Skip to main content

DCU: TOWENI VIBALI VYA MIRADI HARAKA DK: MNGEREZA

 



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI        06/03/2023

 

DCU Toweni Vibali vya Miradi Haraka - Dkt Mngereza

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Dkt. Mngereza Mzee Miraji ameitaka Kamati ya Udhibiti na Usimamizi Ujenzi (DCU) kutochelewesha kutoa vibali vya miradi ili ujenzi wa miradi hiyo utekelezwe kwa muda  uliyotakiwa.

Dkt. Mngereza aliyasema hayo jana baada ya kupokea maoni ya wajumbe katika kikao cha 74 cha kamati hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Baraza la Manispaa ya Magharibi “B” Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, alisema maombi ya vibali vya miradi yasikae muda mrefu yawe yamejibiwa ili ujenzi wa miradi uanzwe kutekelezwa kwa wakati.

Pia aliitaka kamati hiyo kuanzisha utowaji wa vibali vya ujenzi kwa njia ya mfumo wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia (ICT) ambapo utawezesha kamati hiyo kufanya majukumu yao ipasavyo.

“Vibali vya miradi visikae muda mrefu havijatolewa, kuwe na time frame, pia kuwe na land forum, mfikirie kuanzisha mfumo wa ICT na mkimfanye kazi kwa mashirikiano itasaidia kupunguza malalamiko” Alisema Dkt. Mngereza.

Aidha Dkt. Mngereza alisisitiza  umuhimu wa  kuitumia ardhi vizuri. Alisema ardhi ikitumika kwa mujibu wa matumizi yake ndio maendeleo ya kiuchumi Zanzibar yatafikiwa kwani mipango bora katika sekta ya ardhi ni kwaajili ya huduma za makaazi na kiuchumi ndio adhma ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Sambamba na hayo Katibu Mkuu huyo  alisema wizara yake itajenga nyumba za Maendeleo sehemu mbali mbali ambayo wameyaainisha ila hakusema eneo lipi litakuwa la kwanza kujengwa, bali  alieleza muda sio mrefu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi itasaini mkataba wa ujezi  wa nyumba za mkopo wa bei nafuu.

Naye Mkurugenzi Idara ya Ardhi kutoka Kamisheni ya Ardhi Zanzibar Ndg. Mtambua Hamziji Haji aliunga mkono hatua ya kuanzishwa Jukwaa la Ardhi (Land Forum) kwani litaweza kusaidia  watendaji wa sekta ya hiyo kuzungumza kwa kina na kila mmoja atazungumza kinachomhusu katika majukumu yake.



“Bora kuwe na Land forum kwasababu DCU wao wanalenga kukusanya mapato na kusahau matumizi bora ya ardhi wakati ardhi ikitumika vizuri mapato yatapatikana kwa mujibu wa matumizi yake, sisi Kamisheni ya Ardhi tunasimamia matumizi bora ya Ardhi” Alisema Haji.

Kwa upande wao wajumbe wa  Kamati ya Udhibiti na Usimamizi Ujenzi (DCU) wamelalamikia ukosefu wa fedha katika kutekeleza majukumu yao kwani wanakusanya fedha kutokana na utowaji wa vibali vya ujenzi na kuingiza katika mfuko mkuu wa Serikali lakini fedha hazirudi (return) hali ambayo inapelekea kutokutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Kikao hicho cha Kamati ya Udhibiti na Usimamizi Ujenzi (DCU) kimeandaliwa na  Mkurugenzi Mipango Miji Muchi Juma Ameir ambae ndie mwenyekiti wa kamati hiyo.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch