Skip to main content

MAJUKUMU MAZITO YA FAMILIA CHANZO CHA WANAWAKE KUTOGOMBEA UONGOZI

 




IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

Jamii ya Tanzania, kama ilivyo katika nchi nyingi nyengine, imejenga mazoea ya kuwa mwanawake ni mama wa nyumbani tu na hapaswi kushiriki au kushirikishwa katika mambo ya maendeleo.

 

Kwa maana nyengine mwanamke amekuwa kama abiria katika basi na hana maamuzi juu ya safari, seuze ya kupewa usukani wa kuongoza hicho chombo.                   

 

Mtazamo huu uliokuwa unatumika kwa muda mrefu umeiathiri jamii na kumuacha mwanamke kuwa nyuma, jambo ambalo sio sahihi kabisa.

 

Hali hii ipo kinyume na mafunzo na maelekezo ya dini mbali mbali. 

 

Kwa mfano, katika dini ya Kiislamu mwanamke hatakiwi kuachiwa pekee mzigo mzito wa nyumbani na pamekuwepo matokeo ya mwanamke kupewa uongozi hata katika masuala mazito, kama ya kuongoza kikosi kwenye vita.

 

Zipo hadithi sahihi na simulizi nyingi juu ya namna wanawake walivyoongoza kwa mafanikio, wakiwa kama majeshi.

 

Mzigo mzito wa nyumbani wanaoachiwa akina mama umekuwa sababu kubwa ya kuwakwaza na kushindwa kushiriki katika shughuli za jamii, uchumi, siasa na maendeleo.

 

Katika visiwa vya Unguja na Pemba wapo wanawake ambao wanakiri kwamba kikwazo kikubwa kwao kujiendeleza kimaisha na hata kushika nafasi za uongozi ni mzigo mzito wa malezi na kazi za nyumbani.

 

Miongoni mwa wanawake wenye uzoefu wa kuielewa hali hii inayowakuta wanawake wengi ni Saumu Ali Abeid, mkaazi wa Fuoni, Unguja.

 

Anasema, uzito wa kazi za nyumbani unaomzunguka mwanamke ni pamoja na kupika, kushughulikia usafi wa nyumba, malezi ya watoto, kumhudumia mume na wakati mwengine wazee wa mume na wa kwake mwenyewe.

 

‘’Katika hali kama hii sio rahisi kwa mwanamke kujiingiza katika harakati za kugombea uongozi," anaeleza.

 

Anafahamisha kwamba, mwanamke anayezongwa na kazi nyingi za nyumbani hushindwa kushiriki kwenye vikundi na kutoa mawazo yake ambayo yangempa ujasiri na maarifa na hivyo kujiamini kuwa anaweza kuongoza wenzake au jamii.

 

Mwananchi wa kijiji Kipangani Wete, anasema, mzigo wa kazi za nyumbani aliokuwa nao mwanamke umepelekea kuwepo wanawake wachache katika vyombo vya maamuzi.

 

Hii ndio moja ya sababu ya kushindwa kutatuliwa changamoto kadhaa zinazowakabili wanawake, kwani panakuwa hakuna mtetezi wa hali ya wanawake katika vyombo vya maamuzi.

 

"Kazi za nyumbani zinatuchosha sana na kushindwa kujiingiza kwenye mambo ambayo yatailetea maslahi jamii kwa ujumla," aliongeza.

 

Maida Saleh yeye ameona mzigo mzito wa nyumbani unadumaza fikra za mwanamke na hivyo kupoteza haki zao.

 

Salama Mohamed wa Ole Pemba, anasema mara nyingi mrundiko wa kazi za nyumbani unawazuwia wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi.

 

Hafidh Abdi Said ambae ni Mkurugenzi wa mradi wa kutoka PEGAO anasema, kazi nyingi za nyumbani zinasababisha wanawake wengi kutoshiriki katika uongozi.

 

‘’Tokea mwanamke anapoamka ni kazi mpaka jioni huwa hana hata muda wa kupumzika au kufanya mambo mengine nje ya kuta ya nyumba yake’’, aliongeza.

 

Alitoa nasaha kwamba kama jamii itaendelea kuwaachia mzigo mzito akinamama basi hata maendeleo ya nyumbani yatachelewa kupatikana.

 

‘’Mwili unahitaji mapumziko ili baadaye uweze kufanya vizuri’’, anaeleza.

Katibu Kanda ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Pemba, Habid Ali Khamis anaeleza, wanawake wanakosa msaidizi, hivyo hata anapokwenda kwenye vikao anachelewa na hatimae kukosa ajenda zilizozungumzwa, ambapo yeye huishia kuwa msikilizaji.

Mwalimu Saleh Nassor Juma ambae ni Katibu wa ACT Wazalendo Mkoa wa Chake Chake kichama, anasema elimu inahitajika zaidi ili wagombee na kazi za nyumbani isiwe kikwazo kwao kuwa viongozi.


 

ATHARI YAKE 

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said anasema, akinamama watashindwa kuingia katika vyombo vya maamuzi na hatimae hawana mtetezi katika masuala yao.


''Tunajitahidi kuwajengea uwezo wanawake kwa kuwapa elimu na jamii kwa ujumla, ili kuondosha dhana potofu na wajiamini kuingia majimboni,'' anafahamisha.





Saumu Ali mkaazi wa Fuoni anasema, mwanamke huwa anadumaa kiakili pale ikiwa hana jengine la kufanya baada ya kuhudimia nyumbani.

 

"Mwanamke aliyeelemewa na kazi za nyumbani huwa hapati fursa ya kujiendeleza, inawezekana ana mawazo mazuri ya kuleta mabadiliko na maendeleo katika jamii, lakini hapati fursa ya kwenda kuyatoa, hivyo, mawazo yake huwa anakaa nayo tu moyoni," aliongeza.

 

Awatif Ramadhan Awesu  wa Kariakoo Dar-es-salaam anataja athari ya mwanamke kubanwa na kazi za nyumbani  ni kuendeleza ukosefu wa usawa wa kijinsia na kuzuia maendeleo yao kitaaluma.

 

Anasema mwanamke anayezidiwa na majukumu ya kifamilia anakosa muda wa kujijengea uwezo, kujifunza na kujiendeleza katika uwanja wa uongozi.

 

‘’Hali hiyo huchangia ukosefu wa usawa kwenye fursa za uongozi na kuwafanya wanawake washindwe kufikia uwezo wao kamili katika maswali ya kazi na uongozi’’, alisisitiza.

 

Zainab Hassan Ali, mkaazi wa Bopwe Wete anasema inakuwa vigumu kwa mwanamke anayekuwa nyumbani wakati wote kupanua akili yake au kuchanganua mambo kwa sababu akili yake inabaki nyumbani na haitoki nje ya kuta za nyumba hizo.

 

TUNAWASAIDIAJE WANAWAKE.

 

Mkaazi wa shehia ya Uwandani Wilaya ya Chake Chake, Safia Abdalla, anaamini ushirikiano katika familia unawapa nafasi wanawake kushiriki katika masuala ya kijamii na hatimae kuwa na ujasiri wa kivifikia vyombo vya maamuzi.

 

Anashauri kutolewa elimu zaidi ili imsaidie mwanamke kujipanga mapema kushiriki katika mambo mbali mbali ya kijamii, kiuchumi na kimaendeleo.

 

Kilichoitokeza katika mahojiano zaidi na wanaume na wanawake wa maeneo mengine ni kuwepo umuhimu wa kuubadili mwenendo wa maisha katika familia zetu na zaidi kwa wanaume kuwapunguzia kwa njia moja au nyenine wenza wao na hata watoto wao wa kike mzigo mzito wa kazi za nyumbani.


Wapo walioshauri wanawake wapewe elimu ya kujitambua ili wapate uelewa mzuri utaowafungulia njia ya kujiendeleza na hata kuwa viongozi katika jamii.

                     MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan