Skip to main content

MCT LATOA TATHIMINI UHURU WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI

 



Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Tathmini ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) kuhusu hali ya uhuru wa vyombo vya habari nchini

 

leo Agosti 04, 2022

Kanzidata ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) imerekodi matukio 10 ya madhila ambayo waandishi wa habari wamekutana nayo katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Julai mwaka 2022.

Hii ni kwa mujibu wa kanzadata hiyo ambayo inapatikana kwenye www.pressviolations.or.tz

Madhila ambayo Baraza limeyarekodi kwenye kanzidata yake katika kipindi hicho ni matukio matatu ya vyombo vya habari kufungiwa, tukio moja la kunyanyaswa, matukio matatu ya kukamatwa, kunyimwa taarifa na matukio mawili ya waandishi kutishiwa.

Katika matukio hayo polisi wanaongoza kwa kuwa taasisi yenye migogoro na waandishi wa habari, ikifuatiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Matukio mengine ni ya waandishi wa habari kutishwa, yakitolewa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma tukio moja, na la watu wasiojulikana pia tukio moja.

Kipindi kama hiki mwaka jana kulikuwa na madhila 14 ya ukiukwaji wa haki za waandishi wa habari.

Madhila hayo kwa mwaka jana yalikuwa kufungiwa tukio moja, udhibiti hasi binafsi (self-censorship) (1), kukamatwa (4), kunyimwa taarifa (2), mauaji (1), vifaa kuharibiwa (1), na vitisho matukio manne.

Kwa mujibu wa kanzidata ya MCT, kipindi cha mwaka 2020 kanzidata hiyo ilirekodi matukio ya ukiukwaji wa haki za waandishi wa habari 43 wakati mwaka 2021, ilirekodi matukio 25.

Kwa jinsi hali ilivyo hivi sasa matukio hayo yamepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na miaka iliyopita.

Tumekuwa tukishuhudia mabadiliko kutoka kwa utawala ambao ulibana uhuru wa vyombo vya habari na wamiliki wa vyombo vya habari hadi kuvifuta mpaka utawala wenye kuanzisha mchakato wa kupitia sheria za vyombo vya habari ili kurekebisha sheria kandamizi kwa uhuru wa vyombo vya habari.

Kuthibitisha hilo, Februari 10, 2022, wakati akitoa leseni kwa magazeti manne yaliyokuwa yamefungiwa, Waziri Nape Nnauye aliweka wazi kuwa kufunguliwa kwa vyombo vya Mawio, Tanzania Daima, Mseto na MwanaHALISI yalikuwa ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa MCT, ishara ya kwanza kwamba mabadiliko yanakuja ilikuwa utayari wa mawaziri kufanya maongezi na wadau, ambapo wakati wa utawala uliopita Baraza lilihangaika bila mafanikio kwa muda wa miaka mitatu kupata nafasi ya kukutana na Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni bila mafanikio wala barua kujibiwa.

Lakini ndani ya utawala wa Rais Samia, katika kipindi cha miezi mitatu Umoja wa Haki ya Kupata Taarifa (CoRI) ulikuwa umekutana na Waziri wa iliyokuwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Waziri wa Katiba na Sheria ili kujadili mfumo wa kisheria unaoongoza vyombo vya habari. Baadae walikutana pia na waziri wa sasa wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. Haya ni mabadiliko makubwa na ya kuungwa mkono.

Hapo awali tulishuhudia msururu wa sheria mpya zilizotungwa, wakati mwingine kwa hati ya dharura, na ambazo zilikandamiza uhuru wa vyombo vya habari, ambazo ni pamoja na Sheria ya Uhalifu wa Mtandaoni, 2015 na Kanuni zake za 2016, Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari, 2016, Kanuni za EPOCA (Maudhui ya Mtandaoni) 2018. Kitu ambacho kwa sasa hakionekani kujitokeza na sheria hizi hizi ziko katika mchakato kubadilishwa.

Kipindi kilichopita muda kama huu wa kati ya Januari mpaka Julai, wahariri wangekuwa wamepokea simu za kuonywa kuacha kuandika habari fulani, na simu hizo ni kutoka ndani na nje ya vyombo vyao vya habari.

Kutokana na hofu iliyokuwa imetanda katika tasnia ya habari, ilifikia hatua wamiliki wa vyombo vya habari wakawa wanaingilia uhuru wa uhariri kwa kuhofia leseni zao kufungiwa au kufutwa na mamlaka, kutokana na kurushwa au kuchapishwa kwa habari fulani.

Kubadilika kwa hali hiyo kunasababishwa na utayari wa kiongozi mkuu wa nchi ambaye ameonyesha kuithamini tasnia ya habari na kuwa tayari kufanya nayo kazi.

Matamshi ambayo yanatolewa na viongozi hasa wanaosimamia tasnia ya habari ni dalili tosha kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wa tasnia ya habari tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo waandishi wa habari walionekana kama maadui wa serikali.

Kitu kikubwa cha kuzingatia ni kuhakikisha tunaendelea kufanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha sheria zote kandamizi zinafanyiwa marekebisho.

Tasnia ya habari inapaswa kukumbuka kuwa sheria kandamizi bado zimo vitabuni. Haki ya raia kujieleza na kupashana habari ni haki ya msingi na haipaswi kutegemea tu nia njema ya kiongozi aliyeko madarakani. Wakati tukimpongeza Rais kwa kuonyesha nia ya kuleta mabadiliko, hatupaswi kubweteka, tuendelee kusukuma mbele mchakato wa kubadilisha hizi sheria. Bila sheria kubadilika kicheko tulichonacho hivi sasa kunaweza kuwa cha muda mfupi.

Kajubi D. Mukajanga

Katibu Mtendaji

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch