Skip to main content

SMZ KUKOMESHA TATIZO LA OMBAOMBA

 




Na Mwandishi Wetu::::::


WAPO  baadhi ya watu huwatumia watu wenye ulemavu kama ni mtaji wa kuwapatia kipato hali ambayo imechangia kuwepo kwa idadi ya ombaomba kwa watu wenyeulemavu Zanzibar.

Kwa kuliona hilo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewaonya wenye tabia hiyo ya kuwatumia watu wenyeulemavu kwa shughuli zao binafsi ikiwemo za ombaomba watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na idara maalum SMZ Masoud Ali Mohamed, anasema  serikali inafahamu kuwepo kwa watu wanaowatumiya watu wenye ulemavu kwa ajili ya kujipatia kipato binafsi.

 Waziri huyo anasema serikali inafahamu kuwepo kwa matukio ya aina hiyo ambapo tayari baadhi ya watu wamekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa ajili ya kuwatumiya watu wenye ulemavu.

Anasema watu hao waliokamatwa wamekutwa wakiwahifadhi watu wenyeulemavu katika nyumba moja visiwani Zanzibar na huwasambaza katika maeneo mbalimbali ya mji wa Zanzibar kwa ajili ya kuomba ili kupata fedha.

Anasema jumla ya watu watano wamekamatwa katika eneo la Mboriborini Unguja katika nyumba moja wakiwa wamewaweka watu wenye ulemavu kwa ajili ya kuwatumiya kwa shughuli za ombaomba katika maeneo mbalimbali ya mjini.

 Anasema kwa mujibu wa sheria ya watu wenye ulemavu namba nane ya mwaka 2022 ni makosa kuwatumiya watu wenye ulemavu kwa ajili ya shughuli binafsi ikiwemo kuwapa majina mabaya na kuwatumiya kwa maslahi yao.

 ‘’Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar itahakikisha inaitumiya sheria ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2022 ambayo imewabana watu wanaowatumiya watu wenyeulemavu kwa maslahi yao binafsi na kujipatia kipato ikiwemo shughuli za ombaomba’’anasema.

 Aidha anasema matukio ya ombaomba sio silka na mila za utamaduni wa wananchi wa Zanzibar kwa hivyo vitendo hivyo vinatakiwa vidhibitiwe.

Anasema katika kudhibiti kitendo cha ombaomba hasa kwa watu wenyeulemavu serikali imetoa fedha kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kufanya shughuli mbalimbali za ujasirimali kwa lengo la kuepukana na matukio hayo.

 ‘’Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar tutahakikisha tunapambana na matukio ya ombaomba katika maeneo mbalimbali ambapo tumejipanga kuona kwamba watu wenye ulemavu tunawawezesha katika vikundi mbalimbali kukomesha matukio hayo’’alisema.

Katibu wa baraza la Taifa la watu wenyeulemavu Zanzibar, Ussi Debe anasema baadhi ya watu wanawatumia watu wenyeulemavu kama ni mtaji jambo ambalo si sahihi na linavunja utu na heshima kwa watu wenyeulemavu.

“Utawaona watu wenyeulemavu hasa wale wenye umri mkubwa au watoto wanaongozwa kupitishwa katika maduka wakiomba pesa kwa kweli kitendo hiki kinaniskitisha sana maana huwafanya kama ni mtaji wao”anasema.

Aidha Mkurugenzi huyo anasema ulemavu usiwe kigezo cha kutumikishwa au kudhalilishwa kwa sababu wanahaki ya kutafuta kipato kwa njia zinazokubalika kama walivyo watu wingine.



Mwenyekiti wa shirikisho la watu wenyeulemavu Zanzibar, Mwandawa khamis vitendo vya udhalilishaji au utumikishwajwi wa watu wenyeulemavu vinahitaji kupigwa vita na kila mmoja.

Anasema kuenelea kwa vitendo vya Ombaomba kwa watu wenyeulemavu kunasababisha kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji kwa watu hao hivyo ni vyema vikakomeshwa.

Aidha anasema watu wenyeulemavu wanahitaji kuwezeshwa kwa kupatiwa mititaji kwa ajili ya kufanya biashara na kumudu gharama za maisha.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch