barabara hiyo ya Kipapo- Mgelema itatunzwa inaweza kuishi kwa wastani wa miaka 10, bila ya kuharibika.

Ujenzi wa barabara hiyo, hadi kukamilika kwake, umeshatumia zaidi ya shilingi bilioni 2.109, fedha zilitolewa na serikali ya Mapinduzi, kupitia Mfuko wa Bara bara na imejengwa na Wakala wa Barabara Zanzibar.

                                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan