Skip to main content

PACSO PEMBA YAWAPA UJUMBE MZITO WASIOPENDA MIGOGORO

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA:

email: hajipembatoday@gmail.com:


JAMII kisiwani Pemba, imetakiwa kujitenga mbali na baadhi ya watu wanaotumia vibaya nafasi zao, kwa kushawishi kujiingiza kwenye migogoro isiyokuwa na tija, kwani amani itakapochafuka, gharama ya kuirejesha ni kubwa.

Hayo yalielezwa na mtoa mada, ya utatuzi wa migogoro kisiwani humo, Ali Abdalla Juma, wakati akielezea njia za kujinga na migogoro, kwenye mafunzo ya siku mbili ya utatuzi wa migogoro, yalioandaliwa na Jumuiya mwemvuli ya asasi za kiraia kisiwani Pemba PACSO, na kufanyika Chake chake.

Alisema, inawezekana mtu kwa sababu ya cheo chake au umaarufu wake katika jamii, akalikusanya kundi mfano kama la vijana, na kuwashawishi kuvunja amani, akijua matokeo yake ni kujipatia maslahi yake binafsi.

Mtoa mada huyo alieleza kuwa, jamii lazima ione umuhimu wa kuwepo kwa amani na utulivu, na vivyo hivyo wawe mashuhuda wazuri, kwa nchi zilizotumbikia kwenye migogoro, namna ambavyo maisha yanakuwa magumu.

‘’Sisi jamii, lazima kama kuna mtu kwa sababu ya cheo chake anataka kututumia vibaya, tujitenge nae, maana migogoro inapokuwa kuwa mikubwa, huzaliwa vurugu na mauwaji,’’alieleza.






Katika hatua nyingine, amewataka washiriki hao, wanapopokea migogoro kutoka katika jamii zao, lazima waangalie chanzo, wahusika, athari na kisha waanze kutoa elimu ya upatanishi.

Akifungua mafunzo hayo, Mwenyekiti wa ‘PACSO’ Mohamed Ali Khamis, alisema suala la ndoa kuwa ni chanzo cha migogoro, sio dhana sahihi, bali wanandoa kwa tabia zao mbaya, ndio inayopelekea migogoro.

Alieleza kuwa, suala la ndoa hata la wake wanne, kwa imani ya dini ya kiislamu, halina shida, bali ikiwa wanandoa watakosa kuaminiana, wao ndio huwa chanzo cha migogoro.



‘’Hata nafasi ya usheha, uhakim, majaji mahakamani, ndoa, ofisi ya Mufti kama vilivyo na asili yake, huwa havina shida, bali watumishi wa tasisi hizo, kama sio waamifu wanaweza kuzalisha migogoro,’’alieleza.

Mapema Katibu Mkuu wa PACSO Sifuni Ali Haji, alisema wapo wanaoshika nafasi za usheha, mahakimu na majaji, wamekuwa chanzo cha migogoro, kutokana na kukosa uaminifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Wakichangia mada kwenye mafunzo hayo, washiriki hao walisema, bado wanandoa, wamiliki wa ardhi kinyume na sheria, wamekuwa wakisababisha migogoro kwa jamii.

Walisema, kama wenye mamlaka katika uongozi, wakishindwa kutenda haki na wakaendeleza ubaguzi miongoni mwa jamii, hapo huwa rasihi, kuzaliwa kwa migogoro.

Mchungaji Benjamen Kissanga, alisema haki ndio tunda la amani, ambalo kisha huzaa upendo na wananchi kuishi kwa amani.

‘’Ikikosekana haki kwa jamii, na uvumilivu ukifikia mwisho, huwa rahisi kuzaliwa na migogoro ambayo mwisho wake, ni vurugu na visasi vya muda mrefu,’’alieleza.






Nae Mwenyekiti wa Jumuiya ya wasioona Pemba ‘ZANAB’ Suleiman Mansour Suleiman, alisema wanasiasa kwa kule kutotosheka na madaraka, wamekuwa wakiwagonganisha vichwa wananchi na kuzaliwa kwa migogoro.

Nae Khadija Ahmed, alisema kukosekana kwa uvumilivu na kutoheshimiana kwa wanandoa, hupelekea migogoro ambayo mwishowake, huvunjika kwa ndoa.

Sheha wa shehia ya Wara Massoud Mohamed Khamis na mshiriki Hamad Faki Rashid, walisema elimu ya uraia, utaifa na uzalendo unahitajika kwa jamii, ili kuzuia migogoro.

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyotayarishwa na PACSO kwa kushirikiana na the foundation for Civil Society na Search for Common Ground, na yamefadhiliwa na Umoja wa nchi za Ulaya EU.     




Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch