Skip to main content

SAKINA KHAMIS WA PEMBA: RUZUKU YA TASAF YAMZALISHIA RUNDO LA MIRADI

 




Alianzia nazi, genge, samaki wa kukaanga, sasa auza nguo


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

email:: hajipembatoday@gmail.com


‘’MIMI sasa sijioni mwanamke, najiona kama mwanamme mwenye uwezo mkubwa, ndio maneno ya mwanzo wa mlengwa kaya maskini Sakina Khamis Mbwana miaka 37, wa kijiji cha Tumbe Mashariki Pemba.

Nilipotaka kujua kwanini asijifananishe na mwanamke aliyepata mafanikio, kwanza aliagusha kicheko na kusema, ameshahama kwenye uwanawake kiuwezo, na sasa ni sawa na mwanamme.

Nilipomng’ang’ania sababu za kujifananisha na mwanamme, alisema ilishazoeleka na kuaminika kuwa mwanamke hawezi kwa na mafanikio.

KABLA YA KUFIKIWA NA TASAF

Sakina kwa bahati mbaya, mwaka 2013 alifiliwa na mume wake, aliyemuachia watoto sita, wakati huo wakiishi kwenye nyumba ya miti na makuti.

Matunzo ya watoto hao, anakumbuka kuyapata ndani mwezi mmoja, baada ya kufiliwa na muumewake, ingawa kuanzia hapo, hakuna tena mchango hata wa kupata majani ya chai kutoka kwenye familia.

Hadithi ikawa kwake yeye ni mgagaa na upwa hali ugali mkavu, ingawa baadhi ya siku, akiukosa hata huo mkavu kula na watoto wake sita mayatima.

Haki ya elimu kwa watoto, ilikuwa ni ya kusua sua, mara wasimamishwe mara waruhusiwe kutokana na kutokuwa na uhakika wa mchango hata wa shilingi 100.

Baada ya kuondokewa na mume wangu, kazi sasa ilikuwa ni kuuza maandazi na maziwa eneo la soko la samaki Tumbe, ingawa kipato kilikuwa kidogo.

‘’Nikilimaliza bidhaa hizi, ilikuwa faida haizidi shilingi 4000, wakati ndani nna watoto sita, wanaohitaji mlo wa asubuhi pekee ni shilingi 6,000 kwa siku,’’anasema.

Alikuwa akimaliza bidhaa hiyo, miguu yake huelekea baharini kuungana na wenzake, kwenye kilimo cha mwani ambapo kwa wakati huo, kilo mmoja mkavu ni shilingi 300.

Hata alipojiunga kwenye kilimo cha mwani, anasema hakumbuki hata siku moja, watoto wake waliokula wakibakisha chakula kwenye dishi.



‘’Mimi ili nishibe vyema na watoto wangu, kuanzia asubuhi hadi jioni, ilikuwa nahitaji shilingi 1,5000 kwa siku, ingawa nilikuwa natimiza shilingi 5000,’’anasimulia.

Sakina hakumbuki watoto wake kuvaa nguo mpya hata siku za sikukuu, na siku moja baada ya kukosa cha kuvaa, aliwatembeza watoto wake soko la samaki Tumbe, baada ya kukosa hata nguo za mtumba.

‘’Wao hawakujua kwa sababu gani, tunakwenda kutembea sokoni, badala ya eneo letu la kusherehekea sikukuu, lakini ilitokana na kukosa nguo,’’anasilimulia.

Hakuwa na ndoto hata siku moja, kupata chakula cha kutosha, kutimiza ada ya skuli ya watoto wake, au kufikia sikukuu wakavaa nguo za dukani kama wenzao.

BAADA YA UJIO WA TASAF

Sakina anakiri kuwa, hakuamini alipoitwa na sheha wake, juu ya kurodhesha majina ya watoto wake, na taarifa nyingine za maisha, akiona kama ni mchezo.

Alikuwa na hakika kuwa, hakuna mpango wa kunusuru kaya maskini, ambapo anaweza kulipwa fedha na pasi na kufanya kazi.

‘’Ukishakuwa na watoto yatima na hali yako ikiwa ya kinyonge, atakuja huyu kukuandika, yule kukupiga picha na kisha mwisho wa siku, hakuna jambo,’’anakumbuka.

Baada ya TASAF kuitia roho na kuitwa jina lake kwa ajili ya kupokea, hakuamini moyo, macho na hisia zake kuwa amepata ruzuku hiyo.

‘’Siku ya mwanzo nilipokea shilingi 48,000 na nilielezwa ni kwa ajili ya watoto, iwe katika elimu ya skuli au huduma za afya, na hapo ndio nikaanza kuamini,’’anasema.

Sakina ambae yumo kwenye wale walengwa 14, 280 wa Pemba kuanzia mwaka 2014 hadi mwaka 2019, anakumbuka fedha hizo, hakufanya kosa na aliwanunulia vifaa vya elimu watoto wake.

Kuanzia hapo, watoto wake ilikuwa hawaendi skuli na sare mbovu, viatu visivyofahamika na hakuna siku waliyorejeshwa kwa ukosefu wa michango wa skuli.

Alidumu kwa miezi mitatu kupokea shilingi 48,000, ingawa baada ya kukiuka masharti, alipokea ruzuku ya shilingi 36,000 kutoka TASAF.

MRADI WA KUKAANGA SAMAKI

 ‘’Nikiwa napokea shilingi 36,000 sasa nikamua niende bandirini Tumbe, kununua samaki wa shilingi 10,000 kwa ajili kukukaanga na na mafuta ya shilingi 200 na baada ya kuuza, nilipata faida ya shilingi 5000,’’anasema.

Mlengwa huyo, kazi hiyo ilimgia gegoni sawa sawa, na kuanzia mwaka 2000, akawa ananunua samakini wa shilingi 45,000 hadi shilingi 50,000.

‘’Huku watoto wangu wakiwa wanakwenda skuli kama kawaida, na biashara yangu iling’aa, na sasa hadi kufikia kujipatia faida ya shilingi 15,000 kwa siku kutoka ile shilingi 5000 ya zamani,’’anasema.



GENGE

Hapa, baada ya kujikusanyia faida hadi kufikia shilingi 50,000 huku akiendelea kuwahudumia watoto wake sita mayatima, alizaa wazo la kuanzisha genge.

Genge hili aliamua kuuza bidhaa kama tungule, bilingani, bizari, nazi ingawa halikudumu, kutokana na kutokuwa na nafasi ya kuwepo nyumbani.

‘’Asubuhi nafuata samaki sokoni Tumbe, wakati huo huo natakiwa nikafuatilie viungo vya mchuzi mjini, nikaona siwezi kujigawa, hivyo baada ya muda genge niliacha,’’anasema.

Fedha alizoanzia genge na faida anayoendelea kuipata kwenye samaki wa kukaanga, hadi inalifikia shilingi 20,000 sasa alizaa mradi mwengine.

Ingawa pembeni ya miradi hii, Sakina alikuwa akiendesha mradi mwengine, wa kununua na kuuza sabuni za karafuu, akisema mwenyewe kwa ajili ya chai ya watoto.

‘’Nilidumu nao kwa muda wa zaidi ya miaka mitatu, lakini huu ulikuwa ni baada ya saa za kazi, lakini hata navunja kisanduku mlikuwa na shilingi 200,000,’’anasema.

MRADI WA NGUO ZA MITUMBA

Hapa, faida ya sabuni ya shilingi 200,000 ndio alioanza kununua nguo za mitumba kutoka Kenya, ambapo alimtuma mtu aliyekuwa kuweko kwa shughuli za uvuvi.

‘’Kwa sasa nimeshaolewa, na mume wangu alipofika Kenya wakati anataka kurudini mwezi Disemba mwaka 2021, ndie niliemuagiza na sasa naendelea na biashara hii hapa kwangu,’’anasema.

Mara ya kwanza, alipotuma shilingi 200,000 kwa bidhaa hiyo, alijipatia faida ya shilingi 40,000 na sasa kwa mara ya pili, alituma tena shilingi 400,000 ambapo hadi mwezi Aprili akiendelea kuuza.

Kwa sasa anamiliki wastani wa shilingi milioni 1 kama mtaji, na hasa baada ya kujiingiza kwenye kisanduku (kikoba), ambapo mwezi Machi mwaka 2022, alikopa shilling 300,000.

MALENGO YAKE

Tayari ameshanunua kiwanja kutoka kwa familia, na hapo baadae anajipanga kuanza ujenzi, ili aondokane na kodi ya mlango kwenye biashara yake.

Kwa sasa anaishi kwenye maisha ya ubinaadamu na furaha, na hasa baada ya kuwaona watoto wake wanaendelea na masomo.

KATIBU WA SHEHA

Katibu wa sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki, Makame Hassan Makame, anasema wapo wananchi 20 waliomo kwenye mpango, ambao sasa wamejiongeza.

Maana shehiani hapo, kati ya wananchi 7,675 waliofikiwa na mpango wa kunusuru kaya maskini walikuwa ni 231, ingawa kwa sasa wanaoendelea ni 225, akiwemo Fatma Rubea Ali.

Wapo walioanzisha ushirika wa biashara kilimo cha mboga, ufugaji vikundi vya kuweka na kukopa.

Lakini, akasema ipo miradi kadhaa ambayo inawalenga jamii wote, kama vile ujenzi wa tuta la kinga maji, ambapo wakulima zaidi ya 45, wamenufaika.

“Wakulima 45 walishayahama mashaba yao kwa kuingia maji ya bahari, lakini TASAF ilianzisha mpango wa kujenga tatu la kukinga maji, na sasa wakulima wamerudi,’’anasema.

Akaiomba TASAF, mara itakapomalizika mpango huo kwa awamu ya kwanza, bado kwenye shehia yake, anao zaidi ya wanachi 200 wanaohitaji kunusuriwa.

MUUME WA SAKINA

Kwana hakupenda jina lake lichapishwe, ingawa anasema mke wake sasa anamuona kama mfalme kwenye maisha yake.

‘’Hata namma ya kumshirikisha kwa kila jambo langu la maisha, sasa najiona liko juu, maana amekuwa mtunza fedha na mtumiaji mzuri,’’anasema.

Kwake sasa hana wasi wasi wa huduma za ndani, maana mke wake amekuwa akitoa zaidi ya asilimu 60 ya kukamilisha huduma za kila siku.

TASAF

Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said, anasema wapo walengwa 14, 280 kwa Pemba, ambao wanaendelea kupata fedha za kunusuriwa na umaskini.

Walengwa hao wapo kwenye shehia 78, ikiwemo ya Tumbe Mashariki, ambapo tayari shilingi bilioni 14. 4 zimeshwafikia.

Mtu kama Fatma, ndio hasa malengo ya TASAF ya kumtoa mwananchi katika unyonge, na kumleta kwenye taa, ili nae aishi maisha mazuri.

“TASAF inaorodhesha ya zaidi ya walengwa 50,000 kutoka wastani wa walengwa 15 kila shehia, kati ya shehia 78, ambao wamenzisha miradi ya kujikwamua.

“Mtu kama Fatma wa Tumbe, Amina wa Mgogoni, Mfaki wa Kwale Gongo na Maryam wa Ukunjwi ambao hatuna shaka, hawawezi kurudi tena kwenye umaskini mzito, wanafikia 50,000 kwa Pemba yote,’’anaeleza.

Mratibu Mussa anabainisha kuwa, kwa mwaka 2014 hadi 2015 walengwa hao wa kunusuru kaya maskini, waliibua miradi ya kijamii 41, idadi iliongozeka mwaka uliofuata, kwa kufikia miradi 84.

Mwaka 2017 hadi mwaka 2018, walijukuta na miradi mengine ya kijamii 21, inayuhusisha upandaji miti kama vile Makangale, uazishwaji wa vitalu na ujenzi wa matuta ya kinga maji ya bahari Ndagoni, Kiwani, Micheweni na Tumbe.

Achia mbali idadi ya watu 50,000 waliojiwekeza wenyewe, vipo vikundi 942 vikizaa walengwa 12,000 vilivyoanzishwa, kuanzia mwaka 2014 hadi sasa.

WANANCHI WA KAWAIDA

Fatma Hamad Mkandi, wa Tumbe anasema fedha zilizoekezwa kunusuru kaya maskini, zimetumika vizuri kwa vile matunda yanaoonekana.

Hassan Haji Omar, anasema kilichobakia sasa ni tasisi nyingine kuvilea vikundi hivyo, ili walengwa wake wasirudi tena kwenye umaskini.

‘’Kwetu sisi Sakina tumeshamuona kama mwanamke mwenye uwezo mkubwa, sasa maana ruzuku ya TASAF aliitumia kama inavyotakiwa,’’anasema.

                     Mwisho           

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch