Skip to main content

WANAFUNZI WENYEULEMAVU WASUBIRI KUONANA NA RAIS DK. MWINYI

 


Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi ameridhia kukutana na wanafunzi wenyeulemavu waliofaulu mitihani yao ya taifa ya kidato cha nne na sita angalau kwa kupata ufaulu wa daraja la pili badala ya kuonana na wanafunzi wote wanaopata daraja la kwanza kila mwaka.

Dk Mwinyi ameridhia ushauri huo wakati akizungumza na waandishi wa habari Ikulu Zanzibar mwishoni mwa mwezi uliopita baada ya muandishi mmoja wa gazeri la Nipashe kumshauri Dk Mwinyi kukutana na wanafunzi hao ili kuwafariji kama anavyowafaraji wanafunzi wingine.

“Ni kweli kila mwaka nawaita wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja la kwanza kwa ajili ya kuwapongeza na kuwapa zawadi lakini kwa bahati mbaya huwa hakuna wenyeulemavu lakini kama wapo waliopata angalau daraja la pili hii itakuwa ni nafasi yao maalum nitakutana nao”anasema.

Kauli hiyo ya Dk Mwinyi imeungwa mkono na wanafunzi Abdulazizi Ali Khamis mwenye ulemavu wa Uziwi ambae amepata daraja la pili la ufaulu katika mitihani yake ya kidato cha nne mwaka huu.

Mwanafunzi huo anasema kwa mwanafunzi mwenyeulemavu hasa kiziwi kupata daraja la pili ni hatua ya kupongezwa kutokana na changamoto wanazokabiliana nazo katika kupata elimu.

“Bado kuna uhaba mkubwa wa walimu wanaojua lugha ya alama na mwanafunzi kiziwi lugha ya alama ni njia moja wapo itakayomuwezesha kufanya vizuri katika mitihani”anasema.

Aidha anaiomba serikali kuongeza idadi ya walimu wa lugha ya alama Skuli ili wanafunzi viziwi kuwa na mawasiliano mazuri hasa mwalimu anapofundisha darasani.

“Bila ya kuwa na mwalimu wa lugha ya alama sisi viziwi tunakosa mawasiliano na kutofahamu kile ambapo amekifundisha mwalimu darasani”anasema.

Abdul -Azizi ni miongoni mwa wanafunzi 103 wa Shule ya Sekondari ya Dk John Joseph Magufuli visiwani Zanzibar, amefanikiwa kupata alama hiyo katika matokeo ya mitihani ya Kidato cha nne yaliotangazwa hivi Karibuni na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).

Licha ya ulemavu alionao Abdul-Azizi  amewapita wanafunzi wezake wasio na ulemavu na ni  mwanafunzi pekee kwa Zanzibar  mwenye ulemavu wa uziwi aliepata ufaulu huo wa masomo ya sayansi.

Shule aliyosoma  imetoa wanafunzi 9 waliopata daraja la pili la ufaulu akiwemo yeye, wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja la kwanza ni mmoja, 28 daraja la tatu, 59 daraja la nne na sita daraja sifuri.

Anasema siri ya mafaniko yake ni juhudi zake za kusoma kwa bidii, juhudi za walimu wake, wazazi wake na wakalimani ambao walikuwa wakijitolea pamoja na ushirikiano kutoka kwa wanafunzi wezake.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch